Marekani hajawahi kujifunza: Kufanya kitu kile kile ambacho hakijaweza kumletea matarajio aliyotegemea. They are not pragmatic!

Marekani hajawahi kujifunza: Kufanya kitu kile kile ambacho hakijaweza kumletea matarajio aliyotegemea. They are not pragmatic!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Marekani imekuwa ikijaribu kuzuia maendeleo ya nchi inazozihofia kwa kuziwekea vikwazo kwa matumaini kwamba zitadhoofika kiuchumi na kuzifanya zisiendelee kijeshi hata kuzifanya zisiwe tishio tena. Mategemeo yake ni kuwa zitakuja kumpigia magoti na kumwabudu kana kwamba kuwepo kwao kunategemea hisani ya marekani!

MIFANO:
1. Iran: Taifa la Iran limekuwa tishio kwa Marekani kwa maana ya nguvu za kiuchumi kupitia mafuta na kisha uchumi huo kuendeleza kujiimarisha kijeshi kitu ambacho ni tishio kwa Marekani. Marekani inataka lisiwepo Taifa linaloweza kumvimbia kama halikubaliani na matakwa yake!! Kwa hiyo Marekani iliiwekea vikwazo lukuki vya kiuchumi nchi ya Iran kwa matarajio kwamba itaporomoka sana kiuchumi na kijeshi hivyo kuilazimisha kusalimu amri na kuiangukia marekani.

Kinyume chake Iran haikuporomoka kihivyo kiasi cha kushindwa kuendeleza mipango yake ya kujiimarisha kijeshi na kuwa tishio kubwa zaidi kwa marekani kuliko awali. Sasa hivi Iran iko mstari wa mbele katika teknologia ya drones za kivita, makombora ya masafa marefu, na utaalamu wa teknologia ya nyuklia!. Ia ina meli na manowari za kivita na vyote hivi imejiendeleza yenyewe pamoja na uwepo wa vikwazo. Kwa sasa Iran ni tishio zaidi kijeshi kuliko ilivyokuwa kabla ya vikwazo. Kwa hiyo kwa Iran havikuweza kuipatia Marekani matokeo iliyoyatarajia.

2. Korea ya kaskazini: Korea ya Kaskazini ilikuwa tishio kwa Marekani tangu wakati wa vita vya korea. Ili kuizuia korea ya kaskazini isijiimarishe kiuchumi na kijeshi, Marekani pia iliiwekea vikwazo korea ya kaskazini mbali na vile vya umoja wa mataifa. Lakini pamoja na vikwazo hivyo Korea ya kaskazini imekuwa tishio zaidi leo kijeshi kwa kufanikiwa kutengeneza silaha za nyuklia, makombora ya masafa marefu, kurusha satelite angani na kadhalika. Pia kwa sasa Korea ya kaskazini ni tishio zaidi kijeshi kuliko ilivyokuwa kabla ya vikwazo!! Kwa sasa Marekani haiwezi kuthubutu kuishambulia Korea ya kaskazini kama ilivyofanya Libya au Iraq.

3. Urusi: Pia Marekani na washirika wake waliamini kuwa kwa kuiwekea vikwazo Urusi itaporomoka sana kiuchumi na kuilazimisha isalimu amri kwenye vita vyake na Ukraine!! Kinyume chake vikwazo hivyo vimeshindwa kuilazimisha urusi kusalimu amri badala yake uchumi wa nchi za magharibi ndio ulioathirika, na mataifa yanayoinukia kama India, Brazil, China nk yameamua kuanza kutumia fedha ya nchi zao kwenye biashara ya kimataifa na kuanza kupunguza matumizi ya dola ya marekani kitu ambacho marekani haikutarajia. Kwa sasa Urusi ni tishio zaidi kwa nafasi ya marekani maana kwa sasa urusi inayaongoza mataifa mengine kuangusha upolisi wa marekani kimataifa/American hegemony, na marekani si tena sauti ya mwisho kama ilivyokuwa inajiamini. A multipolar world is developing under the guidance of Russia and China!

Kama hiyo haitoshi, waswahili husema sikio la kufa halisikii dawa!! Hivi sasa Marekani inaiandama sana China kwa kuanza kuiwekea vikwazo vya kiuchumi na kupiga marufuku kuishirikisha teknologia ya juu katika vitu mbali mbali kama vile semiconductors technology. Lengo ni kuikwamisha isiwe tishio zaidi kiuchumi na kijeshi!! Ninashangaa: Kama ilishindwa kuikwamisha Iran na korea ya kaskazini kujiimarisha kijeshi je itafanikiwa kwa China?

Uncle Sam keshaanza kuadhirika mdogo mdogo na bado!
 
Chura amemwongezea mwendo baada ya kumpiga teke.

Wanaidosha dola waione jeuri yake.

Screenshot_20230314-140022.jpg
 
Kwa akili ya Marekani yuko tayari aumize uchumi wake mwenyewe katika harakati za kumkwamisha China kwa kumwekea vikwazo!!

Biden willing to damage US economy to counter China – US Treasury​

Janet Yellen has conceded that protecting national security may come at an economic cost
Biden willing to damage US economy to counter China – US Treasury

US Treasury Secretary Janet Yellen arrives to deliver a speech on Wednesday at John Hopkins University in Washington. © Getty Images / Anna Moneymaker
President Joe Biden will stop at nothing to protect America against security threats posed by China, even if it means damaging the US economy, Treasury Secretary Janet Yellen has claimed.
 
Marekani imekuwa ikijaribu kuzuia maendeleo ya nchi inazozihofia kwa kuziwekea vikwazo kwa matumaini kwamba zitadhoofika kiuchumi na kuzifanya zisiendelee kijeshi hata kuzifanya zisiwe tishio tena. Mategemeo yake ni kuwa zitakuja kumpigia magoti na kumwabudu kana kwamba kuwepo kwao kunategemea hisani ya marekani!!

MIFANO:
1. Iran: Taifa la Iran limekuwa tishio kwa Marekani kwa maana ya nguvu za kiuchumi kupitia mafuta na kisha uchumi huo kuendeleza kujiimarisha kijeshi kitu ambacho ni tishio kwa Marekani. Marekani inataka lisiwepo Taifa linaloweza kumvimbia kama halikubaliani na matakwa yake!! Kwa hiyo Marekani iliiwekea vikwazo lukuki vya kiuchumi nchi ya Iran kwa matarajio kwamba itaporomoka sana kiuchumi na kijeshi hivyo kuilazimisha kusalimu amri na kuiangukia marekani.

Kinyume chake Iran haikuporomoka kihivyo kiasi cha kushindwa kuendeleza mipango yake ya kujiimarisha kijeshi na kuwa tishio kubwa zaidi kwa marekani kuliko awali. Sasa hivi Iran iko mstari wa mbele katika teknologia ya drones za kivita, makombora ya masafa marefu, na utaalamu wa teknologia ya nyuklia!. Ia ina meli na manowari za kivita na vyote hivi imejiendeleza yenyewe pamoja na uwepo wa vikwazo. Kwa sasa Iran ni tishio zaidi kijeshi kuliko ilivyokuwa kabla ya vikwazo. Kwa hiyo kwa Iran havikuweza kuipatia Marekani matokeo iliyoyatarajia.

2. Korea ya kaskazini: Korea ya Kaskazini ilikuwa tishio kwa Marekani tangu wakati wa vita vya korea. Ili kuizuia korea ya kaskazini isijiimarishe kiuchumi na kijeshi, Marekani pia iliiwekea vikwazo korea ya kaskazini mbali na vile vya umoja wa mataifa. Lakini pamoja na vikwazo hivyo Korea ya kaskazini imekuwa tishio zaidi leo kijeshi kwa kufanikiwa kutengeneza silaha za nyuklia, makombora ya masafa marefu, kurusha satelite angani na kadhalika. Pia kwa sasa Korea ya kaskazini ni tishio zaidi kijeshi kuliko ilivyokuwa kabla ya vikwazo!! Kwa sasa Marekani haiwezi kuthubutu kuishambulia Korea ya kaskazini kama ilivyofanya Libya au Iraq.

3. Urusi: Pia Marekani na washirika wake waliamini kuwa kwa kuiwekea vikwazo Urusi itaporomoka sana kiuchumi na kuilazimisha isalimu amri kwenye vita vyake na Ukraine!! Kinyume chake vikwazo hivyo vimeshindwa kuilazimisha urusi kusalimu amri badala yake uchumi wa nchi za magharibi ndio ulioathirika, na mataifa yanayoinukia kama India, Brazil, China nk yameamua kuanza kutumia fedha ya nchi zao kwenye biashara ya kimataifa na kuanza kupunguza matumizi ya dola ya marekani kitu ambacho marekani haikutarajia. Kwa sasa Urusi ni tishio zaidi kwa nafasi ya marekani maana kwa sasa urusi inayaongoza mataifa mengine kuangusha upolisi wa marekani kimataifa/American hegemony, na marekani si tena sauti ya mwisho kama ilivyokuwa inajiamini. A multipolar world is developing under the guidance of Russia and China!!

Kama hiyo haitoshi, waswahili husema sikio la kufa halisikii dawa!! Hivi sasa Marekani inaiandama sana China kwa kuanza kuiwekea vikwazo vya kiuchumi na kupiga marufuku kuishirikisha teknologia ya juu katika vitu mbali mbali kama vile semiconductors technology. Lengo ni kuikwamisha isiwe tishio zaidi kiuchumi na kijeshi!! Ninashangaa: Kama ilishindwa kuikwamisha Iran na korea ya kaskazini kujiimarisha kijeshi je itafanikiwa kwa China?

Uncle Sam keshaanza kuadhirika mdogo mdogo na bado!!
Uzi bora kabisa kiongozi umeendika fact kabisa
 
Marekani anaporomoka alafu nchi gani unaona kama inachukua nafasi ya USA?
 
Marekani anaporomoka alafu nchi gani unaona kama inachukua nafasi ya USA?
Shida ya wwengi ndyo mnataka icho ila kumbuka mambo huanza polepole kma utani na kuyadharau na kuisi ilo haliwezekani njia ya kuinusuru marekani ni trump kushika nchi bila ivyoo tutaona mengi
 
Shida ya wwengi ndyo mnataka icho ila kumbuka mambo huanza polepole kma utani na kuyadharau na kuisi ilo haliwezekani njia ya kuinusuru marekani ni trump kushika nchi bila ivyoo tutaona mengi
Yaani nchi ya Marekani yote unamwona Trump ndo mwenye uwezo? Huko nchi za wenzetu wakiona nchi inayumba hawatafuti kiongozi bali wanaangalia sehemu za kuziboresha kwenye taasisi zetu...taasisi zao ndo zinaongoza nchi.
 
Kwa akili ya Marekani yuko tayari aumize uchumi wake mwenyewe katika harakati za kumkwamisha China kwa kumwekea vikwazo!!

Biden willing to damage US economy to counter China – US Treasury​

Janet Yellen has conceded that protecting national security may come at an economic cost
Biden willing to damage US economy to counter China – US Treasury

US Treasury Secretary Janet Yellen arrives to deliver a speech on Wednesday at John Hopkins University in Washington. © Getty Images / Anna Moneymaker
President Joe Biden will stop at nothing to protect America against security threats posed by China, even if it means damaging the US economy, Treasury Secretary Janet Yellen has claimed.
Zile ban alizomwekea china zina fireback. Sasa china ndio the largest market ya EV maker mwaka jana china kauza magari milion 23 compared to america ambaye kauza magari milion 10 na Japan milion 7.
Export ya china imeongezeka kwa asilimia 14.
Mwaka huu katika maonyesho ya Shanghai week hii, BYD ambaye ni mshindani wa tesla kazindua gari ambalo linauzwa $11000 ambalo linakupa range ya mile 300 kwa kilichaji mara moja huku cheapesr tesla ev inauzwa $33000, uzinduzi huu ukafanya hisa za tesla ziangule kwa asilimia 12. Huawei naye kaonyesha vifaa vyake vya 5G na system zake za 5g za viwanda huku akitangaza kuja na 5.5G na kufamya hisa za cisco zianguke kwa 8.1%.
Hii wanaiita 4th industrial generation hii vita ya kiuchumi ikija kuisha US atakuwa kaumia zaidi.
 
Back
Top Bottom