Nikujibu ili iweje? Nipoteze muda wangu kujibu mtu mwenye mawazo ovu? Hata sasa nimeheshimu hisia zangu kuandika haya...Hustahili majibu yangu wewe!Hujajibu nikichouliza na ulichojibu sijauliza.
Kwa msingi huu nakubali hamuendi popote.
Mtabaki kwenye umasikini, maradhi na ujinga.
Mkuu utaua.Katiba tunayo na hatuifuati...
Tumeirekebisha na tukaikacha, tukarejelea ile ambayo tuliona haitufai...
Nchi ni ya vyama vingi na bunge ni la vyama vingi lakini bado maamuzi yake ni ya chama kimoja (mtindo wa wengi wape)...Kifupi tuna mfumo unaojichanganya changanya
Akiondoka Magufuli atayefuata baada yake naye atakuja na mambo ya kwake, usishangae naye akaja kumponda Magufuli na wananchi tutashangilia...
Sasa mbona unaendelea kujibizana na mtu mwenye "mawazo ovu"?Nikujibu ili iweje? Nipoteze muda wangu kujibu mtu mwenye mawazo ovu? Hata sasa nimeheshimu hisia zangu kuandika haya...Hustahili majibu yangu wewe!
Nimezungumzia suala la kupendwa au suala la watu kuonekana kufurahia na kuombea rais akutwe na umauti?! Hata JK watu walikuwa hawampendi lakini hatukuwahi kushuhudia haya!! Hizi kauli za kwamba sijui "mtenda haki", sijui nini na nini ni kujaribu kufanya ujanja wa mbuni, kuficha kichwa chini wakati kiwili kiwili kinaonekana!!!Duniani kote, hakuna mkweli na mtenda haki akapendwa. Angalau Injili na Quran vinasema hivyo.
Yesu hakusulubiwa kwa vile alitenda uovu, mifano ipo mingi. Kama Mungu ni ukweli basi wengi wetu hatumpendi Mungu kwa yakini, tunazipenda nafsi zetu ambazo zimejaa uovu, dhuluma na unafiki.
Anayeitaka haki ni lazima ajikane, sisi hatujajikana, bado hatujaweza kuuza tulicho nacho tumfuate.
Hata leo hii tunaulizwa, kati ya Baraba na Yesu nani asulubiwe, bila aibu tunasema Yesu.
Njia ya uzima haijanyoika, imejaa dhiki, mahangaiko na dhihaka. Raid Magufuli ni mtu wa haki, hana cha kujitafakari, atende kama alivyopanga kutenda, dunia haijawahi kubadilika, inapenda dhuluma kuliko haki.
Kila mmoja wetu anaifahamu nafsi take, kama ni ya dhulma au ya haki. Kwa lolote ulifikialo jiulize Mimi ni wa dhulma au wa haki halafu chukua hatua stahiki
Wengi wapi? Raia mmoja wa israel ni sawa na raia elfu nchi nyingine , hivyo jibu unalo hapo.Rudi kwenye mada... kwanini wengi wanaonekana kumuombea mabaya zaidi?!
Hao raia 1000 wa nchi nyingine ni wale wenye fikra kama za kwako! Na kama hujaona hao wengi, sorry, sina namna ya kukusaidia!!Wengi wapi? Raia mmoja wa israel ni sawa na raia elfu nchi nyingine , hivyo jibu unalo hapo.
Maisha au ulimwengu ni mzunguko, na watu hatufanani , hivyo zamu ya dhaifu imeshapita na , sasa ni zamu nyingine zamu ya kunyoosha hivyo watu watulie tu.Hii hoja ina ukosefu wa mantiki.
Inawezekana kabisa kiongozi mmoja akawa dhaifu sana, na kiongozi mwingine akawa mbabe sana, na kwa hiyo, wote wawiki wakakosa sifa za kiongizi mzuri.
Kwa sababu kiongizi mzuri anatakiwa asiwe dhaifu wala mbabe, awe anajua ku balance mambo.
Sasa mtu kama mimi nikisema Kikwete aliowaya jwa sababu alikuwa dhaifu sana na Magufuli anaowaya kwa sababu ni mbabe sana na tunahitaji kiongozi asiye dhaifu wala mbabe, utajibu vipi?
Kuna ubaya kwa wananchi kukosoa viongozi wao nankutaka uongozi bora zaidi?
Sijaomba kusaidiwa na wewe sorry ya nini sasa? Na ulichosaidia hapo sikioni , hahaha usijihami hao 1000 ndio nyie , asante kwa kujitambua.Hao raia 1000 wa nchi nyingine ni wale wenye fikra kama za kwako! Na kama hujaona hao wengi, sorry, sina namna ya kukusaidia!!
Mkishindwa msiwe mnatafutiza sababu ambazo hazipo.Kunyoosha mambo ni kunajisi box la kura?
Ni nani aliyetukuza watu wa taifa lingine kama sio wewe?! Sasa unakwepa vp kutoka kwenye hilo kundi lenu la watu 1000 mnaojiona si lolote si chochote mbele ya Mwisrael mmoja?!Sijaomba kusaidiwa na wewe sorry ya nini sasa? Na ulichosaidia hapo sikioni , hahaha usijihami hao 1000 ndio nyie , asante kwa kujitambua.
Hakuna kunyoosha bila viwango na nidhamu.Maisha au ulimwengu ni mzunguko, na watu hatufanani , hivyo zamu ya dhaifu imeshapita na , sasa ni zamu nyingine zamu ya kunyoosha hivyo watu watulie tu.
Mkishindwa msiwe mnatafutiza sababu ambazo hazipo.
Kumbe kulikua na nini ? Unaelialia oh wamenajisi oh nini , sema ueleweke.Kumbe kulikuwa na ushindani, ndio nasikia kwako, kwahiyo mlioshinda mmebeba kombe?
Na awamu ya dhaifu nayo uifafanue ehe kilitokea nini ?Hakuna kunyoosha bila viwango na nidhamu.
Ukitaka kunyoosha hivyo utaunguza. Maana hata pasi ina moto wake kwa nguo tofauti, sasa ukitaka kunyoosha nguo kwa kupandisha moto mpaka juu, wakati nguo ya nylon, utajikuta unaunguza nguo.
Hoja ya kunyoosha naielewa na nimeitaja hapo juu, kwamba kulikuwa na haja ya kunyoosha mambo fulani yaliachiwa sana.
Lakini, kunyoosha kuna lazimisha kutukana wananchi? Rais ni lazima awe na kauli mbovu ili anyooshe?
Hiyo anayenyoosha mwenyewe una hakika ananyoosha kweli au anacheza mchezo wa maigizo ya kunyoosha?
Mbona tunaambiwa kauzia nyumba za serikali mpaka kimada wake na ndugu yaje kinyume cha utaratibu?
Mbona anafanya manunuzi makubwa nje ya bajeti na bila kufuata utaratibu wa tenda wala ukaguzi wa mahesabu?
Akiwa anawapiga hela kubwa hapo, na kuwapa maigizo ya kunyoosha, mtajuaje?
Hakuna ulichonisaidia na sijakuomba kufanya hivyo , ukweli utabaki kuwa kweli na umeelewa kiroho safi , hayo maneno mengine ndio ya wale 1000.Ni nani aliyetukuza watu wa taifa lingine kama sio wewe?! Sasa unakwepa vp kutoka kwenye hilo kundi lenu la watu 1000 mnaojiona si lolote si chochote mbele ya Mwisrael mmoja?!
Btw, utasemaje nilichosaidia hukioni wakati nimekuambia wazi kwamba siwezi kukusaidia?! Ikiwa sentensi fupi kama hiyo umeshindwa kuelewa, hakika siwezi kushangaa unapojaribu kuweka rehani utu wako na wenzako mbele ya Mu-Israel 1!
Wapi nimekuambia nimekusaidia?! Ni kweli nimeelewa kuhusu wale 1000 manake mashabiki wengi wa Magufuli uelewa wenu ni finyu, ndo maana mnakidhi 1000 nyie kuwa sawa na Mwisraeli mmoja!!Hakuna ulichonisaidia na sijakuomba kufanya hivyo , ukweli utabaki kuwa kweli na umeelewa kiroho safi , hayo maneno mengine ndio ya wale 1000.
Chochote kikichotokea ni irrelevant kwenye point zangu ambazo hujazijibu.Na awamu ya dhaifu nayo uifafanue ehe kilitokea nini ?
Uzuri ni kuwa umeelewa kuwa ufinyu wa akili ni kubwabwaja na kuuliza mambo ya kuombeana ubaya, hivyo hao 1000 mmijitambua vizuri.Wapi nimekuambia nimekusaidia?! Ni kweli nimeelewa kuhusu wale 1000 manake mashabiki wengi wa Magufuli uelewa wenu ni finyu, ndo maana mnakidhi 1000 nyie kuwa sawa na Mwisraeli mmoja!!
Ukweli uko wazi , mambo yananyooshwa safi kabisa , na nidhamu ilioporomoka inajengwa na kizazi kijacho kitakula matunda yake , sasa hivi tunakula matunda ya zaifu.Chochote kikichotokea ni irrelevant kwenye point zangu ambazo hujazijibu.
1. Hakuna kunyoosha nchi bila viwango na nidhamu.
2. Magufuli si mtu wa kunyoosha nchi, anafanya maigizo ya kunyoosha nchi, kwa sababu, na yeye ni fisadi.
Huko kwa Kikwete kama kulikuwa na udhaifu, udhaifu huo hauondoi point zangu mbili za hapo juu.
Ukweli uko wazi , mambo yananyooshwa safi kabisa , na nidhamu ilioporomoka inajengwa na kizazi kijacho kitakula matunda yake , sasa hivi tunakula matunda ya zaifu.