Maoni yangu kuhusu biashara ya kuagiza bidhaa China

Maoni yangu kuhusu biashara ya kuagiza bidhaa China

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
BIASHARA YA KUAGIZA CHINA

Leo nimeona nitumie haki yangu ya kikatiba chini ya ibara ya 18 kifungu cha kwanza kuhusu uhuru wa kutoa maoni. Nitazungumzia kuhusu hii biashara ya kuagiza vitu China na kuviuza Tanzania. Maoni yangu haya yanatokana na uzoefu wangu kwenye aina hii ya biashara. Pia nimeona ni wakati sahihi wa kutoa haya maoni baada ya kusikitishwa na wimbi kubwa la matapeli wanaowaliza watu hasa wanawake.

Kwanza kabisa tukubaliane hii biashara ni nzuri inalipa kwasababu nchi zetu hazina viwanda hivyo kila kitu kinatoka nje hasa China. Ni biashara ambayo ukiifanya kwa makini itakutoa kirahisi zaidi. Tanzania pamoja na changamoto zake za tozo na mambo mengine ila bado kibiashara ni sehemu nzuri kwasababu ya wingi wa watu. Watu zaidi ya milioni 60 ni wengi hivyo huwezi kosa kabisa wateja. Cha muhimu cheza na BEI pamoja na UBORA wa vitu unavyoagiza.

Baada ya wajanja kugundua Tanzania panalipa ndo kukatokea watu wanaowaagizia bidhaa wenzao kutoka China huku wao wakifaidika na "cha juu" wanachoongezea. Ni kitu kizuri na ninawapongeza. Ila kuna wahuni wachache nao wamejitokeza na kuanza kutapeli watu pesa zao walizopata kwa shida. Mitandaoni ni kilio kila kona. Wanawake wakiwa wahanga wakuu wa hawa matapeli. Poleni sana. Binafsi ninajua maumivu ya kutapeliwa. Nilishawahi tapeliwa na mbongo mwenzangu simu aina ya Iphone. Inauma sana kuona ndugu yako anakutapeli LIVE. Kibaya ni kwamba utakuta mtu anatapeli watu kibao na kuwa na kiburi cha hali ya juu. Na wengi wa waanaoagizia watu mizigo hujifanya miungu watu.

Nini maoni yangu ili mtu asitapeliwe au kupunguza hatari ya kutapeliwa? Binafsi baada ya kupata vipigo mara kadhaa kupitia matapeli niliamua kujivika mabomu na kuanza kuagiza mwenyewe. Ingawa haimaanishi kwamba ukiagiza mwenyewe ndo hutakutana na matapeli wa kichina... la hasha. Kuna wachina matapeli pia ila ni wachache kulinganisha na watanzania wenzetu.

Nilichofanya ni ku-install app ya Alibaba kwenye simu yangu kisha kuanza kutafuta vitu mbalimbali nilivyokuwa navitaka. Baada ya kupata na kukubaliana bei basi huwa ninalipia direct kwa mchina kisha nampa address ya msafirishaji ambapo mara nyingi natumia Silent Ocean Ltd. Baada ya hapo mchina hupeleka mzigo kwa msafirishaji na kunitumia picha ya delivery note kuonyesha kwamba mzigo sasa uko Silent Ocean Ltd. Zamani mizigo ilikuwa inafika mapema sana. Ndani ya mwezi na wiki moja unakuwa ushapata mzigo ila baada ya corona hadi leo mizigo kuipata haipungui miezi miwili (siku 60). Ila matapeli wengi watakuambia haizidi siku 45.

Faida na hasara za kutumia huu utaratibu wangu zipo. Unapoagiza online inabidi umakini sana kwasababu pichani kitu ni kizuri lakini kikikufikia ni ovyo. Pia kwenye Alibaba kuna matapeli pia wa kichina hasa upande wa nguo. Unaweza lipia asikutumie mzigo au akatuma vitu vya ovyo. Faida ya huu utaratibu wangu ni kupata vitu kwa bei chini ambayo itakuja kukupa faida kubwa. Kwa mfano hizi pochi zinazouzwa 6000 hadi 8000 kule China huwa ni 2000 hadi 3000. Faida nyingine unakuwa na uhakika wa mzigo kuja kwa jina lako na sio dalali hivyo unajikuta umeokoa gharama za usafirishaji. Kiukweli kuagiza mwenyewe ni bora zaidi. Kuhusu matapeli wa kichina huwa ni nadra sana kutokea. Pia kuna jinsi ya kuwagundua kabla hata hujaagiza.

Mimi nashauri muwe na hiyo App mjiagizie wenyewe. Kama huelewi omba hata mtu wako wa karibu akusaidie. Isitoshe waagizaji wengi nao huingia tu Alibaba na kuwaagizia watu. UOGA WAKO NDO UMASKINI WAKO.
 
Inategemea na ulichosafirisha. Kila bidhaa ina gharama yake.
Tahadhari tahadhari tahadhari. Hata mwanzisha thread anaweza kuwa ni tapeli anayejitangaza kiana! Huu mtindo uko sana siku hizi. Mtu anasimulia kama alishawahi kuwa victim na sasa amejua njia sahihi. Anajifanya kama anasimulia masaibu aliyopata na namna alivyojikwamua.

Baada ya hapo anatega mingo kusubiri raia waanze kuomba msaada ili awasaidie. Ukienda kichwa kichwa ''anakusaidia'' kweli kweli. ANGALIZO: Sijasema huyu jamaa ni tapeli ila nimesema kuna matapeli wanatumia njia za aina hii.

Hivyo akili kum-kichwa!
 
Nataka nikige swali, [emoji17] sorry
Hivi mfano nimeagiza mzigo wa Millioni 3 ... Pale bandarini Ninatakiwa nilipie Kodi tsh ngapi?
Kama umeagiza na kusafirisha kwa kutumia kampuni kama silent ocean ltd huwa huhitaji kulipia kodi.

Gharama zako za kusafirisha tu, wao wanamaliza kila kitu unaenda kuchukua mzigo wako ofisini kwao. Yaani ukiambiwa utalipia mfano dola 100 ya usafiri basi huhitaji kutoa gharama nyingine. Ila ukinunua kwa mchina kisha akakusafirishia kwa kampuni zao hapo mzigo ukifika bandarini unapambana kuutoa mwenyewe.

Uzuri wa option ya pili huwa cost ya usafirishaji ya wachina iko chini kidogo (at least kwa uzoefu wangu). All in all Silent ocean ni bora zaidi in terms of cost na usalama pia.
 
Tahadhari tahadhari tahadhari. Hata mwanzisha thread anaweza kuwa ni tapeli anayejitangaza kiana! Huu mtindo uko sana siku hizi. Mtu anasimulia kama alishawahi kuwa victim na sasa amejua njia sahihi. Anajifanya kama anasimulia masaibu aliyopata na namna alivyojikwamua.Baada ya hapo anatega mingo kusubiri raia waanze kuomba msaada ili awasaidie. Ukienda kichwa kichwa ''anakusaidia'' kweli kweli. ANGALIZO: Sijasema huyu jamaa ni tapeli ila nimesema kuna matapeli wanatumia njia za aina hii. Hivyo akili kum-kichwa!
Ndugu naheshimu maoni yako ila MIMI SIFANYI BIASHARA YA KUMUAGIZIA MTU KITU KUTOKA CHINA.

Nimetoa tu ushauri na sihitaji mtu yeyote kuniomba nimuagizie kitu China. Pia jitahidi kuwa positive badala ya kuwaza mabaya muda wote.
 
Unasema unamlipa mchina mwenyewe je unamlipa kwa njia gani?
 
Usijaribu kuagiza nguo kupitia Alibaba unless uwe umepata mchina unayeheshimiana naye , nguo ni risk Sana , utawekewa lonya mpak utakubali
 
Usijaribu kuagiza nguo kupitia Alibaba unless uwe umepata mchina unayeheshimiana naye , nguo ni risk Sana , utawekewa lonya mpak utakubali
Uko sahihi kabisa. Mara mbili niliwekewa vitu vya ajabu mno.
 
Kila nikiingia alibaba nachat na hao wachina ila sasa kuagiza ndo nasita kwa kweli and sijui kwa nini,
Mimi kitu cha kwanza huwa naangalia star rate za kampuni na kusoma maoni ya wateja wengine waliowahi kuagiza. Nimeweka mfano wa kampuni mbili tofauti.

Screenshot_20220516-135859_Alibabacom.jpg


Screenshot_20220516-135946_Alibabacom.jpg
 
Kuna huyu jamaa hapa,nilljikuta tu nimekuwa added kwenye group lake Ila nikawa interest na bidhaa anazopost na bei anazoweka.Lkn nimekuwa mzito sn wa kufanya maamuzi maana nilipoona amezuia watu kucomment nimejikuta nimeona Kam amefanya udicteta watu kutoa feedback

IMG_20220516_152629.jpg
 
Kuna huyu jamaa hapa,nilljikuta tu nimekuwa added kwenye group lake Ila nikawa interest na bidhaa anazopost na bei anazoweka.Lkn nimekuwa mzito sn wa kufanya maamuzi maana nilipoona amezuia watu kucomment nimejikuta nimeona Kam amefanya udicteta watu kutoa feedback

View attachment 2226885
Nakupa tahathari hao majama asilina 90 ni wasani kwamfano mke wangu aliagiza mzigo toka kwao now ni mwezi wa 6 Unaenda ni sound 2 na ukikuta mkwell atakuletea mzigo kwell kwa bei rahisi ila transport fee inakuwa ni zaid ya bei ya mzigo ulio lipia co unajikuta umenunua kitu bei ya juuu zaid hata ya hapa bongo

Sent from my GM1910 using JamiiForums mobile app
 
Kuna huyu jamaa hapa,nilljikuta tu nimekuwa added kwenye group lake Ila nikawa interest na bidhaa anazopost na bei anazoweka.Lkn nimekuwa mzito sn wa kufanya maamuzi maana nilipoona amezuia watu kucomment nimejikuta nimeona Kam amefanya udicteta watu kutoa feedback

View attachment 2226885
Hawa ni matapeli bro. Na baadhi yao hata China hawajawahi kufika wanacho Fanya ni kufungua magroup ya watsap then wanachukua bidhaa hapo hapo kariakoo wanapost na kudanganya kuwa wanafuata China , jaribu kufuatilia bei wanazotoa na bei zilizopo huko kwenye platfm ya Alibaba
 
Back
Top Bottom