Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #1,541
Kabla ya mgonjwa kukutana na muuguzi hukutana na dakitari sasa maelekezo ya dakitari yanasema nini?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Martin Maranja Masese
@IAMartin_
August 2021 ndugu Daniel Chongolo uliwasimanga na kuwananga sana watanzania ambao wanataka Katiba Mpya na ukasema Katiba Mpya haileti unga mezani
November 2023 Daniel Chongolo unaandika barua kujiuzulu nafasi ya katibu mkuu CCM ukitoa sababu za kuchafuliwa mitandaoni kwamba unawajibika
Daniel Chongolo unajiuzulu kwa shinikizo la ndani ya CCM uliyokuwa mtendaji mkuu ukitetea harakati za kukataa katiba mpya. Kiko wapi!? Kiko wapi!?
Watafiti wa mambo tunajua, hakuna ‘kuchafuliwa mitandaoni’ isipokuwa CCM sasa hawakutaki, na wamesema uondoke, wapachike mtu wao.
CCM wenzako walivyo wapumbavu, wamekubaliana watengeneze ‘skendo hewa’ kwamba unafanya uzinzi na kutuma kende zako WhatsApp.
Chongolo kwa kuwa umeshirikishwa mchongo huo, umeamua kuandika barua kujiuzulu ukipita katika njia hizo ambazo wamekuelekeza.
Ulipotuhumiwa kutafuna zaidi ya shilingi bilioni 3 katika ziara ya CCM kanda ya ziwa, hukujiuzulu, ujiuzulu kwa sababu ya message za WhatsApp?
Kulikuwa hakuna sababu za msingi za kujiuzulu kwa kutunga skendo za uzushi na uongo. CCM hawakutaki kwa sababu hufai katika biashara zao.
Gari inayosambazwa kwamba ni yako na imepata ajali ya mchepuko wako, kadi ya gari haifanani na plate number. Siyo gari yako. Unashiriki uongo.
Propagandists wa MaCCM hawana akili hata nukta. Kuandaa wanachama wao kwa katibu mkuu wao anajiuzulu hadi wamtengenezee skendo feki?
CCM mnatumia akili ndogo kucheza na hisia za wanachama wenu. Wanachama wenu, hawana ubongo wa kudadisi, kufikiri na kuhoji. MAZOMBI.
Una nyumba karibu 70 hapa Dar es Salaam, una magari ya kutosha, una mashamba mengi, na mengine umeyapata kiharamia, unahitaji kuyalinda.
Tunaelewa, huwezi kuhamia upinzani, huwezi, utabaki CCM kwa sababu umejinufaisha sana na umepata utajiri mkubwa. Utabaki kulinda mali zako.
Lakini watanzania tutaishi tukisema kwamba, Daniel Chongolo ukiwa katibu mkuu wa CCM, ulipinga mchakato wa kupatikana Katiba Mpya hadharani.
Daniel Chongolo unaondoka katika ofisi ya katibu mkuu wa CCM ukiwa huna tofauti na mtangulizi wako, Bashiru Ally, wote mmekuwa MIZIGO. KWAHERI!
MMM, Martin Maranja Masese
12:27 PM · Nov 28, 2023