Maoni ya Mtanzania anayeishi UK kuhusu kupanda kwa kodi za majengo

Ni kweli ni ndogo, fanya tafiti kwanza kwa nini imetoka 1500 hata mwaka haujaisha imepanda tena, hii inamanisha ni eneo potential kwa makusanyo ya kodi! Badara ya kuja na sera ya kila nyumba iwe na umeme kusudi ukusanye kikubwa bila hata ya kuongeza kiwango. Wewe unaongeza mzigo kwa wachache waliopo! Kwanini usiongeze kwa kuongeza idadi ya nyumba zenye umeme ili ukusanye pakubwa??? Unakuta kijiji kina kaya 800 ila zenye umeme ni kaya 200 tuu. Sasa unataka kuwabebesha mzigo wa kaya 800 kwa kaya 200 akili matope??
 
Kumbe anaishi marekani sasa atajuaje shida zetu? Kodi tunalia cha ajabu kila cku wanakopa
 
Hizo hela zisingekuwa zinatafunwa na watu wachache bila kuchukuliwa hatua yeyote labda hoja yake ingekuwa na mashiko na wananchi wangeelewa maana kinachofanyika kinaonekana...hauweji kujenga nchi huku unafuja hela
Is it really true hujawahi kuona kinachofanyika hata kimoja?Tujaalie hujawahi kuona sasa kama hatutolipa Kodi kabisa Itakuwaje?Halafu tunalalamika kwann nchi inaenda kukopa,sababu NI moja Tu Wananchi hawalipi Kodi na hata elf mbili nayo wanaiona dili kubwa kwa mweZi,Nchi ina watu 61m registered tax payers hawazidi milioni 4 tutajiendeshaje?Kila mtu atakuja aseme tutafute vyanzo vipya vya mapato sijui kodi lkn mtu huyo huyo aliyeona sababu yakuanzisha vyanzo vipya vya kodi hatoweza kukwambia yeye kaona chanzo kipya ni kipi,Watanzania hawatiridhika mpk kila kitu wakipate bure nahilo haliwezekani sababu hakuna serikali ya hivyo duniani
 
Mimi mtazamo wangu Ni kuwa wigo wa walipaji uongezwe Kwa kasi kwenye upande wa umeme na huduma nyingine kama maji pia mita uwe na Kodi walau 500 hizi ila wahakikishe huduma zinasambazwa Kwa kiwango kikubwa. Ila hayo yote hayatofaa bila kiongozi wa nchi kuwa mkali na kuhakikisha watendaji wa chini hawachezei pesa za wananchi kwa vyovyote kupitia bajeti na mtumizi yasiyo na msingi. Yakidhibitiwa hayo mbona nchi tutaijenga vizuri kwa kufunga mkanda tu.
 
Kodi ya jengo haifuati ukubwa wa jengo, inafuata aina ya jengo na eneo.
 
Kama una mita ya luku tu lazima ulipe kodi ya jengo
Ndiyo, mara moja kwa mwezi na jengo moja lenye mita zaidi ya moja linalipiwa kulingana na idadi ya mita zilizopo, kwa mfano fremu za maduka kwenye jengo moja.
 
Huu ni ujinga unajua pengine Mwigulu na Wenzake wanakula kwa urefu wa kwamba kiasi gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…