Mapenzi yalikuwa zamani jamani

Quinton Canosa

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2012
Posts
1,224
Reaction score
1,250
Mapenzi ya zamani raha sana mwanamke anatoka Kwao kabeba chakula kwenye hotpot hadi ghetto kwako
Hawa wa siku hizi sio romantic kabisa anachokibeba yeye toka kwao ni chaja ya smartphone tu,hata hela ya nauli hana
 
Labda wa mjini lakini wa huku vijijini kwetu bado wapo sana wa hivo
 
dah umenikumbusha nilikuwaga Makambako nilipata kabinti jirani na nyumba ninayoishi kalikuwa kananiletea wali usiku nyama zimefunikwa uzioni yaani ile unapiga kijiko hakiendi kumbe chini ya wali ni full manyama-nyama.
 
na a
Mapenzi ya zamani raha sana mwanamke anatoka Kwao kabeba chakula kwenye hotpot hadi ghetto kwako
Hawa wa siku hizi sio romantic kabisa anachokibeba yeye toka kwao ni chaja ya smartphone tu,hata hela ya nauli hana
huyu wa chaja bila nauli akifika gheto anahitahu na chips yai kwanza
 
dah umenikumbusha nilikuwaga Makambako nilipata kabinti jirani na nyumba ninayoishi kalikuwa kananiletea wali usiku nyama zimefunikwa uzioni yaani ile unapiga kijiko hakiendi kumbe chini ya wali ni full manyama-nyama.
Ha ha ha umekumbuka mbali eeeh mkuu,zamani raha sana
 
Mkuu hujapata tu akupendae, kaa utampata anayekupenda ma kukujali yote hayo utayapata
 
Mimi huku ifakara nmeng'oa toto la kisukuma. Basi ni fulu kula mahindi ya kuchoma kila tunapokutana..! [emoji6][emoji6][emoji6]
 
Duuh! Nimekaa na kuwaza zamani hiyo ni ipi jamaani.

Sababu malezi waliyopata wasichana wa zamani ilikuwa ni ngumu kwa mtoto wa kike kuyafanya yote hayo hasa akiwa anaishi kwa wazazi wake.

Pia niseme tu acheni kupenda vya kuletewa sababu vingi vinakuwaga na masimango.
 
Mapenzi ya zamani raha sana mwanamke anatoka Kwao kabeba chakula kwenye hotpot hadi ghetto kwako
Hawa wa siku hizi sio romantic kabisa anachokibeba yeye toka kwao ni chaja ya smartphone tu,hata hela ya nauli hana
Na akifika getto ana njaa
 
Hajar ndio maana nasema mapenzi yalikuwa zamani...think beyond the box,what i mean here is the glass was full of water during those previous days.
 
tangu zamani hadi leo hujaoa unasubiri nini ?
kwanini hukumuoa huyo au ndio kuchangamsha genge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…