MAPENZI Vs ELIMU

MAPENZI Vs ELIMU

Lady

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2010
Posts
282
Reaction score
62
Hivi wana jf, kuna uhusiano wowote kati ya mapenzi na elimu?
Ni muhimu kwa wapenzi kuwa na elimu sawa?
Inakuwa vipi kwa mwanaume anapomzidi mwanamke kielimu?
Inakuwa vipi kwa mwanamke anapomzidi mwanaume kielimu?
Toeni mawazo yenu wadau!
 
kwa mimi naona yote sawa tu. mwanamme akizidi elimu au mwanamke. ........
ni sawa na kuwa mwanamke ana biashara yake ambayo inampatia kipato kikubwa sana kuliko cha mumewe.( sidhani kama ni issue japo kuwa wanaume wengine hawawezi kuishi katika misingi hiyo)
 
Kuna uhusiano wowote kati ya mapenzi na elimu?
Hakuna uhusiano. Kitu mapenzi kinakuja naturaly. Unampenda mtu kutokana na tabia, sura, umbile. Labda elimu ni nyongeza tu, lakini haijengi penzi. Elimu SIO MSINGI WA PENZI.

Ni muhimu kwa wapenzi kuwa na elimu sawa?
Sio muhimu. Cha muhimu hapa ni maelewano, kuheshimiana, kuvumiliana na kusaidiana katika kutafuta ridhiki.


Inakuwa vipi kwa mwanaume anapomzidi mwanamke kielimu?
Ukimzidi mwenzako elimu, haibadili kitu katika upendo, haizidishi wala haipunguzi upendo halisi. Labda yawe mapenzi ya pochi.
 
Mapenzi hayana hela wala elimu yoyote akimzidi mwenzake sawa tu ili mradi siku ya mwisho ndani ya mapenzi hayo kama yakienziwa vilivyo elimu hiyo inawasaidia wote wawili!
 
Mapenzi huwa yanaanza kwanza kisha vigezo vingine kama elimu, pesa umaarufu n.k ndo vinafuatia.
 
Ki dhana hakuna mahusiano yeyote ya mapenzi na elimu lakini practically mahusiano yapo.Kutokana na mfumo dume tulionao mwanaume akiwa na elimu zaidi ya mwanamke huwa haina shida kabisa lakini mwanamke akiwa na elimu zaidi ya mwanaume tatizo huanza hapo..Inferiority na superiority sndrome huharibu mapenzi ya wawili hawa....Kuna mifano mingi tu hai imetokea,couple hizi huwa hazi match kabisa mwanamke digrii mwanaume std seven ni ishu kubwa. wengi wameshindwa kudumu hata kama wamependana kwa kiasi gani..Labda mwanaume akiwa na pesa zaidi ya mkewe hawa wanaweza kwenda hata kama hana elimu kabisa hata ya darasa la saba..
 
wanaume hawa wezi kuchukua wanawake kuwa na elimu ya kuwazidi sana, au kuwa na pesa zilowazidi sana...............maugomvi huwa hayeshi nyumbani, kitu kidogo kama si mume basi familia yake utaambiwa mwanamme unaendeshwa kwa kuwa kakuzidi elimu
 
Elimu ni artificial thing, Love ni natural thing you can not compare hata siku moja.

Ukiona mtu anasema nitaoa au kuolewa na msomi basi upendo haujaanza, if love is not bounding.... then thats is a declariotion of the broken marriage,NDOA iliyovunjika kabla ya kuanza! matatizo mengi ya ndoa ni kutokana na watu kukosa upendo wa kweli wakorinto wa kwanza 13 ina maliza kila kitu!
 
wanawake wenye elimu iliyozidi waume zao au vipao vyao hata kama kuna mapenzi ya ukweli ndani yake lakini kwa maumbile ya kike watu wa jinsia hii huwa na dharau ya asili ambayo kama sio leo kesho au keshokutwa atakuja kuionyesha hasa pale mwanaume utakaposhindwa kufanya kitu fulani ama kwa kukosa elimu au kipato basi anaweza kukuleteta jeuri ya wazi wazi kwa kuwa tu yeye ana uwezo wa kufanya hivyo, tofauti na wanaume wao hawako namna hiyo.
kama unataka kuwa na mahusiano na watu hawa(kike) be very carefuuly nad never trust them 100%.
 
Back
Top Bottom