Maprofesa bakini vyuoni kulinda heshima zenu dhidi ya wanasiasa

Maprofesa bakini vyuoni kulinda heshima zenu dhidi ya wanasiasa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Jamii inawaheshimu sana wasomi hasa maprofesa, jamii inadhani kuwa professor sio mtu wa mchezomchezo, anafahamu na kujua na kuweza kila kitu na kila jambo. Inapotokea tukio la professor kubezwa, kuzomewa na kutukanwa au kushindwa kufanikisha jambo inawashangaza sana.

Sio jambo la nadra jamii kusikia wizara inayoongozwa na prof fulani imeshindwa kutatua kero za wananchi na wizara ambayo inaongozwa na asiyekuwa prof inaupiga mwingi katika kutatua kero za watanzania. Lakini pia sio jambo la nadra kuona prof anadhalilishwa na ngazi ya uteuzi kama mtu mwingine tu.

Swali kwenu ni kunatokea nini kuyakimbia madarasa yenu mliyoyazoea na kuyamudu na kukimbilia siasa msizo na ujuzi nazo?

Rudini bhana, tulijenge taifa
 
Katika wooote yule wa jalalani alijua kujidhalilisha ndio mana bwana yule alikiwa anamfokea sana kwenye simu
 
Katika wooote yule wa jalalani alijua kujidhalilisha ndio mana bwana yule alikiwa anamfokea sana kwenye simu
profesa akiambiwa kaongea nonsense anawakilisha maprofesa wenzake. Bakini madarasani jamani, huko shuleni profesa ni mtu muhimu sana, maneno yake ni dhahabu kwa wanafunzi wake na jamii nzima ya chuo.
 
profesa akiambiwa kaongea nonsense anawakilisha maprofesa wenzake. Bakini madarasani jamani, huko shuleni profesa ni mtu muhimu sana, maneno yake ni dhahabu kwa wanafunzi wake na jamii nzima ya chuo
Ila bimkubwa pale kazingua.

Naunga mkono hoja academicians wabaki vyuoni waongezewe stahili zao wafundishe
 
Ili waishi wanaona bora siasa ambazo nazo zimewakalia kushoto
Kama vyuoni kuna tatizo kaeni chini wadau muone mnafanya nini kulitatua ili mbaki vyuoni. Taaluma yetu inashuka kwakuwa kuna idadi kubwa sana ya walimu wenye sifa wake nje ya vyuo.

Maprofesa wa nchi nyingine hawaoni aibu wala kuogopa kudai ujira wao wenye nafuu, sisi hapa kwetu Professor anakufa na tai yake shingoni.
 
Fedheha...
Mpaka saiz bado sijajua mantiki ya ELIMU bongo. Maana wasomi wengi waliofanikiwa katika elimu ndio hao wanashindwa kutatua changamoto katika jamii Bali kugeukia vitu ambavyo havina tija katika jamiii..

Kila msomi mwenye nafasi kitu anachowaza ni upigaji wa pesa za umma na kutumia madaraka aliyonayo kuumiza wengine, kitu ambacho siyo sawa kabisaaa
 
Huko vyuoni mshahara ni mdogo, hakuna posho na marupurupu mengine, maprofesa nendeni tu kwenye siasa mle keki ya taifa😆
 
Huko vyuoni mshahara ni mdogo, hakuna posho na marupurupu mengine, maprofesa nendeni tu kwenye siasa mle keki ya taifa😆
Mshahara unatafutwa na kudaiwa. Professor ni mtu mkubwa sana na uwezo mkubwa wa kujenga hoja ikasikilizwa na watawala hata wafadhili, lakini Maprofessor wetu ni nadra kuwasikia wamegoma au wanadai maslahi yao na ya wengine. Ni vigumu kuwakuta kwenye vyama vya wafanyakazi wala siasa kwa uwazi. Badala yake wanatumia ujanjaujanja wa kutafuta hela haramu kupitia miradi na tafiti zisizo na tija kwa taifa, ziko makabatini. Miradi mingi imefilisiwa na maprofesa.

Hii ni tofauti na maprofessor wa nchi nyingine ambao wanatoa matamko na kulazimisha kukaa meza moja na watawala kudai maslahi yao. Mshahara wa prof wa Kenya ni mkubwa mara 7 ya mshahara wa prof wa tanzania. Wasomi wetu wanasononeka lakini wanashindwa kujitokeza kusema.
 
Back
Top Bottom