YeshuaHaMelech
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 2,596
- 37
CCM walikupa nini?CCM inakubali kuwa kulikuwa na mapungufu, ndio maana mh. Rais alisema hivyo wakati wa kupokea matokeo. Alisema ni vyema tume ikaangalia jinsi ya kuyaondoa mapungufu hayo in the future.
CCM haikubaliani na hysteria inayoonyeshwa na Chadema. Mazungumzo ni jambo ambalo CCM imelikaribisha kila siku, ila mwenyekiti wa CCM ambaye ndio Rais ya Jamhuri hawezi kuanzisha mazungumzo na chama kisichomtambua.
Kubalidilishwa au kuboreshwa kwa katiba ni wazo sahihi, lakini lina taratibu zake. Among hizo taratibu, kutokumtambua Rais na kususia hotuba zake haipo.
Unaweza kufanya mazungumzo na mamlaka usiyoitambua. Ilishatokea Afrika kusini. ANC hawakutambua utawala wa makaburu lakini hatimaye walifikia muafaka.Tofauti ilitakiwa iwepo lakini unfortunatelly kwa CCM mwenyekiti wa chama ndio mkuu wa serikali. Kwahiyo hakuna tofauti hapo, swala la kumtambua kabla ya kuanza mazungumzo haliepukiki.
CCM inakubali kuwa kulikuwa na mapungufu, ndio maana mh. Rais alisema hivyo wakati wa kupokea matokeo. Alisema ni vyema tume ikaangalia jinsi ya kuyaondoa mapungufu hayo in the future.
CCM haikubaliani na hysteria inayoonyeshwa na Chadema. Mazungumzo ni jambo ambalo CCM imelikaribisha kila siku, ila mwenyekiti wa CCM ambaye ndio Rais ya Jamhuri hawezi kuanzisha mazungumzo na chama kisichomtambua.
Kubalidilishwa au kuboreshwa kwa katiba ni wazo sahihi, lakini lina taratibu zake. Among hizo taratibu, kutokumtambua Rais na kususia hotuba zake haipo.
CHADEMA ni lazima wafukuzwe BUNGENI halafu tuone watakachofanya. Baadhi ya viongozi wa CHADEMA hawana busara hata kidogo. Wengi wao hawafai hata kuongoza kata. Wameukwaa ubunge kutokana na makosa ya CCM yenyewe. Lengo la CHADEMA ni kutaka amani ivurugike. Sasa kuiomba CCM eti itumie busara wakati kuna wana-CHADEMA wanataka siasa za ubabe ni kutaka kuionea CCM. CHADEMA wamelianzisha na sasa wawe tayari kukabiliana nalo. Wamelilia wembe na wembe huo wataupata. Tuone huyo Mbowe atafanya nini, Tuone huyo LISSU atafanya nini.
4. Ccm isijaribu kwa namna yoyote kutekeleza tishio lake la kuwafukuza wabunge wa chadema bungeni. Tayari taifa limeshagawanyika na kitendo chochote kitakachoonekana kuwa ni cha kibabe (wengi tunakumbuka suala la zitto na buzwagi) kitakoleza mgongano wa kisiasa nchini. Kuwafukuza chadema hakutasababisha watu wakubali isipokuwa kama watawapeleka mahakamani watanzania wote ambao hawako tayari kutambua ushindi wa kikwete na kuwalazimisha kukubali ushindi huo chini ya tishio la kifungo. Vinginevyo, hekima kubwa inatakiwa kutumika na mimi ninaamini hekima hiyo inaanzia na🙁quote)
chadema ni lazima wafukuzwe bungeni halafu tuone watakachofanya. Baadhi ya viongozi wa chadema hawana busara hata kidogo. Wengi wao hawafai hata kuongoza kata. Wameukwaa ubunge kutokana na makosa ya ccm yenyewe. Lengo la chadema ni kutaka amani ivurugike. Sasa kuiomba ccm eti itumie busara wakati kuna wana-chadema wanataka siasa za ubabe ni kutaka kuionea ccm. Chadema wamelianzisha na sasa wawe tayari kukabiliana nalo. Wamelilia wembe na wembe huo wataupata. Tuone huyo mbowe atafanya nini, tuone huyo lissu atafanya nini.
Unajua hili suala siyo kubwa wala gumu kiasi hicho; ninaamini mzigo wa jinsi gani litaisha ni kwa CCM. Wasipotumia hekima wanaweza kutengeneza mashujaa wengine tena wengi zaidi. Walipomfungia Zitto kwenye Buzwagi lilikuwa dogo kwenye hili itakuwa vurugu sana.
You don't ask for your tights rather you demand your rights, sasa Chadema wamekuwa waungwana sana na pia wanaonyesha kuweka maslahi ya taifa mbele sana, kwa lile vugu vugu iliyokuwepo wakati wa kutangaza matokeo wangeamua kuwatangazia watanzania kuingia mtaani kudai haki yao hivi hata hilo bunge leo lingezinduliwa!! tuwe wakweli CCM wamefanya wizi na hakika wanajua kama ni wezi!! don't tell me kwamba hawana hata akili ya kujua kuwa watanzania wanajuwa kuwa wamepokonywa haki yao!! Hivi nani mkosaji kati ya hawa wawili yule anayepiga kelele au ukunga wa mwizi, mwizi, mwizi ama ni yule mwizi aliyeiba? anachofanya chadema ni kumpigia ukunga mwizi, you can't have it both ways huku unakwiba na huku unataka ustaarabu wa kutokuitwa mwizi. CCM waache udhalimu , mabaya waliokwisha kutufanyia watanzania yametosha wasitake mengine,
Lakini lawama kubwa zaidi ni hawa watu wanaofanya kazi bila kufuata ethics za kazi zao watumishi wa umma ama watumishi wa taasisi za serikali wanapogeuka kuwa vibaraka wa CCM!! Maana kama Tume ya uchaguzi wangekataa kata kata kutumiwa na CCM kufanya waliofanya haya yote yangetokea wapi, hapa lawama wala si katiba , hapa lawama na laana zielekwezwe kwa watu wa tume na taasisi nyingine zilizopelekea uchaguzi kutokuwa huru na haki, inakuwaje watu wameona yaliyotokea kenya kwa makosa ya Tume ya uchaguzi ya kenya leo hii Tume ya Tanzania inafanya yale yale!! hawa watu wa Tume sioni hata adhabu wanayostahili ukiwacha kuwanyonga adharani maana uroho wao unataka kusababisha taifa liingie katika kukosa amani yake. Mimi siwalaumu CCM sana maana Tume hawakuforciwa kuiba at gun point!! wangeweza kuwa wakweli au wakasema tunajiuzuru we would not be talking about this today.
Nashauri watumishi wa serikali na taasisi zake watambue kuwa wanalipeleka taifa kubaya kwa kuacha kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu na kugeuka kuwa vibaraka wa CCM hawa ndo wanastahili adhabu kwanza alafu ifuatie CCM kwa kuwashawishi watumishi wa serikali, na mwisho CCM at least waoneshe kuwa dhamira inawasuta kwa wale waliotenda hivi watuonyeshe ustaarabu japo kidogo
Mungu Ibariki Tanzania
nafikiri watu bado hawajawaelewa Chadema, viongozi wake ni watu makin sana, sasa ukichukua tu propaganda za CCM utakuwa umepotea. Msimamo wwa Cahdema ni kuwa hawana shida na Kikwete kama yeye, na kuwa wanafahamu sheria kuwa NEC ikishatangaza hakuna mahali unapoweza kupinga. Sasa zingatia yafuatayo:
1. Chadema wanatambua kuwa JK ni Rais isipokuwa wanachokataa ni matokea yaliyomweka madarakani. Ni Rais kwa kuwa ametangazwa na NEC na hakuna mahakama inayoweza kubatilisha.
2. Kinachopiganiwa sasa ni kubadilisha mfumo huu unaoweza kumweka madarakani mtu ambaye hakuchaguliwa na watu. Na wanaonyesha ukweli huo kwa takwimu za kura zilizopigwa vituoni na zile zilizotangazwa na NEC
3. Kinachopiganiwa ni kuandikwa kwa katiba mpya na kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi. Hiki ni kilio ambacho wapinzani wamekilia kwa muda mrefu lakini CCM wameweka pamba masikioni. Ili hili lililotokea lisionekane katika uchaguzi ujao hili ni la lazima. Nakumbuka kuna wakati CUF waliandamana kudai tume huru lakini baada ya ndoa yao na CCM hawalisemi kabisa hili.
4. Kama CCM itajali hili na kuanza mara moja mchakato wa kuweka katiba mpya, misuguano itakuwa imekwisha, lakini kama CCM watakaidi kilio hiki wawe na uhakika kuwa matukio mengi na migawanyiko ya taifa itaendelea kulitesa taifa hili na kamwe agenda ya maendeleo haitapata nafasi kabisa.
KATIKA UMOJA WETU WATANZANIA BILA KUJALI ITIKADI ZETU ZA KISIASA TUJALI TANZANIA YA KESHO, AMBAPO WATOTO WETU WATAISHI KATIKA MAELEWANO NA UHURU NA HAKI.
Hiyo underlined ni kauli yako wewe lakini si ya viongozi wa Chadema (with exception of Zitto Kabwe).
Mahitaji ya katiba mpya nakubaliana nayo lakini natoa angalizo kama ifuatavyo:
1. Katiba iliyopo haijaruhusu tume ya uchaguzi kumtangaza mgombea mwenye kura chache kuwa mshindi. Hivyo basi, kama hilo lilitokea, lilikuwa ni kinyume cha katiba. Hata ikija katiba mpya haitakuwa tiba ya hulka za kutokuheshimu sheria.
2. Mahitaji ya katiba mpya hayatekelezwi kwa kumdhalilisha yule unayetaka majadiliano naye. Kitendo cha kutoka wakati Rais anatoa hotuba, pamoja na kufikisha ujumbe wa kutokumtambua, pia umemdhalilisha. Je, unatarajia response gani toka kwa mtu uliyemdhalilisha? Chadema wamejiweka katika mahali ambapo ni lazima wakubali kumtambua Rais kabla mijadala mingine haijaendelea.
Na wewe hebu taja vifungu vya sheria na kanuni sio bla bla hapa. Nchi inaongozwa kwa sheria hii na si vinginevyo.
Kudhalilisha is a relative term, mie hapa naona unajidhalilisha tu.