Maoni yangu sakata la Manara na Barbara

Maoni yangu sakata la Manara na Barbara

Mndengereko

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2011
Posts
7,296
Reaction score
3,398
MAONI YANGU JUU YA AUDIO CLIP YA MANARA ni kama ifuatavyo

Regardless kama tuhuma anazotuhumu Manara kwamba kufedheheshwa, kunyanyaswa and the like ni za kweli au la! Kitendo alichokifanya cha kuleta claim yake dhidi ya boss wake tena top top boss ,wa watumishi katika taasis /klabu ya simba ,tenatkatika public , tena katika wakati huu ni very unethical and unproffesional hasa kwa taasis kubwa kama simba anayohudumu na hasa pia kwa mtu wa kariba yake, ninachokiona anataka kuwin sympathy ya wanasimba.

Swala hili ni la kiungozi na hakupaswa kulileta katika media /public, kwa maoni yangu alipaswa alimalize ndani ya uongozi, hasa ukizingatia kuwa ana mahusiano mazur na MO. Alikuwa ana faida ya ziada ya kuweza kulalamika na kusikilizwa

Ambacho nimegundua watu wengi wapo emotional sana juu ya swala hili, they dont think and judge rationale, hapa nazungumzia profesionalism guys, tusirelate na mangap haji kaifanyia simba na jinsi gan ana mchango katika taasis,weled katika kazi ni lazima ufuate.

Muhimu la kujifunza ni kuwa 'KUDAI HAKI BILA YA KUFUATA UTARATIBU NI FUJO '

Binafsi sitegemei Barbara aje amjibu Haji katika public, ni imani yangu profesionalism yake itazungumza japo la kiofisi litamalizwa kiofis kwa taratibu za kiofis, period

the great K.
 
Kwa kaliba ya Haji ulitegemea anyamaze?

Mo aliwahi kusema kuwa yeye sio Haji so hawezi kuropoka, kwa maana hiyo hata Mo anajua Haji ni mtu wa namna gani, ametoa vumbi ndani mwake hivyo kwasasa yuko salama.
 
Kwa kaliba ya Haji ulitegemea anyamaze?
Mo aliwahi kusema kuwa yeye sio Haji so hawezi kuropoka, kwa maana hiyo hata Mo anajua Haji ni mtu wa namna gani, ametoa vumbi ndani mwake hivo kwasasa yuko salama.
Kama hana kifua kikubwa basi hafai.
 
Huyu anatafuta huruma za mashabiki wa Simba. Kazingua sana mwamba
 
Kama sio mind game basi kuna machafuko sana huko juu, pengine hali ni mbaya kuliko tunavyodhani.
 
Matokeo mazuri ya Simba yamekuwa sehemu ya kuficha udhaifu wao wa kiuongozi.

Manara amelewa na umaarufu alionao, hana weledi, na hatambui nafasi yake.

Sidhani kama kwenye kampuni yenye uongozi thabiti Staff wa kawaida anaweza ongea ovyo kuhusu Mkurugenzi wake kama anavyofanya Manara.
 
Manara anaendeshwa na uswahili kuliko professionalism ya kazi inayomuweka pale......nadhani kwa level ya Simba sasa Haji sio size yake.....ni nvyema aachie ngazi.....
 
JamiiForums-1146213983.jpg
JamiiForums617938071.jpg
 
Screenshot_20210722-121226_Chrome.jpg

haya ni majibu ya Babra,hata kama Haji ananyanyaswa,kwa majibu haya amemfanya Haji aonekane punguani kwa watu tunaojielewa kama sisi
 
Hayo ni maisha yao binafsi, wayasuluhishe kupitia kwenye familia zao!
 
Kumbe jamaa analamba laki saba tu kwa mwezi
Mkataba mzuri uko mezani kitambo ila hataki kusaini akiamini anastahili zaidi ya huo hivyo kaamua kupokea huo wa kujitolea..
Haiwezekani mkuu wa idara ulipwe laki saba.
 
Mkataba mzuri uko mezani kitambo ila hataki kusaini akiamini anastahili zaidi ya huo hivyo kaamua kupokea huo wa kujitolea..
Haiwezekani mkuu wa idara ulipwe laki saba.
Uwa anapata marupurupu kutoka kwa mashabiki kwa kupewa mia 5, elfu 1, elfu 2, elfu 5 na hata elfu 10!

Ukuona wakati anamkabidhi Mzee Mpili ile ahadi yake kulikuwepo na mchanganyiko wa noti za 1,000, 2,000, 5,000 na 10,000
 
Uwa anapata marupurupu kutoka kwa mashabiki kwa kupewa mia 5, elfu 1, elfu 2, elfu 5 na hata elfu 10!

Ukuona wakati anamkabidhi Mzee Mpili ile ahadi yake kulikuwepo na mchanganyiko wa noti za 1,000, 2,000, 5,000 na 10,000
Unajua hata mm nilikuwa nimeliona hilo la kumpa yule Mzee hela ule ni usanii tu pale umefanyika .
 
Back
Top Bottom