Mapinduzi ya Zanzibar: Ukweli ni Upi?

Maswali kuhusu Mapinduzi Matukukufu ya Zanzibar, bado ni mengi kuliko majibu!.

Nawatakia Maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

Pasco
 
Hili bandiko lina miaka 8 humu, na maswali haya bado yapo na bado hayana majibu ya kutosheleza.

Hata hivyo natuma salamu za pongezi ya miaka 54 ya Mapinduzi, matukufu ya Zanzibar kwa Wanzibari wote, Wazanzibara na Wapemba, japo hawakushiriki Mapinduzi.

Mapinduzi Daima.

P
 
Ukimsoma vizuri mwandishi nguli wa makala kwenye gazeti la raia mwema ndg Joseph Mihangwa utaujua ukweli kuhusu mapinduzi.
 
Ukimsoma vizuri mwandishi nguli wa makala kwenye gazeti la raia mwema ndg Joseph Mihangwa utaujua ukweli kuhusu mapinduzi.
Nakumbuka kumsoma gezatini, kama mada uliletwa humu naomba link.

P.
 
Dr. Ghassany.
Katika kitabu chake yeye alifanya kazi ya kuchukuwa maelezo ya wahusika na kuyaweka kama kumbukumbu. Sijaona pahali anatowa maelezo yake binafsi katika mirengo yeyote lbda watu wamemuelewa tofauti. Yeye mwenyewe amesisitiza kufanywe utafiti wa kina ili watanzania wawe na uwelewa mpana kuhusu mapinduzi.

Sema kwasababu huyu Dr. Ghassany kajitambulisha kuwa ni mzanzibari na rangi yake ile ya kipemba pemba hivi ndio hizi chuki za kibongo unazozionesha hapa.
 
Nasikitika sana kwa kuharibika kompyuta yangu hii video unayoizungumzia hapa nilikuwa nayo. Inasikitisha sana watu wengi walipoteza maisha kwenye fukwe za bahari.
 
Kikundi cha John Okello, Kundi la Wakommunist chini ya Babu na Vijana wa ASP walioasi msimamo wa ASP kutaka kuingia madarakani ndio waliofanya MAPINDUZI ila kikundi cha kwanza kuanza kufyatua risasi ndipo penye utata hapo
 
Nyerere ndie aliefanya mapinduzi Zanzibar. Na ndio ukaanza utawala wa Tanganyika ndani Zanzibar Mpaka hii leo.
 
Nawatakia kumbukumbu njema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyovikomboa visiwa hivi.
P
 
Today’s official slogan in Zanzibar is “Mapinduzi daima!” (Revolution forever!). Revolution, Yes! But Zanzibar, Tanzania and the rest of Africa needs a Mapinduzi ya Mawazo (Mental Revolution), to learn from the past, to appreciate the present and to plan and work for a better future!
 
Hahaha kaka ili usiitwe tena kuhojiwa na Bunge, kubali yote unayoyasikia. Chama cha mapinduzi nao wanasemaga ndio walileta ukombozi. Ukiwasikiliza ccm wanakueleza eti Karume aliongoza mapinduzi takatifu. Waliisha sema na kutunga sheria kwamba wao tu ndio husema ukweli, wengine wote hamruhusiwi kuhoji wala kupinga wasemalo wao.
Nakumbuka marehemu Mtikila katika harakati zake kudai usajili wa DP aliwahi kuambiwa kwamba alisema uongo kwasababu aliyoyasema hayakuwa kwenye kiapo. Mtikila akamuuliza Marehemu jaji Lihundi yani uongo nikiusema chini ya kiapo unabadirika kua ukweli?! Na akiwa hapo hapo mahakamani akaomba aende kwenye kizimba aape, na aliomba muda wote aongee akiwa kizimbani ili Lihundi amuamini, hahaha jamaa alikuwa matata. Anyway wao tu ndio wakweli kaka.
 
Natepe alishafariki mwaka Jana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu, habari Kuna sehemu nimepitia nikaona kuwa John okelo ndiye rais wa kwanza wa zanzibar, wakati tunajua kuwa ni Karume, mwenye kujua hili atusaidie,wakuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…