Marais wanacheka na kuteta kirafiki sisi mtandaoni tunaandikiana laana na kila aina ya matusi

Marais wanacheka na kuteta kirafiki sisi mtandaoni tunaandikiana laana na kila aina ya matusi

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Kanisani mara nyingi Padre anayeongoza ibada huweka msisitizo wa kuiombea dunia nzima. Hukataza ile aina ya maombi yenye kunihusu mimi na watu wa familia yangu pekee. Huwa anasema tupunguze zile 'yangu' kila tunapoongea na Mungu. Kazi yangu, mume wangu, mke wangu, watoto wangu, nyumba yangu, jirani yangu. Padre kwa lugha ya kinabii kabisa amekuwa akikataza sala binafsi zenye ubinafsi mwingi ndani yake.

Anasisitiza kuombea walio wengi na hayo maombi yangu yawe ni sehemu tu ya nia pana. Namuelewa Padre kadri anavyorudia mahubiri yake pale katika mimbari ya kanisa, ni ujumbe wa upendo unaojali walio wengi. Lakini katika kuzama kwenye tafakuri naona kabisa kuwa maneno yake yanazisuta nafsi za mamilioni ya wanaolitumia hili jukwaa kwa nia mbalimbali haswa zile za kupanua uwezo wa mawazo yetu.

Naamini nia inayomsukuma Mgombea Urais mpaka akachukua fomu na kuilipia shilingi milioni moja kisha akazunguka nchi nzima kutafuta wadhamini, ni kuleta mchango wake katika mabadiliko chanya ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Naamini hiyo ndio nia ya kwanza kabisa ya Mgombea Urais, ikiwa anakabidhiwa ilani na kulazimika kuitekeleza kurasa baada ya kurasa hilo huwa ni suala la pili lakini la mwanzo kabisa ni kutumia kila alichonacho kwa faida ya wengine.

Nchi yetu imeshaongozwa na Marais sita mpaka dakika hii na wote hawa lengo lao kuu ni moja tu, na kizuri kwao ni kwamba wote wanatoka CCM wanatekeleza sera zile zile. Tofauti inaweza kuwa kwenye maarifa na utendaji kazi binafsi lakini wote wanayo nia moja kutoka ndani kabisa ya mioyo yao, kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya mtanzania mmoja mmoja kadri inavyowezekana.

Inashangaza kusoma humu namna baadhi yetu tunavyotamani kutoana macho kwa ushabiki tu wa hawa marais, wote hawa ni watekelezaji wa ilani ya CCM, ndio wanayokabidhiwa kama rejea yao baada tu ya mchakato wa kuapishwa na Jaji Mkuu.

Anachoweza kufanya Rais wa Awamu ya Kwanza hukifanya na yule wa Awamu ya Pili huendeleza pale anapoishia. Anachoweza kuendeleza wa Awamu ya Pili hukiendeleza mpaka pale atakapoishia na muendelezo wake anamuachia wa Awamu ya Tatu. Uhalisia umekwenda hivyo mpaka imefika awamu ya sita. Hivi ndio Tanzania inavyojengwa na chama kimoja cha CCM.

Hii mikwaruzano ni siasa za upambe ule ule unaodumu miongoni mwetu ambazo kwa kweli zinatuchukulia muda na akili bila ya sababu ya msingi. Marais wote sita ni watekelezaji wa ilani ya CCM, wanaachiana vijiti na kuendeleza anapoishia mtangulizi. Hajawahi kuingia miongoni mwao akatoka CHADEMA na kuingiza sera tofauti na zile zilizotimizwa na Mwasisi wa Taifa Julius Nyerere.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
 
A very rosy picture. Mkuu jitahidi kuwa realistic basi. Wengi hapa tunaishi Tanzania, tuna taarifa ya yanayoendelea nchini na ni "great thinkers" at least by assumption. Kwamba wote ni marais wa CCM, sawa kabisa. Kwamba wote wanatekeleza "ilani ya CCM", sawa kabisa. Kwamba ni "kitu kizuri", si sawa hata kidogo - kwa mfumo tulio nao na kwa uhuni unaofanyika kwenye chaguzi zetu (an open secret).

Halafu hiyo ILANI YA CCM lazima iwe kitu cha kushangaza sana. Kila Rais (wa CCM) anapoingia madarakani anatuambia ana vipaumbele vyake na mambo mengine anayakataa kabisa. Anaendelea kutuhabarisha jinsi nchi ilivyoharibiwa sana miaka ya nyuma na jinsi yeye atakavyoirekebisha na kuiimarisha bila kutufahamisha nani aliyeiharibu na hatua atakazomchukulia! Huu ni msiba wa kitaifa, si kitu kizuri hata kidogo.

Ndio maana ukiwa realistic huwezi kushangaa kwa nini kuna vita kubwa huko CCM baina ya wapambe, machawa na makada wa watu na vikundi mbalimbali. Hiyo inayoitwa ilani ya ccm hakika ni kiini macho (illusion) tu. INASHANGAZA SANA. Rais anaweza kupuuza mihimili mingine yote ikiwa ni pamoja na Bunge na mahakama akapanga miradi yake mwenyewe na kutumia pesa za umma anavyotaka yeye bila kushauriwa na kuelekezwa na mhimili au taasisi yoyote ya kitaifa inayohusika na mipango ya maendeleo. Anaweza hata kuachana na miradi iliyopangwa na kuanza kutekelezwa na awamu zilizotangulia! Unaposifia kuwa "anafanya kwa manufaa ya taifa" inashangaza sana.
 
Kanisani mara nyingi Padre anayeongoza ibada huweka msisitizo wa kuiombea dunia nzima. Hukataza ile aina ya maombi yenye kunihusu mimi na watu wa familia yangu pekee. Huwa anasema tupunguze zile 'yangu' kila tunapoongea na Mungu. Kazi yangu, mume wangu, mke wangu, watoto wangu, nyumba yangu, jirani yangu. Padre kwa lugha ya kinabii kabisa amekuwa akikataza sala binafsi zenye ubinafsi mwingi ndani yake.

Anasisitiza kuombea walio wengi na hayo maombi yangu yawe ni sehemu tu ya nia pana. Namuelewa Padre kadri anavyorudia mahubiri yake pale katika mimbari ya kanisa, ni ujumbe wa upendo unaojali walio wengi. Lakini katika kuzama kwenye tafakuri naona kabisa kuwa maneno yake yanazisuta nafsi za mamilioni ya wanaolitumia hili jukwaa kwa nia mbalimbali haswa zile za kupanua uwezo wa mawazo yetu.

Naamini nia inayomsukuma mgombea urais mpaka akachukua fomu na kuilipia shilingi milioni moja kisha akazunguka nchi nzima kutafuta wadhamini, ni kuleta mchango wake katika mabadiliko chanya ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Naamini hiyo ndio nia ya kwanza kabisa ya mgombea urais, ikiwa anakabidhiwa ilani na kulazimika kuitekeleza kurasa baada ya kurasa hilo huwa ni suala la pili lakini la mwanzo kabisa ni kutumia kila alichonacho kwa faida ya wengine.

Nchi yetu imeshaongozwa na marais sita mpaka dakika hii. Na wote hawa lengo lao kuu ni moja tu, na kizuri kwao ni kwamba wote wanatoka CCM wanatekeleza sera zile zile. Tofauti inaweza kuwa kwenye maarifa na utendaji kazi binafsi lakini wote wanayo nia moja kutoka ndani kabisa ya mioyo yao, kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya mtanzania mmoja mmoja kadri inavyowezekana.

Inashangaza kusoma humu namna baadhi yetu tunavyotamani kutoana macho kwa ushabiki tu wa hawa marais, wote hawa ni watekelezaji wa ilani ya CCM, ndio wanayokabidhiwa kama rejea yao baada tu ya mchakato wa kuapishwa na Jaji Mkuu.

Anachoweza kufanya rais wa awamu ya kwanza hukifanya na yule wa awamu ya pili huendeleza pale anapoishia. Anachoweza kuendeleza wa awamu ya pili hukiendeleza mpaka pale atakapoishia na muendelezo wake anamuachia wa awamu ya tatu. Uhalisia umekwenda hivyo mpaka imefika awamu ya sita. Hivi ndio Tanzania inavyojengwa na Chama kimoja cha CCM.

Hii mikwaruzano ni siasa za upambe ule ule unaodumu miongoni mwetu ambazo kwa kweli zinatuchukulia muda na akili bila ya sababu ya msingi. Marais wote sita ni watekelezaji wa ilani ya CCM, wanaachiana vijiti na kuendeleza anapoishia mtangulizi. Hajawahi kuingia miongoni mwao akatoka CHADEMA na kuingiza sera tofauti na zile zilizotimizwa na Mwasisi wa Taifa Julius Nyerere.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Kama tunataka kufanya mipango mizuri basi tuwe na ilani ya taifa na wala siyo ilani ya chama. Wakiingia chadema na ilani yao, wakiingia ACT wazalendo na ilani yao!
 
A very rosy picture. Mkuu jitahidi kuwa realistic basi. Wengi hapa tunaishi Tanzania, tuna taarifa ya yanayoendelea nchini na ni "great thinkers" at least by assumption. Kwamba wote ni marais wa CCM, sawa kabisa. Kwamba wote wanatekeleza "ilani ya CCM", sawa kabisa. Kwamba ni "kitu kizuri", si sawa hata kidogo - kwa mfumo tulio nao na kwa uhuni unaofanyika kwenye chaguzi zetu (an open secret).

Halafu hiyo ILANI YA CCM lazima iwe kitu cha kushangaza sana. Kila Rais (wa CCM) anapoingia madarakani anatuambia ana vipaumbele vyake na mambo mengine anayakataa kabisa. Anaendelea kutuhabarisha jinsi nchi ilivyoharibiwa sana miaka ya nyuma na jinsi yeye atakavyoirekebisha na kuiimarisha bila kutufahamisha nani aliyeiharibu na hatua atakazomchukulia! Huu ni msiba wa kitaifa, si kitu kizuri hata kidogo.

Ndio maana ukiwa realistic huwezi kushangaa kwa nini kuna vita kubwa huko CCM baina ya wapambe, machawa na makada wa watu na vikundi mbalimbali. Hiyo inayoitwa ilani ya ccm hakika ni kiini macho (illusion) tu. INASHANGAZA SANA. Rais anaweza kupuuza mihimili mingine yote ikiwa ni pamoja na Bunge na mahakama akapanga miradi yake mwenyewe na kutumia pesa za umma anavyotaka yeye bila kushauriwa na kuelekezwa na mhimili au taasisi yoyote ya kitaifa inayohusika na mipango ya maendeleo. Anaweza hata kuachana na miradi iliyopangwa na kuanza kutekelezwa na awamu zilizotangulia! Unaposifia kuwa "anafanya kwa manufaa ya taifa" inashangaza sana.
Unachosema ni kipya kabisa ukweli ni kwamba kimeandikwa katika ilani ya chama inayoelekeza awamu nzima nini kitafanyika. Tatizo ni sisi namna tunavyotsiri kile kilichofanyika kwa maana ya kukosoa jinsi kilivyofanyika.

Ununuzi wa ndege uliandikwa kwenye ilani na JPM akahakikisha anazinunua ndege na zinaanza kazi, hapo hapo kwa kutoelewa vyema kilichomo kwenye ilani tukaanza kuzipinga tukisema eti zoezi zima halikufuata utaratibu wa kupitia kwanza bungeni wakati ukweli ni kwamba michakato yote ya ununuzi wa hizo ndege ina baraka za bunge.
 
Unachosema ni kipya kabisa ukweli ni kwamba kimeandikwa katika ilani ya chama inayoelekeza awamu nzima nini kitafanyika. Tatizo ni sisi namna tunavyotsiri kile kilichofanyika kwa maana ya kukosoa jinsi kilivyofanyika.

Ununuzi wa ndege uliandikwa kwenye ilani na JPM akahakikisha anazinunua ndege na zinaanza kazi, hapo hapo kwa kutoelewa vyema kilichomo kwenye ilani tukaanza kuzipinga tukisema eti zoezi zima halikufuata utaratibu wa kupitia kwanza bungeni wakati ukweli ni kwamba michakato yote ya ununuzi wa hizo ndege ina baraka za bunge.
Ndugu yangu, Waingereza wana msemo maarufu: the devil is in the details. Viongozi wetu wa kisiasa huongea kirahisi rahisi kulaghai wananchi kuwa wanatimiza kazi zao na kufuata sheria na taratibu.

Details zikiwekwa hapa, ndipo kasoro kubwa za msingi zitajitokeza katika yote uliyoandika. Sipendi sana kumjadili JPM kwa vile habari zake kama ninavyozijua kwangu mimi zinaangukia nje ya any intellectual discourse kabisa. Nawaachia mashabiki na wanazi.

Kwako wewe nakusisitizia: kumekuwa na mporomoko wa integrity na consistence katika utendaji wa serikali ya CCM tangu hususan awamu ya tatu kiasi kwamba ni kama nchi imekuwa ikitawaliwa na magenge tofauti tofauti ya kimafia. Hii mada yako inadhihirisha mashaka hayo: CCM moja haipo; ilitoweka zamani kiwiziwizi.
 
Kanisani mara nyingi Padre anayeongoza ibada huweka msisitizo wa kuiombea dunia nzima. Hukataza ile aina ya maombi yenye kunihusu mimi na watu wa familia yangu pekee. Huwa anasema tupunguze zile 'yangu' kila tunapoongea na Mungu. Kazi yangu, mume wangu, mke wangu, watoto wangu, nyumba yangu, jirani yangu. Padre kwa lugha ya kinabii kabisa amekuwa akikataza sala binafsi zenye ubinafsi mwingi ndani yake.

Anasisitiza kuombea walio wengi na hayo maombi yangu yawe ni sehemu tu ya nia pana. Namuelewa Padre kadri anavyorudia mahubiri yake pale katika mimbari ya kanisa, ni ujumbe wa upendo unaojali walio wengi. Lakini katika kuzama kwenye tafakuri naona kabisa kuwa maneno yake yanazisuta nafsi za mamilioni ya wanaolitumia hili jukwaa kwa nia mbalimbali haswa zile za kupanua uwezo wa mawazo yetu.

Naamini nia inayomsukuma Mgombea Urais mpaka akachukua fomu na kuilipia shilingi milioni moja kisha akazunguka nchi nzima kutafuta wadhamini, ni kuleta mchango wake katika mabadiliko chanya ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Naamini hiyo ndio nia ya kwanza kabisa ya Mgombea Urais, ikiwa anakabidhiwa ilani na kulazimika kuitekeleza kurasa baada ya kurasa hilo huwa ni suala la pili lakini la mwanzo kabisa ni kutumia kila alichonacho kwa faida ya wengine.

Nchi yetu imeshaongozwa na Marais sita mpaka dakika hii na wote hawa lengo lao kuu ni moja tu, na kizuri kwao ni kwamba wote wanatoka CCM wanatekeleza sera zile zile. Tofauti inaweza kuwa kwenye maarifa na utendaji kazi binafsi lakini wote wanayo nia moja kutoka ndani kabisa ya mioyo yao, kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya mtanzania mmoja mmoja kadri inavyowezekana.

Inashangaza kusoma humu namna baadhi yetu tunavyotamani kutoana macho kwa ushabiki tu wa hawa marais, wote hawa ni watekelezaji wa ilani ya CCM, ndio wanayokabidhiwa kama rejea yao baada tu ya mchakato wa kuapishwa na Jaji Mkuu.

Anachoweza kufanya Rais wa Awamu ya Kwanza hukifanya na yule wa Awamu ya Pili huendeleza pale anapoishia. Anachoweza kuendeleza wa Awamu ya Pili hukiendeleza mpaka pale atakapoishia na muendelezo wake anamuachia wa Awamu ya Tatu. Uhalisia umekwenda hivyo mpaka imefika awamu ya sita. Hivi ndio Tanzania inavyojengwa na chama kimoja cha CCM.

Hii mikwaruzano ni siasa za upambe ule ule unaodumu miongoni mwetu ambazo kwa kweli zinatuchukulia muda na akili bila ya sababu ya msingi. Marais wote sita ni watekelezaji wa ilani ya CCM, wanaachiana vijiti na kuendeleza anapoishia mtangulizi. Hajawahi kuingia miongoni mwao akatoka CHADEMA na kuingiza sera tofauti na zile zilizotimizwa na Mwasisi wa Taifa Julius Nyerere.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Kacheke nao, mwingine walicmchekea kisha wakamliza na sasa kazi zake wanajibariki wao,acha ufala
 
Phillipo Bukililo ,

..kuna kundi liliukamia Uraisi kupita kiasi.

..kinachoendelea ni frustrations za kundi hilo.

..ni kundi lenye hasira na gubu kwasababu tu mtu wao sio Raisi.

..sasa sijui kama wataanzisha chama, au watabaki ndani ya Ccm.
 
Phillipo Bukililo ,

..kuna kundi liliukamia Uraisi kupita kiasi.

..kinachoendelea ni frustrations za kundi hilo.

..ni kundi lenye hasira na gubu kwasababu tu mtu wao sio Raisi.

..sasa sijui kama wataanzisha chama, au watabaki ndani ya Ccm.
Akili za kibinafsi ni tatizo la watanzania wengi. Kujiona wanajua kuliko uhalisia wenyewe..

Wengi wapo humu na ukisoma maandishi yao unajua huyu anaishi na kinyongo na kinamtesa mpaka siku ya kwenda kaburini.
 
Akili za kibinafsi ni tatizo la watanzania wengi. Kujiona wanajua kuliko uhalisia wenyewe..

Wengi wapo humu na ukisoma maandishi yao unajua huyu anaishi na kinyongo na kinamtesa mpaka siku ya kwenda kaburini.

..waliotenda dhuluma, unyama, na ukatili, wana hasira na kinyongo kuliko wahanga au victims wa maovu yao.
 
..waliotenda dhuluma, unyama, na ukatili, wana hasira na kinyongo kuliko wahanga au victims wa maovu yao.
Kujua madhara ya unyama unaotendwa ni karama kutoka kwa Mungu, Ndio hapa nguvu ya msamaha inapoingia.
 
Inaonesha hao viongozi huchekeana wakiwa hadharani tu, lakini wakiwa maeneo yao huwa ni watu tofauti

Kinachoandikwa hapa mtandaoni ni sehemu ya mipango ya kila kambi dhidi ya wenzao.

Kwasasa, kuna mitandao zaidi ya 3 imeundwa kuelekea 2030, kama hakutakuwa na nguvu kuizuia, Watanzania tutaumia 🙆
 
Kanisani mara nyingi Padre anayeongoza ibada huweka msisitizo wa kuiombea dunia nzima. Hukataza ile aina ya maombi yenye kunihusu mimi na watu wa familia yangu pekee. Huwa anasema tupunguze zile 'yangu' kila tunapoongea na Mungu. Kazi yangu, mume wangu, mke wangu, watoto wangu, nyumba yangu, jirani yangu. Padre kwa lugha ya kinabii kabisa amekuwa akikataza sala binafsi zenye ubinafsi mwingi ndani yake.

Anasisitiza kuombea walio wengi na hayo maombi yangu yawe ni sehemu tu ya nia pana. Namuelewa Padre kadri anavyorudia mahubiri yake pale katika mimbari ya kanisa, ni ujumbe wa upendo unaojali walio wengi. Lakini katika kuzama kwenye tafakuri naona kabisa kuwa maneno yake yanazisuta nafsi za mamilioni ya wanaolitumia hili jukwaa kwa nia mbalimbali haswa zile za kupanua uwezo wa mawazo yetu.

Naamini nia inayomsukuma Mgombea Urais mpaka akachukua fomu na kuilipia shilingi milioni moja kisha akazunguka nchi nzima kutafuta wadhamini, ni kuleta mchango wake katika mabadiliko chanya ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Naamini hiyo ndio nia ya kwanza kabisa ya Mgombea Urais, ikiwa anakabidhiwa ilani na kulazimika kuitekeleza kurasa baada ya kurasa hilo huwa ni suala la pili lakini la mwanzo kabisa ni kutumia kila alichonacho kwa faida ya wengine.

Nchi yetu imeshaongozwa na Marais sita mpaka dakika hii na wote hawa lengo lao kuu ni moja tu, na kizuri kwao ni kwamba wote wanatoka CCM wanatekeleza sera zile zile. Tofauti inaweza kuwa kwenye maarifa na utendaji kazi binafsi lakini wote wanayo nia moja kutoka ndani kabisa ya mioyo yao, kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya mtanzania mmoja mmoja kadri inavyowezekana.

Inashangaza kusoma humu namna baadhi yetu tunavyotamani kutoana macho kwa ushabiki tu wa hawa marais, wote hawa ni watekelezaji wa ilani ya CCM, ndio wanayokabidhiwa kama rejea yao baada tu ya mchakato wa kuapishwa na Jaji Mkuu.

Anachoweza kufanya Rais wa Awamu ya Kwanza hukifanya na yule wa Awamu ya Pili huendeleza pale anapoishia. Anachoweza kuendeleza wa Awamu ya Pili hukiendeleza mpaka pale atakapoishia na muendelezo wake anamuachia wa Awamu ya Tatu. Uhalisia umekwenda hivyo mpaka imefika awamu ya sita. Hivi ndio Tanzania inavyojengwa na chama kimoja cha CCM.

Hii mikwaruzano ni siasa za upambe ule ule unaodumu miongoni mwetu ambazo kwa kweli zinatuchukulia muda na akili bila ya sababu ya msingi. Marais wote sita ni watekelezaji wa ilani ya CCM, wanaachiana vijiti na kuendeleza anapoishia mtangulizi. Hajawahi kuingia miongoni mwao akatoka CHADEMA na kuingiza sera tofauti na zile zilizotimizwa na Mwasisi wa Taifa Julius Nyerere.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Hujiulizi tabia hii mbona haikuwepo mpaka alipoingia madarakani Magufuli?
 
To quote Brother Mouzone kutoka ile series ya zamani ya The Wire "The game is the game"...Siasa kwa ujumla ni mchezo wa watu wachache..wanasiasa wote wanaelewa mamlaka iko and they know how to preserve their power and influence. Ni mchezo wa watu wachache hamtakiwi kuwa wengiii hence they will always move chess pieces to make sure it stays that way..sio wapinzani sio maccm.. mara moja moja inatokea anomaly ya watu wa juu kutoka nje ya mfumo,lkni mambo huwa yanatokea na watu wapo wanaohakikisha yanatokea Ili mfumo urudi katika mpangilio wake.
 
Unachosema ni kipya kabisa ukweli ni kwamba kimeandikwa katika ilani ya chama inayoelekeza awamu nzima nini kitafanyika. Tatizo ni sisi namna tunavyotsiri kile kilichofanyika kwa maana ya kukosoa jinsi kilivyofanyika.

Ununuzi wa ndege uliandikwa kwenye ilani na JPM akahakikisha anazinunua ndege na zinaanza kazi, hapo hapo kwa kutoelewa vyema kilichomo kwenye ilani tukaanza kuzipinga tukisema eti zoezi zima halikufuata utaratibu wa kupitia kwanza bungeni wakati ukweli ni kwamba michakato yote ya ununuzi wa hizo ndege ina baraka za bunge.
CCM hawakuwa na ilani ya uchaguzi, bali waliorodhesha mahitaji yote ya binadamu, kutoka kwenye hiyo orodha chochote watakachofanikisha kutekeleza wanasema wametekeleza ilani yao!
 
Kujua madhara ya unyama unaotendwa ni karama kutoka kwa Mungu, Ndio hapa nguvu ya msamaha inapoingia.

..tatizo liko kwa waliotenda uovu.

..wana hasira ya kukosa mamlaka ya kuendelea na uovu wao.

..hawako tayari kutubu makosa yao na kuomba msamaha.

..wanakwamisha process ya kupatana, kusamehewa, na kuridhiana.
 
Back
Top Bottom