Mheshimiwa Rais, salaam!
Umeingia madarakani ukiwa na lengo la kuwatumikia Watanzania kwa kuona wanaishi maisha bora na salama.
Lengo hilo limetokana na fursa ya raslimali nyingi zilizopo hapa nchini hivyo wewe kuamini kwamba hakuna sababu ya Watanzania kulia na umaskini kwa kua raslimali hizi zikisimamiwa vizuri zinaweza kunufaisha kila raia wa nchi hii.
Naamini Kuna mpango kazi ambao umejiwekea (priorities) kufikia ndoto ya Tanzania unayoitarajia.
Tukirudi nyuma, tawala zilizopita kuanzia awamu ya kwanza mpaka ya nne Kuna mema zimefanya na Kuna mabaya pia yalifanyika.
Ndugu Rais, baadhi ya wadau wakiwemo na wanasiasa wanataka ufanyie kazi tuhuma mbali mbali za awamu zilizopita, za ubadhilifu wa Mali ya umma.
Kwangu mimi kazi hii ni ngumu sana na ni mtego wa kuhakikisha hufanikiwi katika malengo yako, Kwani muda mwingi utabaki kushughulikia kashfa zilizopita badala ya kuwaletea Watanzania maendeleo.
Huu ni utawala mpya wa awamu ya tano, unavipaumbele vyake.
Nashauli kama ni masuala ya ufisadi hakikisha hayafanyiki kwenye utawala wako kwa kuibana mianya yote ya ufisadi kama mkuu wa nchi, ikiwemo kuengua watumishi wasio waaminifu na kuweka wazalendo zaidi kwenye serikali yako, japo si jambo jepesi kutokana na utamaduni wa watumishi wetu, wa business as usual.
Jukumu la kulinda na kurejesha raslimali za nchi hii ni za Watanzania wote. Wanaharakati, mahakama kama muhimili upo, bunge lipo. ni kazi ya wananchi wenye ushahidi wa tuhuma hizo kuzipeleka maeneo husika kwa ajili ya hatua stahiki, na si kila jambo Magufuli fanya hivi, fanya vile.
Ikizingatiwa hayakufanyika chini ya utawala wako.utakachotakiwa ni kuwa transparent kwa kutoingilia mihimili iliyopo kwa mujibu wa katiba.
Nashauri bana kuanzia sasa, siku hazigandi.