Marekani: Aliyeua Watu Weusi 10 kwa risasi alipanga kuendelea za tukio kama hilo sehemu nyingine pia

Marekani: Aliyeua Watu Weusi 10 kwa risasi alipanga kuendelea za tukio kama hilo sehemu nyingine pia

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
1652769825153.png

Kijana Payton Gendron, 18, ambaye aliwaua watu 13 kwa kuwafyatulia risasi, 10 kati yao wakiwa wenye rangi nyeusi inaelezwa alipanga kufanya mauaji zaidi kama angetoroka eneo la tukio Jijini New York, Marekani.

Kamishna wa Polisi, Joseph Gramaglia amesema: “Alitaka kwenda kwenye gari alekee Jefferson Avenue ili kuendelea kufyatua risasi kama alivyofanya eneo la Buffalo."

Inaelezwa FBI wamelazimika kuingilia kati kuchunguza tukio hilo linalodaiwa kutokana na chuki dhidi ya Watu Weusi aliyokuwa nayo kijana huyo.

Rais wa Marekani, Joe Biden na mkewe, Jill Biden wanatarajiwa kutembelea eneo hilo la tukio leo Mei 17, 2022.

Source: CNN
 
Ubaguzi wa rangi hauwezi kuisha...
 
Wamarekani mna Nini kwenye ishu hi shooting ya watu ovyoovyo? Kwa umri wangu huu sijawahi sikia nchi nyingine yenye matukio Kama haya ya shooting ya watu bila sababu ya maana zaidi ya us?
Je Ni kwasababu ya Sera zake katika silaha? Kwamba kila mtu hata kichaa ana bunduki?
Poleni sana wafiwa
 
Wamarekani mna Nini kwenye ishu hi shooting ya watu ovyoovyo? Kwa umri wangu huu sijawahi sikia nchi nyingine yenye matukio Kama haya ya shooting ya watu bila sababu ya maana zaidi ya us?
Je Ni kwasababu ya Sera zake katika silaha? Kwamba kila mtu hata kichaa ana bunduki?
Poleni sana wafiwa
Midude ni mibaguzi hatari, history inajirudia tu, hawa wanasapoti wazungu humu akili zao kama mazombi yaani ipoipo tu, vitu viko wazi ila litatokea jitu litatetea ujinga, usishangae humu yakawa yanatetea ushoga, ukiwauliza mzungu kawasaidia nn watakuambia condom na dawa zaukimwi
 
Huenda wakiweka Sheria Mtu akifanya Mass shooting namna hii ahukumiwe Kunyongwa, tena hukumu itekelezwe mbele ya vyombo vya habari ili iwe fundisho.. Maana hii tabia imeanza kuota mizizi sasa
 
Midude ni mibaguzi hatari, history inajirudia tu, hawa wanasapoti wazungu humu akili zao kama mazombi yaani ipoipo tu, vitu viko wazi ila litatokea jitu litatetea ujinga, usishangae humu yakawa yanatetea ushoga, ukiwauliza mzungu kawasaidia nn watakuambia condom na dawa zaukimwi
Kondom na dawa za ngoma hizo zote zinahusiana na ule mchezo wetu pendwa was wakubwa tu watoto wakishalala
 
Back
Top Bottom