Maoni yangu binafsi juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea duniani

Maoni yangu binafsi juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea duniani

Nilisikia Urusi wanatoa crude oil na hapa kwetu hakuna uwezo wa kuyachakata mkuu naomba nipate elimu hapa..
Ni kweli kiwese cha urusi kinahitaji kuchakatwa kabla ya kutumika. Lakini tunachoamini EWURA kama wangekuwa hawabebwi leo uwezo wetu wa kuchakata mafuta ungelikuwa mkubwa na tungeachana na uagizaji wa mafuta yaliyochakatuliwa kutoka India.

Bulk supplies ni utaratibu wa kifisadi na EWURA wanauendeleza kwa sababu baadhi yao wako kwenye payroll na kwa vile wao hawaathiriki hawana msukumo wa kubadilisha.

Hivyo kutokana na huu udadavuaji ni dhahiri EWURA wanyimwe kodi utaona sera zitakavyobadilika na kuwa chombo cha usimamizi chenye kujitegemea.

Tunakiri upo uwekezaji umeanza wa kuchakata lakini ni mdogo na hauwezi kupunguza mzigo wa kuibeba EWURA na kupunguza bei ya kiwese kwa walaji kwa sababu unategemea wawekezaji kutoka nje eneo ambalo lipo ndani ya uwezo wetu.

Kwa nchi inayojenga uchumi wa viwanda ungelitegemea uwezo wa kuchakata kiwese upo mikononi mwa umma kuondoa bei za kupangwa ambazo zitakwamisha nia ya serikali ya uchumi wa viwanda.

Bila bei poa ya nishati zote uchumi wa viwanda ni vuvuzela la majukwaani tu.

USHAURI

Warusi wako tayari kuisaidia Tanzania kujenga uwezo wa kuchakata mafuta tatizo au kikwazo chetu uwezo huo utamaliza ufisadi wa bulk suppliers ambao unawatajirisha watendaji ndani ya EWURA na Wizara ya nishati.

Sasa tuamue ama zao au zetu.

Ugumu wa kutatua hii kero ni ukosefu wa utashi wa kisiasa tu kwa sababu vyeo serikalini hutolewa kama fadhila tu siyo wenye uwezo wa kutatua kero!
 
Ni kweli kiwese cha urusi kinahitaji kuchakatwa kabla ya kutumika. Lakini tunachoamini EWURA kama wangekuwa hawabebwi leo uwezo wetu wa kuchakata mafuta ungelikuwa mkubwa na tungeachana na uagizaji wa mafuta yaliyochakatuliwa kutoka India.

Bulk supplies ni utaratibu wa kifisadi na EWURA wanauendeleza kwa sababu baadhi yao wako kwenye payroll na kwa vile wao hawaathiriki hawana msukumo wa kubadilisha.

Hivyo kutokana na huu udadavuaji ni dhahiri EWURA wanyimwe kodi utaona sera zitakavyobadilika na kuwa chombo cha usimamizi chenye kujitegemea.

Tunakiri upo uwekezaji umeanza wa kuchakata lakini ni mdogo na hauwezi kupunguza mzigo wa kuibeba EWURA na kupunguza bei ya kiwese kwa walaji kwa sababu unategemea wawekezaji kutoka nje eneo ambalo lipo ndani ya uwezo wetu.

Kwa nchi inayojenga uchumi wa viwanda ungelitegemea uwezo wa kuchakata kiwese upo mikononi mwa umma kuondoa bei za kupangwa ambazo zitakwamisha nia ya serikali ya uchumi wa viwanda.

Bila bei poa ya nishati zote uchumi wa viwanda ni vuvuzela la majukwaani tu.

USHAURI

Warusi wako tayari kuisaidia Tanzania kujenga uwezo wa kuchakata mafuta tatizo au kikwazo chetu uwezo huo utamaliza ufisadi wa bulk suppliers ambao unawatajirisha watendaji ndani ya EWURA na Wizara ya nishati.

Sasa tuamue ama zao au zetu.

Ugumu wa kutatua hii kero ni ukosefu wa utashi wa kisiasa tu kwa sababu vyeo serikalini hutolewa kama fadhila tu siyo wenye uwezo wa kutatua kero!
Hii Nchi ni ngumu sanaa... sijui lini wezi watakoma
 
Mheshimiwa ajiandae jina kukatwa 2025 maana kawavua nguo zote hadharani na kujiundia genge la maadui wa kisiasa.

Ataishia upinzani ambako nako wakurugenzi wa majiji na Halmashauri wanamsubiri kumalizana naye
 

Attachments

  • PSX_20231103_230148.jpg
    PSX_20231103_230148.jpg
    228.4 KB · Views: 2
Back
Top Bottom