Habari zenu wana jf,leo napenda kuwasilisha mada kuhusu mapenzi,heshima na urafiki kati ya watu hasa wa dini tofauti.kipindi hiki ambacho nchi yetu tz ina shutuma nyingi za udini na hata muungano unapelekwa kwenye udini naona nipate mawazo ya wengi kuhusu hii mada. Kwa ufupi napenda wana jf mtoe kumbukumbu ambayo unayo ya mapenzi,heshima au urafiki ambayo ushawahi kuonyeshwa na mpenzi/rafiki au hata jirani wa dini tofauti,namaanisha kitu ambacho kimekugusa sio mapenzi y kununuliana bia au kumpisha mtu kiti kwenye basi.namaanisha mtu wa imani nyingine kwenda 'beyond call of duty' kukuomyesha heshima/urafiki au mapenzi hasa pale unapotaka nafasi ya kufanya mambo yanayohusiana na dini yako.Labda tukilichambua hili tunaweza kurudisha heshima na upendo miungoni mwetu bila kujali dini ya mwengine,tukitilia maanani ingawa dini huwa tofauti lakini nia ni moja.