Mapokezi ya Mbowe Jimboni Hai yadoda, CHADEMA yaahidi kugawa nyama Kama motisha Kwa wahudhuriaji

zanku

Member
Joined
Jun 9, 2020
Posts
70
Reaction score
152
MAPOKEZI YA MBOWE HAI YA DODA, WANANCHI WASUSIA, CHADEMA YATANGAZA KUGAWA NYAMA KWA KILA MHUDHURIAJI

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mapokezi ya ujio wa aliewahi kuwa Mbunge wa Hai ndugu Mbowe yameingia dosari baada ya wananchi wengi kuonesha kutokuwa na munkari nae tena kama zamani, hii inachagizwa na uchapakazi wa Mbunge Mpya Saashisha Mafuwe ambae amekuwa akijikita katika kupigania maslahi ya maendeleo ya wananchi wa Hai na kuweka pembeni masuala ya uhasama wa kisiasa.

Mapokezi ya Mbowe yameingia upweke baada ya kuzuka taarifa za uwepo wa fujo za vijana wa bavicha waliokodiwa kutoka mara, Arusha na Moshi, taarifa zilizotapakaa katika viunga vya mji wa bomang'ombe ni ujio wa vikosi vya fujo na matusi kutoka mikoani ili kujaza mapokezi hayo ili kuudanganya umma wa watanzania kuwa Mbowe Bado anapendwa.

Wananchi wengi wamechukizwa na tabia ya Chadema kuhatarisha amani Kisha kujivika ngozi ya kondoo kuwa wanaonewa.

Katika hatua nyingine viongozi wa chama hicho wakiongozwa na Simon Mnyampanda wamekuwa wakipita katika makazi ya watu na kuwaahidi kuwa Kila atakaehudhuria mkutano huo atapatiwa nyama robo kilo, jambo ambalo limepingwa vikali na wananchi wa Hai wakisema wao wanataka hai yenye utulivu na maendeleo hasa kipindi hiki ambacho miradi mingi imefanyika Chini ya Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge Saashisha Mafuwe.

Rai Yangu Kwa Chadema ni kuwa hii ni ishara ya kuishiwa hoja za ushawishi na kutumia nyama, watu wa Hai wameelimika hawawezi kudanganyika Kwa nyama Wala kisusio.
Your browser is not able to display this video.
 
Watu wa propaganda mshaanza,havi mnapewa sh ngapi?
 

Mbona umewahi mapema.

Shughuli ni jumapili Tulia basi.

Halafu ni lini chadema imehatarisha amani ya nchi.

Wanaohatarisha amani ya nchi Ni polisi ambao wanaua wafanyabiashara na kuiba pesa zao.

Refer mfanyabiashara wa madini.
 
Hangaika na chama chako kinachotaka kubinafsisha bandari...achana na CDM utakonda.
 
kwa hiyo mkuu unataka kusema kwamba wananchi wa Bomang’ombe wananunulika kwa vipande vya nyama na si vipande vya fedha tena!!?

Hatari na nusu
 
Mbona umeanza kujihami mapema wakati shughuli yenyewe bado haijafanyika?

Subiri mapokezi yadode ndio uje hapa ukiwa na ushahidi, vinginevyo hili andiko lako litakuwa ni porojo tu.
 
Mu
Muda utaongea kesho
 
18 March 2022

Machame, Kilimanjaro

MAANDALIZI YA KUMPOKEA MHE FREEMAN MBOWE MACHAME, NGOMBE 6 KWA AJILI YA SHUGHULI WATOLEWA


Maandalizi mazito hapa Machame Kilimanjaro huku wazee wametoa ngombe kwa ajili ya shughuli ya kumkaribisha mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Aikaeli Mbowe ambaye ametoka mahabusu hivi karibuni baada ya kesi namba 16 ya mwaka 2021 iliyokuwa inamkabili yeye na walinzi wake watatu kufutwa na DPP kwa kuwasilisha hati ya Nolle prosequi kuwa Jamhuri haina nia ya kuendelea na kesi hiyo iliyokuwa ikisikilizwa ktk Mahakama Kuu Maalum Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, kesi hiyo ilikuwa ya tuhuma za Ugaidi.
 
Hela za ccm zinaliwa kijinga sana !

utakuta huyu mfuasi wa Sabaya naye eti analipwa !
 
 

Attachments

  • Kweli Kaka anarudi nyumbani_@freemanmbowetz https___t.co_tdqkcD44ah.mp4
    3.6 MB
Ni mara nyingi mtu asiyebadirika hana maendeleo propaganda za kipuuzi zimepitwa na wakati unachochea ili upate nini, wakati ule haupo na hautarudi tena watu sio wajinga tena, japo ni ngumu tunahitaji kustaarabika siasa za kishenzi hazina nafasi kwa sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…