Papy ndombe
JF-Expert Member
- Oct 24, 2020
- 3,761
- 4,535
Mm nipo upper nazungumzia majority.Kwani uper na Middle Income eaner kwanini nawewe usiwe sehemu yao.
Au unataka wote Wawe kama wewe, acha akili za Kimasikini kirusi wewe
Unaposema kuwa kuchimba chuma ni gharama na kunahitaji teknolojia kubwa unatakiwa kuanisha siyo kusema maneno matupu. Ndiyo nyie mnakubaliana na hali ya sisi kuuza ngozi Italy na kisha waitaliano kuja kutuuzia viatu, mikanda na Wallet. Mnasema kutengeneza viatu ni gharama, kunahitaji teknolojia kubwa, inahitaji ujuzi!.Mkuu hawa ndg zako wanaidi madini yoyot yanachimbwa kama mihogo shambani
Ni lazima tuna na Economic evaluation & analysis yakutosha ili uchimbe chuma ni lazima hu_ improve kwenye high technology
Ndugu kujifananisha na China kwenye soko la chuma ni sawa na mbingu na ardhi; sio Tanzania tu nchi yeyote duniani.Sijaweka ushabiki wa kisiasa hapa. Miradi kama hii ambayo inaweza geuza kabisa uchumi wa nchi huwa inapata upinzani mwingi sana. Niliandika kwenye jukwaa la great thinkers jinsi US ilivyomzuia mjapan kumuuzia Korea Kaskazini kinu cha kufua chuma. Alijua umuhimu wa chuma kwa nchi.
Hapa kwetu mtu anaweza pinga kwa ajenda mbalimbali. Labda ni mkenya hataki Tanzania iwe na chuma, Labda ni msauzi anaogopa upinzani sokoni nk. Wazo la ubishani wa kisiasa halikuwepo kabisa.
Chuma hata usikiingize kwenye kucompare na uwekezaji mwingine kwenye ishu za opportunity cost. Chuma ni kama elimu, hospitali, barabara, madaraja na vitu vingine vya msingi kwa nchi. Hii siyo bidhaa tu ya kuuza na kununua, ni kitu cha msingi kama elimu na afya. Inatakiwa kufanya kila njia kuwa nayo.
Unafikiri kwanini wachina wako tayari kutoa Ore Njombe, kusafirisha mpaka Mtwara kupakia kwenye meli mpaka uchina? Unafikiri imeweza kuwa mzalishaji namba moja duniani kihivihivi?. Kama yeye ameweza kusafirisha chuma toka Brazil, SA na Australia na anaona kuna faida, sisi tunashindwa nini kuchimba na kusafisha hapo hapo?
Hakuna anaesema tuanze kama China alivyo leo. Tunaanza chini. Unaangalia mahitaji ya nchi kwa mwaka na kuanza na kiwango hicho. Unaendelea kupanua kulingana na soko. Unaanza na vitu basic. Hivyo vyuma sijui vya kwenye oil rigs ni mambo ya baadaye. Tunaanza na chuma cha kufaa reli, nondo, nut, bolt, baiskeli, shoka, jembe, nk. Vitu basic. Marekani hawazalishi sababu ya gharama kubwa za mishahara na mambo ya mazingira. SA wana chuma cha kuwafaa wao na kuexport pia. Kila nchi ina hali na changamoto zake. Siyo sababu Marekani hawachimbi chao basi na kwetu haitawezekana.Ndugu kujifananisha na China kwenye soko la chuma ni sawa na mbingu na ardhi; sio Tanzania tu nchi yeyote duniani.
China ananunua 60% ya iron ore inayochimbwa duniani na wachimbaji wote wakubwa wa iron ore mteja wanaemtegemea ni mchina (matter of fact yeye ndio ana influence flactuation ya iron ore market price, based on their annual demand).
China ana umeme wa kutosha wa bei nafuu kupunguza gharama za uzalishaji, ana advanatages za huge economies of scales kwenye resources mobilisation na kwenye kuzalisha final product.
Ana soko kubwa la bidhaa zake duniani haya ma sky-scrapers yanayokwenda angani kupitiliza yanatengenezwa kuhimili earth quakes na makash makash mengine nature inayoweza yatupia; chuma kinachotumiwa sijui kinatakiwa kuchanganywa na mineral gani kiwe stable zaidi, kuna wengine kwenye madaraja makubwa wanataka vyuma strong ila vinauwezo wa ku sway, huko kwenye offshore rigs nao wana specifications zao; mchina ndio mwenye technology and cheaper cost za ku meet a variety of design specification na ndiye anae supply chuma kwenye miradi mikubwa mingi duniani including US and EU.
Ana uwezo wa kuja africa kutafuta tender za ujenzi utakaoitaji chuma, akazikopesha nchi za Africa zisizo na uwezo wa kifedha, akajipa yeye tender na akatekeleza hiyo miradi kwa kutumia chuma kutoka kwao.
Juzi kwenye mkutano na waziri wa china ulimskia Magufuli akisema in the past 10 years kampuni za kichina zimepata tender za almost $10 billion kutokana na miradi waliyofanya Tanzania.
Back to the point investment ya kuchimba iron ore is capital intensive na viwanda vinavyofuata i.e at secondary and tertiary level na vyenyewe ni expensive to build and to run. Sasa uwezi kusema utajenga tu without showing the investment appraisal ata hao S.A wenye reserve ya chuma zaidi yetu wanauza more iron ore to China than what they use to produce for their own markets, US wenye reserve ya billion tonnes of iron ore (many times more than what we have) pamoja na viwanda vya chuma wananunua kutoka China for the most part.
Haya mambo ni easier Said than done once you start crunching the numbers on investment return.
Economic analysis ilishafanywa .... Accoding to Zitto sometimes ago, TZ inaweza kuingiza kama U$ 5 Billion kila mwaka kwa chuma tu. Hayo ni mapato makubwa kuliko dhahabu na Almasi combined!Hahahaaaa acha kuota mkuu, we are after money, hatuchimbichimbi, you can not extract minerals before doing an economical analysis. Is it economical?
Basi kama ni hivyo mkuu, kuna haja ya serikali kutupia jicho kwenye chuma. Japo extraction ya chuma kutoka ore (hamatite au magnetite) inahitaji tutumie makaa ya mawe. Je makaa ya mawe yapo ya kutosha kwenye eneo hilo.Economic analysis ilishafanywa .... Accoding to Zitto sometimes ago, TZ inaweza kuingiza kama U$ 5 Billion kila mwaka kwa chuma tu. Hayo ni mapato makubwa kuliko dhahabu na Almasi combined!
Hakuna anaesema tuanze kama China alivyo leo. Tunaanza chini. Unaangalia mahitaji ya nchi kwa mwaka na kuanza na kiwango hicho. Unaendelea kupanua kulingana na soko. Unaanza na vitu basic. Hivyo vyuma sijui vya kwenye oil rigs ni mambo ya baadaye. Tunaanza na chuma cha kufaa reli, nondo, nut, bolt, baiskeli, shoka, jembe, nk. Vitu basic. Marekani hawazalishi sababu ya gharama kubwa za mishahara na mambo ya mazingira. SA wana chuma cha kuwafaa wao na kuexport pia. Kila nchi ina hali na changamoto zake. Siyo sababu Marekani hawachimbi chao basi na kwetu haitawezekana.
Ni ngumu nchi kuendelea bila chuma, kama tu ilivyo ngumu kuendelea bila elimu au afya. China angekuwa na mentality kama yako asingefika alipofika leo.
Zama za chumaChuma ndio madini mama duniani, mapinduzi makubwa duniani yameletwa na matumizi ya zana za madini ya chuma, ni heri uache vyote ili uchimbe chuma kama unayo. Tena huna haja ya kutafuta mwekezaji kwenye madini ya chuma chimba mwenyewe.
Taifa lengo malengo litachimba chuma kwanza hata kabla ya dhahabu na nickel. Yaani kwa umuhimu itaanza chuma na kufuatiwa na makaa ya wawe, shaba, bati na dhahabu.
Chuma ndiyo itatumika kutengenezea zana kuchimbia madini mengine na njia za kusafirisha madini mengine.
Inaonekana uchimbaji wa chuma haupewi msukumo mkubwa kwakuwa hauna maslahi kwa viongozi mmojammoja, maana huwezi kuficha kipande cha madini ya chuma kwenye begi lako kama dhahabu na almasi.
Usiulizie bei ya chuma duniani bali ulizia bei za bidhaa za chuma duniani kama vile nondo, vyuma vya madaraja, mataruma ya reli, makontena, heavy machines kama skaveta, matrekta, combine harvesters, fork lifts, mitambo ya viwanda, bati, meli, malori, nk ni bei gani?Eeenh, Sawa mkuu 'Mokaze'.
Wewe ni 'mhunzi'?
Nimependa ulivyoeleza jinsi ya kupata hivyo vyuma vya aina mbalimbali,... hebu endelea hadi kule kwa 'graphine basi; kwa vile naona una mwelekeo wa kuyafahamu haya mambo!
Nimesoma hii mada hadi nilipofikia mchango wako nikaona kuna urahisishaji wa mambo mengi yahusuyo chuma.
Ndiyo, pamoja na kuendelea kuwepo na umuhimu wa madini haya katika matumizi mengi, tusisahau kwamba teknologia imekwishakuwa kubwa na kupanuka zaidi. Hatuwezi kukiona chuma katika mwonekano uleule uliokuwepo miaka mia mbili iliyopita.
Ndio, nadhani Tanzania ingefaidika zaidi kama ingeweka mikakati ya kuchimba na kuendeleza utumiaji wa chuma chake katika kutengeneza bidhaa mbalimbali zitokanazo na mali ghafi hiyo hasa katika wakati huu. Tungeunganisha madini yetu mbalimbali kama 'nickel' na 'graphite', madini ambayo sasa yanachimbwa na kusafirishwa nje na kutengeneza aina mbalimbali za vyuma vyenye thamani kubwa na kutengeneza bidhaa mbalimbali kama mafriji, majiko na vitu vingine chungu nzima.
Pamoja na yote hayo, tukumbuke pia tunapojadili bidhaa ya chuma kama anayoiongelea mleta mada, tujiulize bei ya chuma duniani sasa hivi ikoje.? Ni nani watengenezaji wakubwa wa bidhaa hii na wameshikilia soko kwa kiasi gani. Tutaweza kushindana ndani ya soko hilo analotamba nalo mChina?
Watawala wetu wengi wa sasa Afrika wanapenda kuchimba dhahabu almasi na vito. Haya yanaweza yanaibika kwa urahisi kuliko chumaUnazungumzia stage gani ya uzalishaji na chuma cha aina gani.
Nchi gani ya africa unayoijua wewe yenye kiwanda cha chuma ambacho ni classified as heavy iron industry?
Not really the case uchimbaji wa madini ardhini in large scale unahitaji almost similar investment kwenye vitendea kazi only difference some minerals are more precious than others.Watawala wetu wengi wa sasa Afrika wanapenda kuchimba dhahabu almasi na vito. Haya yanaweza yanaibika kwa urahisi kuliko chuma
Chuma n'a makaa ya mawe ni vitu muhimu sana.. Tatizo wewe ni kilazaHahahaaaa acha kuota mkuu, we are after money, hatuchimbichimbi, you can not extract minerals before doing an economical analysis. Is it economical?
Mzee unatoa dozi sana.....Kama tunataka maendeleo ya kweli ambayo yatawaudhi wazungu hatuna budi kutumia our uncommon sense, maana common sense ya hatuwezi, hatuna mtaji, hatuna technolojia ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo. Lazima tuseme tunaweza na tuanze sasa. Viongozi wetu ni rahisi sana kuelekea kwenye dhahabu na almasi kwakuwa ni rahisi kupewa tofali la madini hayo kama zawadi binafsi. Kwenye chuma mambo hayo hakuna hivyo hayawavutii viongozi kuelekea huko. Lakini ni heri pesa yote ya dhahabu, almasi, germstones na nickel tukaitumia kwenye kwenye kusomesha watoto wetu kokote duniani kuhusu chuma na matumizi ya chuma, technolojia ya kutengeneza bidhaa za chuma na uchimbaji wa chuma. Baba wa taifa alishaianza hiyo kazi pale UFI ubungo, Mang'ula na arusha, SIDO nk lakini hatukumuelewa hata kidogo. Leo hii hata jembe la chapa jogoo linaagizwa kutoka china.
Maslahi ya wakubwa wanajua wao lakini ukweli ni kwamba Chuma ndo madini inayopatikana kwa wingi duniani kuliko madini yoyote nyingine na matumizi yake ni mengi sana lakini namna ya kuipata mpaka itumike inahitaji uwekezaji mkubwa sana maana inahitajika viwanda vingi vikubwa. Licha ya uwekezaji mkubwa wa mgodi wenyewe, kiwanda cha kwanza kikubwa ni cha kutoa Chuma toka kwenye udongo (smelter) kupata mali ghafi (ingot) ambayo inauzika lakini haitumiki kwa lolote mpaka ifanyiwe kazi na viwanda vingine. Kutokana na ingot bidhaa aina nyingi za Chuma za matumizi mbalimbali zilizofanyiwa kazi na viwanda mbalimbali zinapatikana tayari kuuzwa kwa viwanda vingine kama vya kutengeneza magari, mashine, mitambo, madege, reli nk. Chuma kukifanyia kazi kunahitaji moto mkali!Yaani kama tungechimba chuma then mradi wa SGR ukafuata inamaana reli ingetengenezwa na chuma chetu na gharama ingekuwa ndogo sana. Sema kuna maslahi ya watu
Gari inatengenezwa kwa chuma kwa asilimia kubwa inawezeka hata 80%+.Mkuu mbona unakoroga mambo sasa, mbona kama unachanganya idhaa? Magari yanatengenezwa na chuma? Makontena ni chuma kile?
Unaelewa tofauti kati ya bati, chuma na aluminium?
Wewe ndio kilaza unayetaka hayo madini yasiyo na thamani duniani. Unabeba mikontena ya vyuma na makaa ya mawe alafu pesa unayolipwa ni ya kilo 3 za dhahabu au Tanzanite sii ujinga huo. Storage yenyewe ni shida. Wakati dhahabu ya mabilioni unaficha kwenye kabegi ka lucky Dube alafu unasepa zako dadeki.Chuma n'a makaa ya mawe ni vitu muhimu sana.. Tatizo wewe ni kilaza
Sent from my JSN-L21 using JamiiForums mobile app