Mapungufu ya stars Leo dhidi ya Uganda

Mapungufu ya stars Leo dhidi ya Uganda

mugah di matheo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2018
Posts
6,307
Reaction score
12,410
Habari wadau naombeni mniambie kama Leo tulivyoangalia mechi ya timu yetu dhidi ya Uganda mapungufu yalikuwa wapo? na je kunapengo la mchezaji wa simba lilionekana miongoni mwq wale walioenguliwa kwenye kikosi wakitokea simba na moja wa yanga ? naombeni maoni yenu
 
Uwanja mbovu sana ule, mpira pass haziendi.
Mapungufu niliyo yaona ni hawakuwa na accuracy ya pass lkn nadhani sababu ni uwanja
 
Kipindi cha kwanza hawajacheza vyema ila kipindi cha pili wamebadilika na kuanza kutafuta bao.

Ila Samatta samahani sana, Sijaona akicheza kama nahodha amezidiwa na Msuva.
Kuna goli la wazi alikosa! Daa ila ndo soka ilivyo! Nashauri Thomas Ulimwengu aanzie benchi! Mabeki wa kati pamoja na Mudadhiri [emoji106] [emoji106] [emoji106] [emoji106]
 
Kapombe pengo lake mimi nili liona na Ulimwengu angetolewa second half mapema aingie Chilunda
 
Kuna goli la wazi alikosa! Daa ila ndo soka ilivyo! Nashauri Thomas Ulimwengu aanzie benchi! Mabeki wa kati pamoja na Mudadhiri [emoji106] [emoji106] [emoji106] [emoji106]
Ulimwengu nae ni Kiazi tu hana kitu bora nafasi yake ingebaki hata wazi hakuna alichoongeza wala kupunguza.
 
Yah huyu Kocha nae hakuona kuwa Ulimwengu ni mzigo afanye mabadiliko ya mapema.
Nahisi bocco angekuwepo ange anza na samatta. Ile mechi ya Lesotho tulizengua leo tume jitahidi sana. Timu za Afcon 2019 zitakua 24, kwa kundi hili tusipo ingia tuta kua wachovu sana.
 
Ulimwengu nae ni Kiazi tu hana kitu bora nafasi yake ingebaki hata wazi hakuna alichoongeza wala kupunguza.
Kweli mkuu! Kocha angemwamini yule dogo Chilunda! Ulimwengu awe anaanzia benchi! But timu imecheza vema hasa kipindi cha pili
 
Washabiki Wa NdalaFC Wamejitengezea Uzi Wanajifariji tu Lakini Nawaapia Kwa Ninavyowajua Wabongo Nyinyi Ndiyo Mutakaokuja Kusema AmunikeOut.
 
Back
Top Bottom