Maonyesho ya nane nane yanaendelea kupoteza mvuto mwaka hadi mwaka

Maonyesho ya nane nane yanaendelea kupoteza mvuto mwaka hadi mwaka

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Maonyesho haya maalum kwa ajili ya wakulima na wafugaji ambayo hufanyika kila mwaka yanaendelea kupoteza mvuto wake tofauti na ile miaka ya uanzishwaji wake Yan 95,96 na kuendelea. Lakini kuanzia miaka hii ya 2000 katikati hali ni tofauti na miaka ya nyuma.

Wamachinga kwenye maonyesho wanaomwaga bidhaa zao chini ni wengi kuliko hata hao wakulima na wafugaji ambao ni sikukuu yao.

Wachezezeshaji kamari ni wengi na wenyewe, hawa hawana mtaji wa pesa wa bidhaa, wala mazao yoyote yale bali mitaji yao na bidhaa zao ni akili tu. Hili pia nimelishuhudia kwa wingi mwaka huu., nimeshuhudia idadi Kubwa ya wacheza kamari mwaka huu kuliko kipindi kingine.

Wafanyabiashara wa nguo za mitumba. Vyombo vya ndani hutumia nafasi hiyo kufanya biashara zao zaidi ya mkulima mwenyewe.

Hakuna mabadiliko yoyote ya teknolojia ya kilimo, mambo yote ni yale yale tu kama vile bustani ya mboga za majani, nyanya, kuku. Sungura nk. Wananchi na wenyewe wamechoka kuona mtindo ni ule ule waoujua miaka yote.

Nimeshudia aina moja ya ng'ombe akiwa na mtoto wake, tofauti na wakati mwingine kunakuwa na aina tofauti za ng'ombe wa kienyeji na wa kisasa.
Mabanda mengi yalikuwa matupu kwa kile kinachodawaida ni ukubwa wa kodi ya pango hivyo watu kushindwa kumudu gharama za uendeshaji kulinganisha na siku zenyewe ni chache.

Wakulima na wafugaji mabanda yao ni madogo kulinganisha na wafanyabiashara wakubwa kama vile makampuni ya simu, makampuni ya gesi na vinywaji.,hapo tunaona kabisa mfanyabiasha amekuwa mkubwa kwenye maonyesho ya wakulima na wafugaji kuliko wakulima na wafugaji wenyewe ambao ni sikukuu yao.
Serikali ijitafakari upya kuhusu sikukuu hizi za wakulima. Zinaenda kupoteza mwamko wake.

Huu uonyeshaji wa bustani za mboga mboga kila mwaka hakuna mabadiliko yoyote wala mboga mpya zilizoingia mbona karibu kila mtu anajua kulima mboga, hili somo lipo tangu shule ya msingi.

Viongozi wengi wanapenda kubeba waandishi ile siku ya kelele tena kwenye mabanda ambayo yatakuwa yameandaliwa vyema ajili ya upigaji picha na kuonekana kwenye tv
Screenshot_20220813-122624.png
Screenshot_20220813-122606.png
 
Kiukweli maana halisi ya haya maonesho imepotea, kuna clip moja mitandaoni nimeona afisa wa Magereza amevunja ngao/zawadi ya ushindi waliopewa Magereza huku akiwakemea wasaidizi wake kwamba wanamdanganya nani kwenye hayo maonesho? (saba saba na nane nane). Anawaambia mnapeleka kitanda kwenye maonesho bei milioni 4 nani atanunua? Je mtu akija kuona kiwanda chenu ataona bidhaa nyingine mlizozalisha na kuuza? Mnaonyesha mifugo, mashamba nk lakini huku kambini hakuna kitu, ni uongo mtupu. Sikuweza kujua huyu boss ni nani but alichosema ni ukweli mtupu... So kiujumla haya maonesho ilitakiwa wale wanaopewa ushindi kuwe na mechanism ya kujua je hiki anachokionyesha hapa huko anakotoka anakifanya na kunufaisha wengine?
 
Maonyesho haya maalum kwa ajili ya wakulima na wafugaji ambayo hufanyika kila mwaka yanaendelea kupoteza mvuto wake tofauti na ile miaka ya uanzishwaji wake Yan 95,96 na kuendelea. Lakini kuanzia miaka hii ya 2000 katikati hali ni tofauti na miaka ya nyuma.

Wamachinga kwenye maonyesho wanaomwaga bidhaa zao chini ni wengi kuliko hata hao wakulima na wafugaji ambao ni sikukuu yao.

Wachezezeshaji kamari ni wengi na wenyewe, hawa hawana mtaji wa pesa wa bidhaa, wala mazao yoyote yale bali mitaji yao na bidhaa zao ni akili tu. Hili pia nimelishuhudia kwa wingi mwaka huu.

Wafanyabiashara wa nguo za mitumba. Vyombo vya ndani hutumia nafasi hiyo kufanya biashara zao zaidi ya mkulima mwenyewe.

Hakuna mabadiliko yoyote ya teknolojia ya kilimo, mambo yote ni yale yale tu kama vile bustani ya mboga za majani, nyanya, kuku. Sungura nk. Wananchi na wenyewe wamechoka kuona mtindo ni ule ule waoujua miaka yote.

Nimeshudia aina moja ya ng'ombe akiwa na mtoto wake, tofauti na wakati mwingine kunakuwa na aina tofauti za ng'ombe wa kienyeji na wa kisasa.
Mabanda mengi yalikuwa matupu kwa kile kinachodawaida ni ukubwa wa kodi ya pango hivyo watu kushindwa kumudu gharama za uendeshaji kulinganisha na siku zenyewe ni chache.

Wakulima na wafugaji mabanda yao ni madogo kulinganisha na wafanyabiashara wakubwa kama vile makampuni ya simu, makampuni ya gesi na vinywaji.,hapo tunaona kabisa mfanyabiasha amekuwa mkubwa kwenye maonyesho ya wakulima na wafugaji kuliko wakulima na wafugaji wenyewe ambao ni sikukuu yao.
Serikali ijitafakari upya kuhusu sikukuu hizi za wakulima. Zinaenda kupoteza mwamko wake.View attachment 2322858View attachment 2322860
Kwa Mwanza maonesho ya wakulima 10% haalafu maonyesho mengine ni 90% ila watu wanayapenda kinoma. Mwakani njoo halafu tafuta Banda la city center, burudani Ile balaa.
 
Kiukweli maana halisi ya haya maonesho imepotea, kuna clip moja mitandaoni nimeona afisa wa Magereza amevunja ngao/zawadi ya ushindi waliopewa Magereza huku akiwakemea wasaidizi wake kwamba wanamdanganya nani kwenye hayo maonesho? (saba saba na nane nane). Anawaambia mnapeleka kitanda kwenye maonesho bei milioni 4 nani atanunua? Je mtu akija kuona kiwanda chenu ataona bidhaa nyingine mlizozalisha na kuuza? Mnaonyesha mifugo, mashamba nk lakini huku kambini hakuna kitu, ni uongo mtupu. Sikuweza kujua huyu boss ni nani but alichosema ni ukweli mtupu... So kiujumla haya maonesho ilitakiwa wale wanaopewa ushindi kuwe na mechanism ya kujua je hiki anachokionyesha hapa huko anakotoka anakifanya na kunufaisha wengine?
Huyo ndio alikuwa mkuu wa jeshi la magereza aliyehamishiwa kuwa mkuu wa mkoa Mara!!kwamba mnatumia mamilioni kuandaa maonyesho hayo, ila mkienda mnauza bidhaa za laki tano tu, mnavirudisha store mnasubilia maonyesho yajayo mna vipaka polish tena!!HUU NI WIZI MTUPU.
 
Sema wewe ndo hauko interested,huu mtindo wa kugeneralize Mambo na kuwaunganisha watu wote kwenye ishu moja sio mzuri.Ungekuja Nanenane Mbeya mwaka huu ungejionea nyomi ya watu.
Haya baadhi ya watu sawa, Nyomi ya watu wote unadhani wote wanakuja kuangalia ishu za kilimo? sio kweli
 
Sahv watu wako bize na matamasha ya wasanii,mipira,kamari basi
Hayo mengine tupa kule

Ova
 
Hiyo ni sikukuu ya wakulima. Wacha wafurahie. Wacheze kamari, walewe nk nk. Ndiyo kusherehekea huko.
 
Huyo ndio alikuwa mkuu wa jeshi la magereza aliyehamishiwa kuwa mkuu wa mkoa Mara!!kwamba mnatumia mamilioni kuandaa maonyesho hayo, ila mkienda mnauza bidhaa za laki tano tu, mnavirudisha store mnasubilia maonyesho yajayo mna vipaka polish tena!!HUU NI WIZI MTUPU.
Duuuh kumbe ndo alikuwa ndiyo alikuwa CGP?? Sijajua amekosea nini wakamtoa huko lakini kiukweli ile hoja yake niliipenda sana na ndiyo ukweli wenyewe. Hata baadhi ya taasisi na halmashauri mbalimbali unakuta wanatumia mamilioni kuandaa banda lao ili lishinde lakini ukibahatika kuwatembelea maeneo yao wanakotoka huwezi kuona chochote.
 
Maonyesho ya nane nane ni ya wakulima,kwanza nashangaa inakuaje wafanyabiashara wa bidhaa zingine wanapewa mabanda wafanye biashara.

makampuni ya gesi yanachukua mabanda,gesi yenyewe bora ingekua ile itokanayo na kinyesi cha wanyama "biogas" wanauza ma gas yanayoagizwa toka nchi za watu.

Maonyesho yamepoteza mvuto sababu wanayoyapangilia wapo hovyo,unaruhusu wachezesha kamari ili iweje? kamari ina uhusiano gani na mboga mboga au wanyama?

Unaruhusu makampuni ya simu yanaingia kufanya nini mle ndani? watangaze mabiashara yao nnje huku sio ndani yani ki ufupi sioni maana halisi ya maonyesho haya ya wakulima.

Mtu anaenda nane nane anarudi na nguo mpya viatu,nk unajiuliza huyu alienda maonyesho ya kilimo au alienda shopping? badala tuone watu wanarejea na Machungwa,maembe,mboga mboga,mazao ya kila aina tunayoyajua na tusioyajua,nk product zote za shamba..

ila sasa hivi ni vice versa watu tunaenda nane nane kununua laptop,Tv,simu maana ndio kuna mapunguzo ya bei Ujinga mtupu... na unadhani viongozi hawalioni hili au hawalijui? wanalijua sanaa ila wanalipotezea maana si wanapewa chochote kitu hvyo wao wanaruhusu tuuu..
 
Watu wanapenda kwenda tatizo kubwa ni vumbi kubwa wao eneo ni hilo hilo kila mwaka wanashindwa kujenga bara bara ili kupunguza vumbi na ishu yao ya kumwagilia maji nane nane pangekua bora watu wengi wangeenda na si kwa Vumbi lile...
 
Maonyesho haya maalum kwa ajili ya wakulima na wafugaji ambayo hufanyika kila mwaka yanaendelea kupoteza mvuto wake tofauti na ile miaka ya uanzishwaji wake Yan 95,96 na kuendelea. Lakini kuanzia miaka hii ya 2000 katikati hali ni tofauti na miaka ya nyuma.

Wamachinga kwenye maonyesho wanaomwaga bidhaa zao chini ni wengi kuliko hata hao wakulima na wafugaji ambao ni sikukuu yao.

Wachezezeshaji kamari ni wengi na wenyewe, hawa hawana mtaji wa pesa wa bidhaa, wala mazao yoyote yale bali mitaji yao na bidhaa zao ni akili tu. Hili pia nimelishuhudia kwa wingi mwaka huu., nimeshuhudia idadi Kubwa ya wacheza kamari mwaka huu kuliko kipindi kingine.

Wafanyabiashara wa nguo za mitumba. Vyombo vya ndani hutumia nafasi hiyo kufanya biashara zao zaidi ya mkulima mwenyewe.

Hakuna mabadiliko yoyote ya teknolojia ya kilimo, mambo yote ni yale yale tu kama vile bustani ya mboga za majani, nyanya, kuku. Sungura nk. Wananchi na wenyewe wamechoka kuona mtindo ni ule ule waoujua miaka yote.

Nimeshudia aina moja ya ng'ombe akiwa na mtoto wake, tofauti na wakati mwingine kunakuwa na aina tofauti za ng'ombe wa kienyeji na wa kisasa.
Mabanda mengi yalikuwa matupu kwa kile kinachodawaida ni ukubwa wa kodi ya pango hivyo watu kushindwa kumudu gharama za uendeshaji kulinganisha na siku zenyewe ni chache.

Wakulima na wafugaji mabanda yao ni madogo kulinganisha na wafanyabiashara wakubwa kama vile makampuni ya simu, makampuni ya gesi na vinywaji.,hapo tunaona kabisa mfanyabiasha amekuwa mkubwa kwenye maonyesho ya wakulima na wafugaji kuliko wakulima na wafugaji wenyewe ambao ni sikukuu yao.
Serikali ijitafakari upya kuhusu sikukuu hizi za wakulima. Zinaenda kupoteza mwamko wake.

Huu uonyeshaji wa bustani za mboga mboga kila mwaka hakuna mabadiliko yoyote wala mboga mpya zilizoingia mbona karibu kila mtu anajua kulima mboga, hili somo lipo tangu shule ya msingi.

Viongozi wengi wanapenda kubeba waandishi ile siku ya kelele tena kwenye mabanda ambayo yatakuwa yameandaliwa vyema ajili ya upigaji picha na kuonekana kwenye tv
View attachment 2322858View attachment 2322860
Kanda ipi hiyo? Kwa Nyanda za Juu Kusini Wala hayapotezi ila waratibu walitoa mda mchache wa kujiandaa..

Ndio maana mh.Rais Amesema sasa kutakuwa na maonyesho ya 8/8 ya Kimataifa Mkoa unaotaka Kuwa mwenyeji lazima wajenga mabanda na viwanja vyenye hadhi na ukubwa unaotakiwa kwa kuzingatia standards zinazotakiwa Kimataifa👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220809-073500.png
    Screenshot_20220809-073500.png
    101.2 KB · Views: 5
Nanenane wafanyabiashara wa vyombo wanafanya nn uko,wacheza kamari wanafanya nn uko,ni mambo mengi sana unatayaona uko hayahusiani na wakulima kabisa Yani.
 
Back
Top Bottom