Maonyesho ya Shandong Yaimarisha Uhusiano kati ya China na Kenya

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
Na Tom Wanjala

Maonyesho ya nne ya bidhaa zinazouzwa nje ya mkoa wa Shandong nchini China, yaliyofanyika jijini Nairobi wiki iliyopita, yalifana kutokana na idadi kubwa ya watu waliohudhuria. Maonyesho hayo yaliyofanyika kati ya tarehe 16 na 19 mwezi huu, na ambayo lengo lake kuu lilikuwa kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya China na Kenya, yalitoa jukwaa la kipekee kwa Wakenya kujionea bidhaa mbalimbali kutoka China.

Ukumbi wa Sarit ulioko viungani mwa jiji la Nairobi na ambako hafla hii iliandaliwa, ulisheheni mashine za teknolojia ya hali ya juu kutoka China. Baadhi ya mashine hizo ni zile za ujenzi, vifaa na zana. Pua kulikuwa na bidhaa za kisasa za nishati ya jua, vipuri vya magari, bidhaa za kemikali na vifaa vya matibabu.

Maonyesho hayo ambayo yalifanyika wakati Kenya inapojitahidi kujikwamua kutokana na makali ya janga la virusi vya Corona, yamefungua milango ya ustawishaji kwa wafanyabiashara wa Kenya, kwa sababu walibadilishana mawazo na ujuzi wa kufanya biashara na wenzao kutoka mkoa wa Shandong, China.

Kwa mujibu wa mratibu wa maonyehso hayo, kampuni ya Afripeak Expo Kenya, jumla ya kampuni 117 zilishiriki, huku 83 ya hizo zikiwa kampuni za kigeni haswa kutoka China. Mkurugenzi mtendaji wa Afripeak Expo Kenya, Bw. Gao Wei amesema Kenya ilipewa fursa ya kuonyesha bidhaa zao na kutafuta soko kwa wafanyabiashara wa China. Bwana Wei alifafanua kuwa hii ni njia moja ya kuhakikisha kuwa China inaisaidia Kenya kujikwamua kiuchumi na kibiashara kwa kutangaza bidhaa zao kwa soko pana la China.

‘Tulitoa nafasi 20 kwa kampuni za Kenya kutangaza bidhaa zao. Kando na maonyesho, pia tulijaribu kuunganisha kampuni hizi za Kenya na wateja wa China,’ alisema bwana Wei.

Bwana Wei aliongeza kuwa maonyesho haya yalifana kwa sababu yaliwaleta pamoja wafanyabiashara wengi, mbali na Wakenya na Wachina.

‘kwenye maonyesho ya mwaka huu tuliongeza nafasi hadi mita za mraba 2,930. Tulikuwa na waonyesha bidhaa 117, wengi wakiwa kutoka China na wengine kutoka Kenya na India. Lengo letu kuu ni kusaidia kuinua viwanda vya ndani vya Kenya, haswa baada ya makali ya janga la virusi vya corona,’ alisema bwana Wei.

Kampuni za Kenya zilizoshiriki kwenye maonyesho hayo ziliteuliwa na chama cha wafanyibiashara cha Kenya. Meneja wa Afripeak Expo Bw. Vincent Muruba, amesema maonyesho ya nne ya bidhaa zinazouzwa nje ya mkoa wa Shandong nchini China, jijini Nairobi, yalifana na matarajio yao ni kuwa maoneysho ya mwaka kesho yatakuwa makubwa zaidi. Amedokeza kuwa huenda mikoa mingine ya China ikashiriki kwenye maonyesho ya awamu ya tano.

‘Mwaka kesho maonyesho yatakuwa bora zaidi. Tunataka kuanza mazungumzo na kampuni za Kichina za mikoa mingine ili kuzialika rasmi mwaka kesho,’ alisema bwana Muruba.

Takwimu zinaonyesha kuwa katika kipindi cha miezi tisa ya kwanza ya 2021, thamani ya biashara kati ya China na Kenya iliongezeka kwa asilimia 29.9 hadi kufikia shilingi bilioni 560 (kama dola bilioni 5 za Kimarekani) licha ya janga la COVID-19. Uwekezaji wa moja kwa moja kutoka China nchini Kenya ulifikia dola milioni 172 na thamani ya kandarasi mpya zilizosainiwa ilifikia dola za kimarekani bilioni 3.2.
 
Muende na Saudia kwenye maonyesho ya wafanyakazi wa ndani ( house maids)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…