Mapambano dhidi ya Ufisadi - wapi tunafanya makosa?

hapa hakuna kinachofanika, mi siko nyumbani lakini nimsesikia jinsi walivyotetewa akina hosea na mwanyika kuwa hawana hatia na juu ya richmond. riport ile ilikuwa wazi na ilieleza wazi wazi kabisa.
mabadiliko yanahitajika tena tubadilike toka ndani kabisa.sasa hivi niko sanoma ripori ya mwnakijiji hapa juu ya meremeta,ninachokiona siamini.nadhani hapa ndo pa kuanzia kama kweli tunataka mabadiliko
 
rushwa hasa zile ndogondogo...

Ulikuwa sahihi kabisa uliposema rushwa imekuwa utamaduni. Na lugha ni sehemu ya msingi kabisa ya utamaduni. Huu utamaduni wa kusema kuna rushwa ndogondogo ndio unajenga nafsi za kifisadi. Rushwa ni rushwa tu na fisadi ni fisadi tu hata umuite fisadi papa, nyangumi, kamongo, kibua, perege, changu au dagaa!

Siku Watanzania watakapokuwa tayari kusema kwa maneno na matendo kuwa "rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa" ndipo tutashinda kwenye haya mapambano dhidi ya ufisadi. Pambano linaanzia nafsini. Lazini tuzikane nafsi zetu za kifisadi!
 

Umesikika ndugu ila.. why dont u walk the talk by sharing your own experience on how you have been corrupt? This will break the ice....

Umenihukumu kuwa nimejitenga kwa kutumia lugha ya " wengine" je hiyo lugha ya nyekundu hapo juu unasemaje?....wewe siyo Mtanzania?
Anyway.. back to the issue.
 

Nyani haoni kundule. Asante kwa kunisahihisha. Siku Watanzania tutakaposema hivyo kwa dhati kabisa kutoka moyoni na akilini basi tutashinda vita. Kwenye mapambano kuna kujikwaa, kuanguka na kurudi nyuma ila kinachotakiwa ni kutokata tamaa daima.

Mimi bado napambana - niliweza kwenye suala la pasipoti japo ilibidi nitumie hela na muda mwingi ili kutota rushwa ambayo ilikuwa ndogo kuliko hizo gharama nilizotumia kuiepuka. Lakini nilijikwaa kwenye suala la kupita kwenye mpaka fulani niliposimamishwa kwa kuwa nilikuwa siioni kadi yangu ya homa ya manjano.

Aluta Continua - Mapambano yanaendelea! Vinceremos - Tutashinda!
 

maelezo mengi na na inafunza kwa namna nyingine na mabadiliko mengi inavyoonekana lakini mbona sioni adhabu ya watendaji, urahisi wa kupatikana kwa evidence kwa walio juu (openly), urahisi wa kumpeleka mtu yeyote Mahakamani ili ajibu shutuma dhidi yake.

Hivyo vyombo vyote hapo juu wanasema tu lakini havipo nje ya mdomo wa serikali sasa watakua na sauti gani na nguvu gani kitendo cha kumfukuza mtu kazi tu akitumi the right message kwa watendao. Hao majaji tu peke hawatoshi na polisi pia waruhusiwe kufanya uchunguzi wao na waweze kupeleka kesi mahakamani kwanza ni wao wanaodili na wafanya biashara wengi nchini.

Inabidi tujifunze kutatua matatizo kwa namna itakayo tatua matatizo sio kwa sheria za kiini macho, kusema si kutenda, kuunda tume au sheria si kutekeleza mabadiliko au hayo mapendekezo. Kuvipa hivyo vyombo nguvu yao bila ya serikali kuingilia kati ndio nguvu yenyewe na hapo utajua kweli wana nia ya kupambana na huo ufisasi.

Amini usiamini tatizo sio watu wale wale, hata ulete wengine wapya kwa sheria zilizopo na nguvu walizonazo katika muongozo wa leo hamna kitakacho badilika jaribu kuangalia tatizo lenyewe linatoka wapi, hebu jiulize kwa nini mtu kama Lowassa akufika mahakani hata kama hana makosa, kwa nini bwana mkapa asifike, mahakamani ata kama ana makosa hayo ni madia yao tu kumbuka na si ya wote, ata Liumba nae anadai ana makosa lakini yeye kaambiwa mahakama ndio iamue na kwa nini isiwe kwa wengine nao wanaoshutumiwa. sasa hapo ata ubadilishe uongozi wote ulete mwingine kwa sheria na nguvu walizo viongozi hasa rahisi uwezi kufanya chochote.

Kumaliza hii fitna ni kukubali kusamehe ya kale kwani hamna atakae kubali kutoa protection yake kwa sasa viongozi wenyewe ndio wanao imaliza hii nchii especially wa ngazi za juu na wenye madaraka ya juu secta zenye faida, hawa awali bila ya mwingine sasa nani atakubali mabadiliko ya kweli kwa uwoga tu wa kujiwa yeye. Kwa hivyo ukweli wenyewe ni msamaha wa yaliyopita na kuanza upya kuvipa vyombo vinavyohusika unlimited power na access hili wafanye kazi ya kweli vinginevyo ni mchezo its a fact.
 
Kwa hivyo ukweli wenyewe ni msamaha wa yaliyopita na kuanza upya kuvipa vyombo vinavyohusika unlimited power na access hili wafanye kazi ya kweli vinginevyo ni mchezo its a fact.

JC,
Umetoa wazo very interesting.KUSAMEHE NA KUANZA UPYA!
Mstari wa kusamehe utauchora kuanzia/kuishia wapi? Kumbuka vitendo vya rushwa/ufisadi huwa na mwanzo mrefu na matokeo yake ni ya baadae.Fikiria EPA ilianza lini na kugundulika lini?
 
Kwanza sipendi mambo ya kujisemea, kwa hivyo sidhani kama ntaanza kufafanua habari ambazo nazipata juu juu. Hila ninacho jua mimi amna aliyeshitakiwa wala kufungwa kwa suala hilo na mengineyo mengi yanayo lalamikiwa humu ndani.

sasa hapo sidhani kama historia yake itatusaidia chochote mimi na wewe hila cha muhimu baada ya kugundulika amna kilicho fanywa na wausika wana hishi bila ya woga na kuendelea kama kulikua amna jana. Hili ndio tatizo lenyewe, ni nini hasa kinachowafanya wajilingie hivi. Narudia tena ni kinga zinazo walinda si kingine. Sasa imagine Msamaha uje leo kwa yale yaliyopita, na vyombo vinavyo usika vipewe unlimited power to their investigation. labda leo uanze wizi mwingine mpya labda ni wa siri hata uchukue miaka kumi kugundulika ikiwa vyombo vinavyo usika vikija gundua yaliokuwa yana endelea watuhumiwa tuna guarantee watafika mahakamani, na kuadhibiwa vilivyo.

Hiyo ndio hoja yangu kwani kwa sasa, nguvu hizo hazi wezi toka, si EPA tu wala kesi nyingi zina semwa humu ndani hawa jamaa wanaishi kwa kutuibia we mwana sheria wa serikali ana afford vipi kununua nyumba uingereza ambayo akai kawanunulia wanawe, mzungu mwenyewe ananunua kwa morgate yeye cash around $ 400,000 katoa wapi hiyo hela ni mshahara wake wa miaka mingapi. Halafu mwanasheria huyo huyo wa serikali ndio mpambanaji na ufisadi. Ni kutoa nguvu tu, na msamaha ndio labda utawafanya waweze ona watakua salama wacha tu tuanze upya, na hou ndio upenyo tunao utaka sisi unlimited access to any investigation.

PS im off to work if u going to respond so if im qiute you know the reason till tmrw
 
Come on, hivi hao wananchi unaosema wataelimishwa na nani? na hao hao wala rushwa, na sisi M, na vyama vya upinzani, au na malaika special toka sayari ingine?
Kwani umesahau moto waliowashiwa wakatoliki kwa kujaribu kuwaelimisha hao unaowaita wananchi?
Na moto huu umewashwa na hao hao wala rushwa tena nyie baadhi ya watanzania mnawaunga mkono? nadhani very soon mtaitisha na maandamano ya kuunga mkono kauli za akina Kingunge Pagani!
 
Nakubaliana na wewe mama, maana kila mmoja hata mafisadi wakisimama jukwaani ulia kilio hicho hicho na sometimes unaweza usijue fisadi ni nani hasa.
Ninajua kisa kimoja live.
Nina rafiki yangu mmoja alikuwa anatafuta tenda kwenye taasisi moja na alitakiwa apigane kuipata.
Aliazimia kuwaona wajumbe wote wa kikao hicho ambao ni directors ili wamsaidie kupata hitaji lake. Alikubaliana nao kila mtu kupata rushwa yake ili at the end of the day wampe tenda hiyo. Alifanya hivyo. Na nilikuwa nawaona wote kila mmoja akija kwa wakati wake kuchukua chake na mmoja wao alikuwa ni katibu wa sisi M wa mkoa na hadi leo hii ni katibu wa sisi M wa mkoa mmoja wapo Tanzania hii hii.
Kitu kilichonisikitisha ni kusikia akiwa jukwaani huku akiisema vibaya rushwa huku ni siku chache tu katoka kuipokea kwa rafiki yangu. Sikuamini masikio yangu kwa jinsi alivyokuwa akiisema kwa uchungu wakati ni siku chache tu katoka kuipokea.
Huu ni unafiki na ndivyo wengi wa viongozi wetu wanavyojifanya kuichukia majukwaani na mbele yetu huku pembeni wanaipokea kama kawa.
Kama tunaichukia rushwa ni lazima tubadilishe utawala tulionao kabisa. Tupate kiongozi katili anayechukia rushwa kikweli. La sivyo itabaki ni hadithi ile ile ya kila siku. Hata tuunde institutions zenye majina ya aina gani. Hii ni kutupiga changa la macho wananchi na wahisani.
 
Rushwa ni tatizo kubwa tu la kitaifa na limekuwa likiota mizizi mirefu kiasi kwamba imekuwa taabu kweli kweli kuliondoa. Tatizo kubwa tulilonalo si watanzania na afrika kwa ujumla ni kutopenda kujifunza kutokana na makosa na pia kutotia shime katika kuziba mianya ya rushwa (ufisadi ukiwemo). scandal zilizotokea zingekuwa funzo tosha katika kutoa ufumbuzi ni wapi palikwenda kombo na jinsi gani tunaweza kurekebisha. Mfano, kuhusu taarifa ya tume kuhusu richmondi imetoa mapendekezo ya uwajibishwaji wa wahusika lakini je kuna jitihada gani zilizofanywa katika kuziba mianya iliyotoa nafasi ya ubadhirifu wa kampuni ya richmond? Na cha kushangaza zaidi serikali inakuja na tamko la kutoa onyo/karipio kwa baadhi ya watendaji! kwa msingi huu hatutafika popote. angalia kashfa ya iliyowakuta baadhi ya viongozi wa umma katika bunge la waingereza, pesa zilizohusika ni viduchu lakini kazi iliyofanyika ni kubwa mno katika kuhakikisha uwazi zaidi na uwajibikaji kwa viongozi.
Pamoja ni kwamba issue za ufisadi ni la kitaifa chama tawala nacho kinahusika kwa kiasi kikubwa tu na hakiwezi kukwepa lawama. na hata ikiwezekana hasira za wananchi. kwani ndiyo wasimamizi wa nchi kwa niaba ya watanzania. jiulize wanapopiga kampeni za uchaguzi huwa wanasema 'barabara hizi ni jitihada za chama tawala, mashule au huduma nzuri ni CCM ndiyo imeleta' basi hata kwa ufisadi na rushwa basi wajitishwe mzegamzega, ni mzigo wao!
 

Jirani maneno mazuri sana hayo. Wako Watanzania wengi sana ambao wanafuata sheria bila kutaka kupindisha sheria ili wapate upendeleo wa aina moja au nyingine na wala hawajawahi kufaidika hata indirectly na utoaji au upokeaji wa rushwa.

Nimekutana na Watanzania mbali mbali ndani na nje ya nchi ambao walikuwa hawana hata godfather au godmother wa kuwasaidia wapate upendeleo wa kufika pale walipo leo hii kimaisha. Wengi ni juhudi za binafsi na wala hawakutoka katika familia za kuwawezesha hata kutoa hiyo hongo. Wengi wa hawa ni wa miaka ile ya Mwalimu Nyerere ambapo rushwa ilikuwa ni ndogo sana kulinganisha na sasa ambapo imeshamiri kila kona na Kikwete na Serikali yake wameifumbia macho.
 
Last edited:
Rushwa imeshageuka utamaduni..njia ya maisha kwa watanzania.Pamoja na kuwa watu "wanachukia" rushwa, bado wanaiendekeza.....wanashiriki..kutoa na kupokea..kuanzia wasio na kitu hadi wenye vitu.

tatizo la mapambano dhidi ya rushwa ni kuwa yako based on a flawed assumption.. kwamba rushwa ni "adui wa haki". The reality ni kuwa rushwa ni rafiki wa haki.. so.. kwanini uachane na rafiki anayekuhakikisha haki yako? This is where we need to reinvent the wheel..
 

- Mkulu Bob, heshima mbele sana vipi mkuu kwa kifupi nimeongelea Wananchi wapenda mipira mipira, Ditopile na Mtikila, Shehe Yahaya, halafu Nchimbi na Masha, eti unasema maana yake ni Uisilamu?

I am sorry mkuu huwa siongelei wala kuchanganya dini na siasa, I m too big for that, yaani low politics ambazo ndio hasa zimetufikisha hapa, ila ukitaka kuwajua wadini humu JF ni kusoma vizuri tu hizi threads, utwaona huwa hawajifichi, lakini sio mimi no way!


Respect.

FMEs!
 

- Strong point mkuu na tupo pamoja sana hapo, ingawa pia kutoka familia zenye uwezo sio a crime na si kweli kwamba watoa rushwa Tanzania ni wale tu wanaotoka familia zenye godmother na godfather, unless una dataz za kui-back up hii hoja!

Respect.

FMEs!
 
yebo yebo, nenda kaendelee na kazi yako ya UWT.... unahitaji nini ili uweze kujua watu wale wale, chama kile kile ndo kina endeleza mambo yale yale tangia mwaka 1961. Hao ndo adui namba moja wa kupambana na rushwa..


TANZANIA WILL NEVER DEVELOP UNDER CCM
 
Wakati mwingine ni vyema tukaongea kwa dataz na facts:-



Source: Bimirngham University, UK.

 
1. A Critique of the History of Combating Corruption in Tanzania


Despite increasing evidence from our personal experiences, legal documents and other documentation in general that corruption in Tanzania is rampant, the public feeling and opinion does not show a sense of remorse or public anger at the phenomenon!

- It seems even no longer useful to debate on the success of efforts to combat. The society at large now seems to take corruption for granted. But almost nobody is aware of its consequences in our society, namely moral decadence.

- A historical analysis of the efforts against corruption, on the other hand, reveals that Tanzanians have not made use of their moral and ethical assets, instead they have depended on political and legal institutions which in fact have become a liability!

- It is ironical that the 1967-1985 period was the period of emergency and wide spread corruption. A critical analysis of the reasons for this will show that corruption rose not because of the certain economic developments negatively affecting the performance of the economy, but rather because selfishness of the leaders took advantage of the suffering of the people. Those with power and influence, rather than living simply so that others might simply live exploited to the full the situation. For that reason it was too late for the government in 1982 to declare war on corruption and other forms of bribery. Also the manner of combating corruption was charged with political emotions and ideological apartheid. It is true that number of corruption cases decreased on the average (Maliyamkon & Bagachwa 1990); but this actually drove underground the practice, and so the spirit was still alive!

- Today we the civil society has the right to ask critical questions about the recent official efforts in combating corruption. For example, Why has the legal enforcements not abated the prevalence of corruption? Why is it that the achievements of PCB and of the Warioba Commission are not made public? Why is transparency not working in this regard? What is the implication here in Tanzania of the Southern & Eastern Africa Ministerial Forum Against Corruption, which was formed in Pretoria, December 1994? And there are many more and more questions...!

- The point here is that our concept of corruption is not yet inclusive enough to enable us to deal with non-legal issues of corruption as well. For many people a legalistic concept of corruption is enough, but my argument here is that it is not. Too many DO's and DON'T's in combating corruption has not helped us very much. If it were just a matter of laws and legal enforcement corruption would no longer be with us today. Many countries have so many laws; Tanzania has had so many
 
Field Masrshall Es,
Unaweza wadanganya wengine lakini sii mimi mkuu wangu...
Unajua kinachotufanya tuwe NDIVYO TULIVYO ni kutokana na kutozungumzia chimbuko la matatizo yetu badala yake tunazungumzia matatizo yenyewe na kuvuta hisia zetu..Na unaweza kuweka majina yoyote yale ila cha msingi ni hoja yenyewe inalenga wapi.. Tunakusoma..
Wewe na mtu mwingine yeyote yule anajua fika kwamba Ditopile kapewa dhamana sii kwa sababu ni Muislaam ila kwa sababu ni mtu wenu CCM. hata angekuwa Mkristu au Baniani maadam ni mshikaji wa JK na mwenye wadhifa ndani ya chama hicho asingeweza kukaa ndani..Iwe Mwadosya, Kingunge, Masha au Lowassa.. wote hawa wanapewa kinga na chama chako..That's the bottom line.

Sasa unapozungumzia waislaam ambao walisimama for Ditopile kumbuka hata aliyeuawa ni Muislaam. Wapo waislaam na Wakristu waliopingana/waliounga mkono na dhamana ile. Hakimu aliyetoa dhamana sii Muislaam wala Prosecutor wake na haikuwa sababu hata kidogo.. Hivyo kitu cha kulaumu kwa pamoja ni mfumo mzima wa sheria nchini ambapo tunawaona viongozi hasa wa CCM wakisimama juu ya sheria..

Katika kesi ya jinai yoyote ile wapo watu watakao kuwa upande wa pili na sii wajinga ila ndivyo sheria inavyojengwa..Till proven Guilty au sio.. hata kama alikusudia kuua ni kazi ya mahakama..
Mkuu wangu hata Mapadre hufanya maovu na kanisa likasimama kuwatetea, hii haina maana wao wajinga ila wanafuata kinga za kanisa lao kutokana na wadhifa wa mhusika. Na hadi itakapo kuwa proven ndipo kanisa humtema mtu huyo. Tumeona kina Lowassa na Rostam wote hawa wakipewa kinga na wapo watu wanamuunga mkono jambo ambalo mimi binafsi siwezi kutumia dini ya mhusika kuonyesha ujinga wa wafuasi wa dini hiyo wala haiwezi kuwa kielelezo cha haki..Ya Masha ya Nchimbi umewazungumzia wao ktk kujenga ukubwa wa matatizo tulokuwa nayo..hivyo kesi yao haihusiani na zile zilizotangulia...

Mkuu wangu nawaombeni sana, jaribuni sana kuondokana na swala la ku lebel watu wakati wakidai haki zao hata kama haileti maana kwako..Umezungumzia pia mahakama ya kadhi.. Ni mtazamo wako ambao binafsi sioni kosa wala ubaya wa hoja hiyo kwani hapa Wahindi Masingasinga wamepewa sheria yao kutembea na majambia yao wakati hairuhusiwi kwa mtu asiyekuwa na imani ya dini hiyo..

Nitazidi kusema kama unapingana na mahakama ya kadhi zungumzia vilivyomo ambavyo wewe hukubaliani navyo na sii kutumia jina la dini kupinga..kwani kufanya hivyo unapingana na mtazamo wa diversity..Tupambane na Ufisadi kwa kutazama kiini chake, tusiwe na fdikra kama za viongozi wenyewe ambao hata kupambana na Maleria tu imetushinda wakati wakijua fika kwamba chanzo chake ni mbu kuzaliana ktk madimbwi ya maji yaliyosimama..walichofanya ni kuomba vyandarua na dawa nyingi sana za kutibu Maleria..Watu wanazidi kufa kwa hesabu kubwa kuliko wakati wowote uliopita!
Beside that It's all good!
 
WoS,
Rushwa imejijenga katika Tanzania hadi kufikia kuwa ni sehemu ya utamaduni wetu. Hebu jikumbushe ulipokuwa Chuo (Kama ulisoma pale UDSM), mawazo ya kila mwanafunzi akitoka pale ataimbishaje ili atengeneze pesa za chapchap. Hayo mawazo pekee ya kupata pesa chapchap tayari yanaashiria kuwa pesa itatafutwa kwa njia yeyote ikiwemo rushwa. Ukienda katika maofisi ya serikali nk kila mtu anawaza atatengenezaje pesa ya chapchap...atatafuta pesa kwa kuiba au hata rushwa ilibidi. Ukienda katika nafasi za viongozi hali ni hivyohivyo. Waandishi wa habari, ndiyo usiseme, ukienda mahakamani, loh wanasheria na mahakimu/majaji wanafanya 'kolabo' halafu wanatoka na single yao.
Anyway kimsingi jamii yote imeoza kwa hiyo inahitajika mikakati ya ziada ya kuturudisha katika ground zero. Mimi binafsi ninaona tatizo la rushwa ni kubwa mno kuliko tatizo lingine lolote katika Tanzania na litachukua miongo na miongo kuweza kupatikana kwa unafuu.
Wengi wa wale wanaopambana rushwa wakiwa nje ya mifumo ya serikali (wanaharakati) ni walarushwa vivuli kwa maana hawajapata nafasi na punde wakiziipata basi nao huanza kazi ya kula rushwa mara moja.
Nini kifanyike? tuendelee kuilaani na pia kila mtu aseme kuwa sitatoa rushwa asilani!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…