Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
SERIKALI HAINA DINI

Post sent using JamiiForums mobile app
 
SERIKALI HAINA DINI

Post sent using JamiiForums mobile app

  1. Mwulize JJPM aliapa kwa kutumia kitabu cha dini gani?
  2. Mwulize JJPM huwa anaenda kusali kanisa gani
  3. Anapowaambia Watanzania tumwombee kupitia dini gani?
Kwa kifupi sana Serikali haina dini lakini Watawala wana dini zao.
Adios!
 
MUDA UTAONGEA...
 
Ashasema hapangiwi cha kufanya. Anajiona mungu mtu.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Kwa akili za kawaida tu ni kwamba huyu jamaa hana dini bali anatumia mwavuli wa dini.

Pili upinzani wa sasahivi siuelewi kabisa, I think Jamaa wa chato ni mchawi balaa, I mean katuroga wote. Maaskofu wamenywea, Mashehe wameshazibwa midomo, wafanyakazi na vyama vyao chali, Upinzani ndo tayari kabisa. Yamebaki matamko, leo tamko hili kesho lile. Mara fulani kawekwa ndani, Mara fulani anahojiwa.

Tunapoelekea MAGU atateua mpaka wenyeviti wa vyama siasa na wafanyakazi na hakuna atakayefungua domo.
 
Mwenzio lema aliota akiwa anawasiliana na Roho Mtakatifu mambo yajayo kumhusu huyo mtakatifu uliyemtaja lakini yalimkuta ya kumkuta. Shauri yako ndugu yangu. Kuna noah made in callmej ziko barabarani

Post sent using JamiiForums mobile app
 

Brother,
Looks like you're talking!! Kama ni hivyo basi inawezekana kweli jamaa anatumia ndumba kweli!! Huku kujiamni kwake si kwa mtu anayemtegemea Mungu!!!!
Lakini ngoja niseme mimi kama mtu ninayemtegemea na kumwamini Mungu wa kweli, hakujawahi kutokea NGUVU ZA GIZA ZIKASHINDANA NA NGUVU ZA MUNGU!! NEVER. Kama ni kweli huyu Rais anatumia nguvu za giza surely Mungu hayuko pamoja naye na atakuwa na anguko baya sana huko mbele. Mungu hadhihakiwi!!!!
 
Kuna mambo yupo sahihi na ukweli bila unafiki nakubaliana naue kabisa lakin kuna mengi ana enda kinyume nyume akirekebisha atakuwa rais bora kwangu 100%

1. Akubali kukosolewa na kukosoleka
2. Aamini kuwa yeye ni kiongozi na sio mtawala
3. Awe na lugha na matendo yanayo waunganisha watanzania bila kujali vyama,imani na makabila yao.
4.apuunguze chuki za wazi hasa kwa makundi anayo dhani hayamuungi mkono na aondoe upendo wa wazi kwa makundi anayo dhani yanamuunga mkono
5. Awe na roho ya kujali makundi yote na kuona kila kundi lina umuhimu kwa taifa mf. Wahanga,watumishi,wakulima,wafugaji,watoto,vijana , wanawake,walemavu, wazee na makundi mengine yooote
6.asimuone kiongozi fulani ni muhimu kuliko wengine ,woote wawe sawa mbele zake wakikosea waonywe wote na wakiweza wasifiwe wote kwa usawa.
Hayo 6 tu kwangu mimi ndio yanayo nifanya niwe nae kwa 50%
Nasisitiza kwangu mimi sijamsemea yeyote ila unaruhusiwa kuniunga mkono na kunipinga pinga pia
 
Hayo 6 huwezi yapata toka kwa JPM!Unatafuta mvua jangwani ndugu!
Hahahaaaaaaa!! Kwakweli kwangu mimi madhaifu niliyo yaona kwake ni hayo tuu na naona akiyarekenisha hayo tuuuu !! Mimi nitapambana vikali na watakao msema vibaya
 
Unadhani akifanyia kazi tamaa za kila mtu atakuwa bado na sifa za kuitwa kiongozi?

Post sent using JamiiForums mobile app
 

Mimi langu namba 7 (lenye vipengele viwili) kuongezea hayo uliyosema ni kama ifuatavyo:
(i) Aendeleze mchakato wa katiba ya Warioba na kutupilia mbali ile iliyoitwa "pendekezwa" baada ya kuchakachuliwa na chama chake cha CCM.
(ii) Muendelezo wa katiba ya Warioba uhakikishe kipengele cha tume huru ya uchaguzi hakichakachuliwi na pia Wabunge wapewe haki ya kuendelea na ubunge wao hata kama watafukuzwa vyama vyao. Kwa maana nyingine, wabunge wawe huru, ili hatimaye tuwe na bunge lenye meno na sio hili kibogoyo la sasa lililojaa wagonga meza waoga. Hapo Magu atakuwa wangu 90% (kuna mengine sijasema ndio maana natoa 90%).
 
Mkuu unapoteza muda wako bure, huyu mtu hashauriki

Post sent using JamiiForums mobile app
 
La nane ......
8. Asiwe juu ya sheria. Awe mfano wa kufuata katiba ya nchi, sheria na maadili yote.
9. Atumie lugha ya kirais
10. Aache kuwaonea wapinzani na kuwatesa kuna kesho na kesho kutwa.
 
Mkuu nipe ruhusa niliongeze hili kwenye uzi ni muhimu sana sana asante kunikumbusha hasa hilo (i)
 
Kwa utafiti mdogo nilio ufanya, Nimefahamu kuwa wanao lichelewesha taifa hili kusonga mbele kwa haraka ni wazee walioko kwenye taasisi na mashirika ya umma. Wengi wao wanafanya kazi kwa mazoea na kutoweza endana na kasi ya serikali yako..hivyo basi fukuza wote ikiwezekana umri wa kustafu kazi uwe miaka 45.

Ajiri vijana wengi uwezavyo..hawa wana nguvu na ari ya kufanya kazi kwa bidii..na wana uwezo wa kwenda na kasi ya serikali yako. Hivyo basi hata dhana ya viwanda itafanikiwa kwa kiasi kikubwa. Nawasilisha
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…