Maalim wangu usemacho hakina ubishi hakika Yanga na Simba ni watani wa jadi ila wapenzi wa kila timu tulikuwa na mapenzi ya dhati kwa timu zetu,bahati nzuri Barza yetu ni mseto lakini ukikuta tunavyo interact kwenye Ukwala na Uabijo ni raha tupu.
Maalim sitaki ubishi na wewe lakini Marehemu kiguru haiwezekani awe kiboko yetu,hata kwetu kuna watu ambao walikuwa kiboko kwenu kwa uchache tuu kulikuwa na Marehemu Mnuwili,Samuel Copper,Zoom bila kumsahau Marehemu Tokyo (aliacha kazi UDA kujakuendesha Bus Yanga)! Kwa kumalizia Amiri Mgido Abijo mlikuwa hamuoni ndani.
[emoji3] [emoji2] [emoji3] [emoji1]
Mtembeni,
Nakutaka ruksa tena nizungumze na wana Simba wenzangu.
Huyu
Mtembeni kama kawaida ya Yanga hawakubali kushindwa.
Hao wote aliowataja mie nakuja na shujaa mmoja tu nione kama
yeye ana mafano wa huyo -
Bin Sudi muuza madafu Odeon Cinema.
Lakini jambo moja niseme hapa hawa Yanga ni muhimu maana ndiyo
wanafanya damu zizunguke kwetu si unaona hapa ananvyotaka bila
sababu kunipandisha midadi tubwatizane.
Ndugu yangu umenikumbusha
Mnuwili.
Barza nitakupeni kisa cha
Mnuwili na
Hafidh Ahmed Saleh.
Muarabu na Mmakonde.
Maarufu,
Hafidh Liwali kwa kuwa baba yake ndiye aliyekuwa liwali
wa Dar es Salaam katika miaka ya 1940 na yeye mwenyewe akacheza
Yanga.
Leo nimemkacha mtani wangu
Kambi Kilago.
Nasubiri ''steam,'' zake zipoe kwanza.
Hofu yangu ni kuwa anaweza kunigongea mlango In Shaallah kesho asubuhi.