Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga

Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga

ahahahhahah sijui ilinipitaje hiii!
pitiku bana haina makuu!
ni majani ya maboga
chumvi
maji
na kapilipili
unakata majani ya maboga vidogo dogo,unaweka maji,na pilipili unabadnika jikoni!
maji yakichemka unaweka mboga
inaiva kama dk 8-10 hiv
halafu weka chumvi!
ehehehheheheh Kaunga come zis way!
Mentor hebu do ze nidful kwa huyo kamwali af unoe mambo!
A LOT IN STORE FOR YU!
lol!

Sisi tuna kitu ya msapagulo
Msusa mchanga (majani ya maboga) ukishauchambua na kuuosha (kama una mchanga, ila kuuosha unaufanya uwe mgumu), unakata mapande makubwa makubwa preferably na mikono sio kisu.
Unabandika maji kiasi jikoni, yakichemka unaweka chumvi na magadi kidogo (au baking powder) ili msusa usiwe mgumu; baadaye waweka msusa wako unafunika kidogo, ukigeuza katia nyanya moja tu, na pilipili (kwa ladha) funika kidogo then weka kinyori cha karanga (karanga iliyosagwa) kidogo sana sana, epua baada ya muda mchache hakikisha rangi ya kijani haipotei.

Waweza usiweke karanga, na bado ikawa nzuri, au ukaweka tone chache za mafuta; ila pilipili ni nzuri kwa walaji na inapendeza ikiliwa ikiwa ingali ya moto.
 
Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga:
Mahitaji:
1. bamia gram 250
2. Majani ya maboga 200
3. Nyanya chungu (kama utapenda) gram 100
4. Magadi 1/4 kijiko cha chai
5. chumvi - to taste
6. nyanya ndogo 1
7. Karanga zilizosagwa gram 100
8. maji - kikombe 1

Matayarisho:
1. Osha na kata bamia na nyanya chungu vipande vidogovidogo
2. Osha na kata majani ya maboga ndogondogo

Jinsi ya kupika
1. Bandika maji mpaka yachemke
2. weka chumvi na magadi
3. Weka majani ya maboga, bamia, na nyanya chungu
4. vikishachemka kwa kama dakika 5, weka nyanya, acha ichemke kidogo.
5. weka unga wa karanga na acha uchemke kwa kama dakika 5 - 7.
Tayari kwa kuliwa.
Mboga hii inapendeza kuliwa na ugali

Yaani umenikumbusha mbali sana. Sisi tulizozaliwa bara tuna raha sana.
 
Yaani umenikumbusha mbali sana. Sisi tulizozaliwa bara tuna raha sana.

Wewe msukuma ndy washakukamata, maana usukumani upo mrenda mpaka wa majani makavu, mrenda pori, mrenda wa majani ya tango! Bara raha sana!
 
Sisi tuna kitu ya msapagulo
Msusa mchanga (majani ya maboga) ukishauchambua na kuuosha (kama una mchanga, ila kuuosha unaufanya uwe mgumu), unakata mapande makubwa makubwa preferably na mikono sio kisu.
Unabandika maji kiasi jikoni, yakichemka unaweka chumvi na magadi kidogo (au baking powder) ili msusa usiwe mgumu; baadaye waweka msusa wako unafunika kidogo, ukigeuza katia nyanya moja tu, na pilipili (kwa ladha) funika kidogo then weka kinyori cha karanga (karanga iliyosagwa) kidogo sana sana, epua baada ya muda mchache hakikisha rangi ya kijani haipotei.

Waweza usiweke karanga, na bado ikawa nzuri, au ukaweka tone chache za mafuta; ila pilipili ni nzuri kwa walaji na inapendeza ikiliwa ikiwa ingali ya moto.

Hahaha, nimekukubali, kitu chukuchuku! Lakini nyanya usiweke, weka mauwa kadhaa ya maboga, na mafuta yasiwe mafuta ya dukani, ni samli mbichi! teh teh, wapi maziwa ya mgando!
 
Ngoni...apa job kwangu kuna wangoni wawili...
Mmoja ver shy akiwa na watu asiowajua ila muongeaji akiwa na kampani aliyoizoea. Ni mzushi mno na promiseless balaa. Never likes to hang out...baba na mama wote ni wangoni.

Huyu wa pili ndo kama nyie...she loves cooking. Yupo friendly tu kwa wote. Alikuja kwangu cku moja akatupikia ugali ila aling'ang'ania ninunue kuku...now i know y. Heheheheh


Hahah, huyo mngoni wa kwanza umempatia kabisaa, waliokulia na kuishi ungonini waongo na wazushi kwelikweli, na wanapenda waume za watu hao...pia hawana wivu, jirani zangu ungonini alioa mke, wakati wa ujauzito akaja mdogo mtu kusaidia kazi, jamaa akasimamia show na kumpenda zaidi mdogo mtu, mke wake alivogundua akaamua kurudi kwao na kumwacha mdogo wake pale aolewe...saafi, na huwa anaffika pale kusabahi na kukumbushia gemu!...ahahahaa, Mngoni mpe pesa atafikisha lakin umpe mke/mume lazima achakachue!
 
Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga:
Mahitaji:
1. bamia gram 250
2. Majani ya maboga 200
3. Nyanya chungu (kama utapenda) gram 100
4. Magadi 1/4 kijiko cha chai
5. chumvi - to taste
6. nyanya ndogo 1
7. Karanga zilizosagwa gram 100
8. maji - kikombe 1

Matayarisho:
1. Osha na kata bamia na nyanya chungu vipande vidogovidogo
2. Osha na kata majani ya maboga ndogondogo

Jinsi ya kupika
1. Bandika maji mpaka yachemke
2. weka chumvi na magadi
3. Weka majani ya maboga, bamia, na nyanya chungu
4. vikishachemka kwa kama dakika 5, weka nyanya, acha ichemke kidogo.
5. weka unga wa karanga na acha uchemke kwa kama dakika 5 - 7.
Tayari kwa kuliwa.
Mboga hii inapendeza kuliwa na ugali

Shukrani.
Ila kuweka magadi siyo unaua virutubishi vinavyopatikana kwenye chakula?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Mrenda wa bombambili hautiwi karanga, itu chukuchuku; utakuwa umeiba sehem hii recipe! teh teh
labda kwenu bombambili hakuna karanga...
njoo mkongotema utaona kama utapeleka mlenda kwa meza usio na karanga
 
Sisi tuna kitu ya msapagulo
Msusa mchanga (majani ya maboga) ukishauchambua na kuuosha (kama una mchanga, ila kuuosha unaufanya uwe mgumu), unakata mapande makubwa makubwa preferably na mikono sio kisu.
Unabandika maji kiasi jikoni, yakichemka unaweka chumvi na magadi kidogo (au baking powder) ili msusa usiwe mgumu; baadaye waweka msusa wako unafunika kidogo, ukigeuza katia nyanya moja tu, na pilipili (kwa ladha) funika kidogo then weka kinyori cha karanga (karanga iliyosagwa) kidogo sana sana, epua baada ya muda mchache hakikisha rangi ya kijani haipotei.

Waweza usiweke karanga, na bado ikawa nzuri, au ukaweka tone chache za mafuta; ila pilipili ni nzuri kwa walaji na inapendeza ikiliwa ikiwa ingali ya moto.
yaani hapa rafiki ndo umetupikia pitiku haswaaaaa....
na uzuri wa hii inapikwa baada ya kusongwa ugali, yaani ikiiva tu kitu kwa meza......
 
yaani hapa rafiki ndo umetupikia pitiku haswaaaaa....
na uzuri wa hii inapikwa baada ya kusongwa ugali, yaani ikiiva tu kitu kwa meza......

waoh, kumbe majina tu ndio tofauti lakini mboga ni ile ile, yaani naimagine kukiwa na manyunyu ya mvua kama sasa hivi upate ugali wa moto na hiyo pitiku ya moto iliyoongezwa nyanya chungu 3 na pilipili ya kutosha; nasahau diet kwa kweli. LOL
 
waoh, kumbe majina tu ndio tofauti lakini mboga ni ile ile, yaani naimagine kukiwa na manyunyu ya mvua kama sasa hivi upate ugali wa moto na hiyo pitiku ya moto iliyoongezwa nyanya chungu 3 na pilipili ya kutosha; nasahau diet kwa kweli. LOL
ha haaa, rafiki ugali na pitiku na nyama ya kuchoma ni diet tosha.....
umenikumbusha mbali sana. hapo napika kwa jiko la kuni na pembeni nachoma mahindi......
Pasaka itabidi niende kwa mama. maana hayo yoote huwa yanakuwepo. na maboga, lol!
 
Mimi chochote kinachoteleza mdomoni sisogeleiiiii
 
Da! Narudi Kwetu Kimbiji MBESA WIlaya Ya Tunduru Mkowa Wa Ruv Uma. Hivi Vote Vipo Takribani Wilaya Ya Tunduru Na Pand3 Za Songeha Kwa Sana Tu. Kwetu Kule Tunamix Na Majani Ya Magimbi,majani Ya Bamia, Nyanya, Chumvi, Magadi, Du! Tamuje! Narudi Kwetu Kimbiji. Chezea Tanganyika Wewe!
 
Mapishi ya Mlenda wa majani ya maboga:
Mahitaji:
1. bamia gram 250
2. Majani ya maboga 200
3. Nyanya chungu (kama utapenda) gram 100
4. Magadi 1/4 kijiko cha chai
5. chumvi - to taste
6. nyanya ndogo 1
7. Karanga zilizosagwa gram 100
8. maji - kikombe 1

Matayarisho:
1. Osha na kata bamia na nyanya chungu vipande vidogovidogo
2. Osha na kata majani ya maboga ndogondogo

Jinsi ya kupika
1. Bandika maji mpaka yachemke
2. weka chumvi na magadi
3. Weka majani ya maboga, bamia, na nyanya chungu
4. vikishachemka kwa kama dakika 5, weka nyanya, acha ichemke kidogo.
5. weka unga wa karanga na acha uchemke kwa kama dakika 5 - 7.
Tayari kwa kuliwa.
Mboga hii inapendeza kuliwa na ugali
tamuje umitisha a useful uzi..
 
Back
Top Bottom