Maoni na Msimamo wa Baraza la Katiba la Wasanii

Maoni na Msimamo wa Baraza la Katiba la Wasanii

Wasanii walotoa maoni niwale wa vinyango na wachoraji sio bongo movie wala bongo flava

Hata hao wa bongo movie unadhani watachangia nini cha maana? mtu kama ray au dr cheni unadhani kuna wanacho kijua? au diamond au shilole wataongea nini?
 
wamesahau

1. Katiba ikataze uvaaji wa suruali chini ya makalio.

2. Katiba ikataze filamu na tamthilia zinazohamasisha ngono. (uvaaji nusu uchi).

3. N.k

aswaaaa
 
Wamesahau

1. Katiba ikataze uvaaji wa suruali chini ya makalio.

2. Katiba ikataze Filamu na Tamthilia zinazohamasisha ngono. (Uvaaji nusu uchi).

3. N.k

au kushika sehemu ya ' babu ' wanapokuwa jukwaani .
 
Naiona taswira fulani katika hicho kinachoitwa Baraza la Katiba la Wasanii,

Mda ukifika mtaona rangi yake halisi,

Watanzania kuweni makini sana katika hivi vinavyojiita "makundi maalumu", vingine ni makundi maalumu kweli kweli kwakuwa yanawakilisha wahuni wawili ama watatu wenye agenda pana zaidi,

Nawaasa ndugu zangu, kuweni na macho manne kila ukionapo kitu kinachojiita "kinawakilisha watu flani"

Ukistaajabu ya CCM utayaona ya Januari Makamba

mkuu sijawahi kukupuuza hata mara moja .
 
....Hayo ni maneno yako si yangu,lakini kwa maelezo ya mleta mada utagundua kabisa kwa nini kazi za wasanii wetu ni viwango duni,uwezo wao ni mdogo sana kiakili, by the way huwezi kumfananisha sugu na wasanii wa kileo eti mr.blue,nyandu tozi,kala jeremiah,chid benz ha ha ha these guys are too low.

Tofauti ya Sugu na hao wengine ni nini?
 
Hii Katiba siyo ya vyama vya siasa.
 
Inawezekana kweli wengi humu ni low in thinking.
Kwanza jifunz kuheshimu mawazo ya wengine
pili tambua uwepo wa makundi/ sekta tofauti ndani ya jamii.

kisha kumbuka kuwa hakuna aliy juu zaidi ya mwingine.

mmesema wengi humu kuwa maoni yetu tuliyatoa tukiwa tumepata viloba n.k. Lakini niwahakikishie tulijadili mengi ktk utamaduni na sanaa ambayo wengi wenu hamkuyaona. Ni wasanii hawa hawa ambao kwa unyong wao walipambana na mfumo hadi kutungwa kwa sheria ya HAKIMILIKI HAKISHIRIKI. Hakukuwpo na support ya kijamii ktk hili. Tuliishinikiza serikali hadi ikakubali uwepo wa sheria hiyo. Hata wanasheria na watunga sheria hawakuliona hili kabla.

Sisi ni kundi ndani ya jamii na tumetumia fursa iliyopo kutoa maoni. HATUBURUZWI na mitizamo yenu na tunatambua wajibu na thamani yetu.
 
Inawezekana kweli wengi humu ni low in thinking.
Kwanza jifunz kuheshimu mawazo ya wengine
pili tambua uwepo wa makundi/ sekta tofauti ndani ya jamii.

kisha kumbuka kuwa hakuna aliy juu zaidi ya mwingine.

mmesema wengi humu kuwa maoni yetu tuliyatoa tukiwa tumepata viloba n.k. Lakini niwahakikishie tulijadili mengi ktk utamaduni na sanaa ambayo wengi wenu hamkuyaona. Ni wasanii hawa hawa ambao kwa unyong wao walipambana na mfumo hadi kutungwa kwa sheria ya HAKIMILIKI HAKISHIRIKI. Hakukuwpo na support ya kijamii ktk hili. Tuliishinikiza serikali hadi ikakubali uwepo wa sheria hiyo. Hata wanasheria na watunga sheria hawakuliona hili kabla.

Sisi ni kundi ndani ya jamii na tumetumia fursa iliyopo kutoa maoni. HATUBURUZWI na mitizamo yenu na tunatambua wajibu na thamani yetu.

Naomba kufahamishwa zaidi,wasanii ndiyo walipambana kuleta sheria ya hati miliki peke yao ama? Pia uwepo wa sheria ya hati miliki,wasanii wamefaidika kwa kiwango gani tofauti na wakati haikuwepo?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Naomba kufahamishwa zaidi,wasanii ndiyo walipambana kuleta sheria ya hati miliki peke yao ama? Pia uwepo wa sheria ya hati miliki,wasanii wamefaidika kwa kiwango gani tofauti na wakati haikuwepo?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
Ni kwamba Kwa sehemu kubwa wasanii walishirikiana kuishinikiza serikali kutunga sheria ya HakiMiliki na HakiShiriki. World Intellectual Property Organization (WIPO) ilishiriki kuisukuma hoja ya kuundwa sheria husika.

Faida za kuwepo kwa sheria tajwa ni pamoja na kupitishwa na kutekelezwa kwa kanuzi za ukusanyaji wa MIRABAHA ya matumizi ya kazi za sanaa. Hapo awali hadi sasa zoezi la kusajili kazi za wasanii linaendelea ili kuweza kusimamia mgawanyo wa haki za wasanii kwa mujibu wa sheria. Pia sheria imeendelea kupunguza uharamia wa kazi za wasanii ingawa kuanzia mwaka 2009 serikali kupitia Waziri Nagu (Viwanda na Biashara) ilianza kujiweka mbali na utekelezaji wa sheria yenyewe hali iliyopelekea wizi kushamiri upya na sasa kupitishwa sheria ya utoaji wa stika maalumu kwa kazi za sanaa unaoendeshwa na TRA ambapo MSANII ameminywa haki zake na mapato kugawanywa baina ya msambazaji na serikali pekee. Awali wasimamizi wa sheria hii COSOTA waliandaa kanuni tangu mwaka 2007 inayohusu matumizi ya stika maalumu na namna mapato yake yatakavyogawanywa. Ila Waziri hakuipitisha kanuni hiyo na bahati mbaya hakukuwepo na juhudi za dhati wizarani kuiridhia hiyo kanuni hadi iliponyakuliwa na wizara ya Fedha na kuletwa rasmi bungeni ili ianze kutumika 2013/2014.

Tukirejea kwenye hoja ya KATIBA MPYA.

Wasanii waliona kuna mapengo ya wazi kabisa kuhusu utamaduni kutamkwa kama ni mojawapo ya utambulisho wa Mtanzania na nchi ulimwenguni. Na pia tulipendekea kuondoshwa ibara inayotamka matumizi ya kiingereza kwani Katiba imeshatamka kwamba lugha ya Taifa ni Kiswahili. Na yamekuja mapendekezo namna ya kusimamia, kulinda na kuendeleza kiswahili ili kukipa chapuo ulimwengun. Kuna mapendekezo kuhusu wageni na wawekezaji kuweza kuwa proofed na proficiency ya kiswahili wanapokuwa ktk harakati zao za uwekezaji kwani inaonesha kwamba uwekezaji wa kwenye ardhi huko vijijini kumekuwa na sintofahamu kubwa kutokana na barrier ya lugha hasa kwa Watanzania walioko huko.

Kwenye mahakama, sote tunafahamu kwamba lugha ya kiingereza imekuwa ikitumika kurekodi daawa (kesi) na mara nyingine nakala za hukumu zinazoandikwa kwa lugha hiyo zimekuwa zinawanyima haki Watanzania waliohukumiwa ama walio na nia ya kukata rufaa hivyo tumeshauri lugha ya kiswahili itumike kwenye vyombo vya kutoa haki.

Kuna lingine ambalo NINYI WANASIASA hamkulizungumzia katu. Nalo ni la uhifadhi na ulinzi wa KATIBA. Viongozi wakuu wa nchi wanapoapa kulinda katiba imeonekana kwamba kuna haja ya kuwepo na chombo huru kitakachosimamia hilo. Tumeshuhudia katiba imevunjwa mara kadhaa ambapo 2010 baada ya uchaguzi mkuu, rais wa Zanzibar Aliapishwa huku akiwa hajakoma kuwa Makamu wa Rais wa Muungano. Hivyo uwepo wa chombo huru cha kuhifandi na kulinda KATIBA kutatoa nafasi kwa viongozi kuwajibika zaidi wanapotekeleza majukumu yao bila kuvunja katiba. Chombo hicho kipewe uwezo kisheria kumhoji na kuchungua madai yoyote ua uvunjwaji ama uchezewaji wa katiba na kikiridhika kuwa kuna makosa, kiandae mashtaka ya mhusika na kupeleka bungeni ambapo Spika hatokuwa na veto ya kuzuia kujadiliwa hoja hiyo na taratibu za kumshati na kumchunguza mhusika kuendelea hadi maamuzi ya haki kutolewa bungeni.

Wasanii pia waliona kuna haja ya kuwa na serikali moja kwani, uwepo wa serikali mbili ama tatu hakuepuki matumizi ,akubwa ya kuendesha serikali hizo. Pia kuwepo na migogoro ya kimamlaka hakujaepukika tangu mwanzo hadi sasa Zanzibar imeshapiga hatua ndefu kuelekea dola kamili. Hivyo badala ya kukwepa tatizo na kufufua serikali ya Tanganyika, basi iwezekane tukaudumisha muungano kwa kuondoa mamlaka za serikali mbili ama tatu na kuweka serikali moja. Bunge la Seneti litakuwa bunge la juu ambapo bunge la Congress litakuwa la chini. Katiba hii itawezesha kutoa mwanya kwa nchi zingine kujiunga na Jamhuri ya Muungano kwa kuridhia kwenye mabunge yao katiba hii na kujiunga. Jeshi liwe moja. Kuhusu mahakama wasanii walishauri iwe ktk ngazi tatu.
  1. Mahakama ya juu,
  2. Mahakama ya Rufaa,
  3. Mahakama ya jimbo na Mwanzo.

Kuhusu Sarafu iwe moja na usimamizi wake uwe kama ifuatavyo.
  1. Benki Kuu (Muungano wa Benki kuu za Majimbo)
  2. Benki za Majimbo

Naamini ktk dodoso kuna mengi yatakayoelezwa na ninaahidi kuyaleta hapa endapo yatakuwa tayari ktk mfumo rasmi. #Justsaying
 
inaonekana palikuwa na wasanii kutoka Tanganyika tuu maana kutoka Zanzibery wangalikuwepo hili la Serikali moja linga piganisha watu
 
Msanii, Napata mashaka kama uwep wa sheria ya hati miliki umewafaidisha sana wasanii maana wanalia mno kuhusu kuibiwa kazi zao,hii inadhihirisha kuna walakini....kwa upande wa stika katika kazi za sanaa naona sekta italasimishwa kwa upande wa serikali kwa kuwa naona stika hizo zitauzwa kama stamp duty hivyo msambazaji atanunua na kubandika hata katika kazi haramu au utaratibu wa stika hizo upoje kwa wasambazaji?
 
Wasanii waliona kuna mapengo ya wazi kabisa kuhusu utamaduni kutamkwa kama ni mojawapo ya utambulisho wa Mtanzania na nchi ulimwenguni. Na pia tulipendekea kuondoshwa ibara inayotamka matumizi ya kiingereza kwani Katiba imeshatamka kwamba lugha ya Taifa ni Kiswahili. Na yamekuja mapendekezo namna ya kusimamia, kulinda na kuendeleza kiswahili ili kukipa chapuo ulimwengun. Kuna mapendekezo kuhusu wageni na wawekezaji kuweza kuwa proofed na proficiency ya kiswahili wanapokuwa ktk harakati zao za uwekezaji kwani inaonesha kwamba uwekezaji wa kwenye ardhi huko vijijini kumekuwa na sintofahamu kubwa kutokana na barrier ya lugha hasa kwa Watanzania walioko huko.


Hawa kweli ni Wasanii ................. tayari wananichanganya!! Msanii na wewe ni mmoja wao ama!!??
 
Last edited by a moderator:
ni kwamba kwa sehemu kubwa wasanii walishirikiana kuishinikiza serikali kutunga sheria ya hakimiliki na hakishiriki. World intellectual property organization (wipo) ilishiriki kuisukuma hoja ya kuundwa sheria husika.

Faida za kuwepo kwa sheria tajwa ni pamoja na kupitishwa na kutekelezwa kwa kanuzi za ukusanyaji wa mirabaha ya matumizi ya kazi za sanaa. Hapo awali hadi sasa zoezi la kusajili kazi za wasanii linaendelea ili kuweza kusimamia mgawanyo wa haki za wasanii kwa mujibu wa sheria. Pia sheria imeendelea kupunguza uharamia wa kazi za wasanii ingawa kuanzia mwaka 2009 serikali kupitia waziri nagu (viwanda na biashara) ilianza kujiweka mbali na utekelezaji wa sheria yenyewe hali iliyopelekea wizi kushamiri upya na sasa kupitishwa sheria ya utoaji wa stika maalumu kwa kazi za sanaa unaoendeshwa na tra ambapo msanii ameminywa haki zake na mapato kugawanywa baina ya msambazaji na serikali pekee. Awali wasimamizi wa sheria hii cosota waliandaa kanuni tangu mwaka 2007 inayohusu matumizi ya stika maalumu na namna mapato yake yatakavyogawanywa. Ila waziri hakuipitisha kanuni hiyo na bahati mbaya hakukuwepo na juhudi za dhati wizarani kuiridhia hiyo kanuni hadi iliponyakuliwa na wizara ya fedha na kuletwa rasmi bungeni ili ianze kutumika 2013/2014.

Tukirejea kwenye hoja ya katiba mpya.

Wasanii waliona kuna mapengo ya wazi kabisa kuhusu utamaduni kutamkwa kama ni mojawapo ya utambulisho wa mtanzania na nchi ulimwenguni. Na pia tulipendekea kuondoshwa ibara inayotamka matumizi ya kiingereza kwani katiba imeshatamka kwamba lugha ya taifa ni kiswahili. Na yamekuja mapendekezo namna ya kusimamia, kulinda na kuendeleza kiswahili ili kukipa chapuo ulimwengun. Kuna mapendekezo kuhusu wageni na wawekezaji kuweza kuwa proofed na proficiency ya kiswahili wanapokuwa ktk harakati zao za uwekezaji kwani inaonesha kwamba uwekezaji wa kwenye ardhi huko vijijini kumekuwa na sintofahamu kubwa kutokana na barrier ya lugha hasa kwa watanzania walioko huko.

Kwenye mahakama, sote tunafahamu kwamba lugha ya kiingereza imekuwa ikitumika kurekodi daawa (kesi) na mara nyingine nakala za hukumu zinazoandikwa kwa lugha hiyo zimekuwa zinawanyima haki watanzania waliohukumiwa ama walio na nia ya kukata rufaa hivyo tumeshauri lugha ya kiswahili itumike kwenye vyombo vya kutoa haki.

Kuna lingine ambalo ninyi wanasiasa hamkulizungumzia katu. Nalo ni la uhifadhi na ulinzi wa katiba. Viongozi wakuu wa nchi wanapoapa kulinda katiba imeonekana kwamba kuna haja ya kuwepo na chombo huru kitakachosimamia hilo. Tumeshuhudia katiba imevunjwa mara kadhaa ambapo 2010 baada ya uchaguzi mkuu, rais wa zanzibar aliapishwa huku akiwa hajakoma kuwa makamu wa rais wa muungano. Hivyo uwepo wa chombo huru cha kuhifandi na kulinda katiba kutatoa nafasi kwa viongozi kuwajibika zaidi wanapotekeleza majukumu yao bila kuvunja katiba. Chombo hicho kipewe uwezo kisheria kumhoji na kuchungua madai yoyote ua uvunjwaji ama uchezewaji wa katiba na kikiridhika kuwa kuna makosa, kiandae mashtaka ya mhusika na kupeleka bungeni ambapo spika hatokuwa na veto ya kuzuia kujadiliwa hoja hiyo na taratibu za kumshati na kumchunguza mhusika kuendelea hadi maamuzi ya haki kutolewa bungeni.

Wasanii pia waliona kuna haja ya kuwa na serikali moja kwani, uwepo wa serikali mbili ama tatu hakuepuki matumizi ,akubwa ya kuendesha serikali hizo. Pia kuwepo na migogoro ya kimamlaka hakujaepukika tangu mwanzo hadi sasa zanzibar imeshapiga hatua ndefu kuelekea dola kamili. Hivyo badala ya kukwepa tatizo na kufufua serikali ya tanganyika, basi iwezekane tukaudumisha muungano kwa kuondoa mamlaka za serikali mbili ama tatu na kuweka serikali moja. Bunge la seneti litakuwa bunge la juu ambapo bunge la congress litakuwa la chini. Katiba hii itawezesha kutoa mwanya kwa nchi zingine kujiunga na jamhuri ya muungano kwa kuridhia kwenye mabunge yao katiba hii na kujiunga. Jeshi liwe moja. Kuhusu mahakama wasanii walishauri iwe ktk ngazi tatu.
  1. mahakama ya juu,
  2. mahakama ya rufaa,
  3. mahakama ya jimbo na mwanzo.

kuhusu sarafu iwe moja na usimamizi wake uwe kama ifuatavyo.
  1. benki kuu (muungano wa benki kuu za majimbo)
  2. benki za majimbo

naamini ktk dodoso kuna mengi yatakayoelezwa na ninaahidi kuyaleta hapa endapo yatakuwa tayari ktk mfumo rasmi. #justsaying
napata halufu ya ujinga hapo katika hoja hizi
 
Hadi sasa hali halisi ni kwamba Wanasiasa wameuteka mchakato wa Katiba Mpya.
Tutakuja kujuta huko mbeleni
 
Back
Top Bottom