Marekani na washirika wake EU wameisaliti Ukraine

Marekani na washirika wake EU wameisaliti Ukraine

DALA

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
2,256
Reaction score
4,647
Awali ya yote natangaza wazi kwamba mimi ninaiunga mkono Urusi.

Hata hivyo, kwa mtu yeyote ambaye amefuatilia hii vita, hitimisho iko wazi. Urusi pamoja na kuchukua muda mrefu kukamilisha malengo yake tofauti na wengi tulivyodhani ukizingatia uwezo wa Urusi kijeshi, bado ushindi upo kwake.

Kiuchumi na kisiasa, Urusi inapiga hatua kubwa sana japo inakuja kwa gharama ya damu ya wanajeshi wengi na halaiki ya raia. Ila kwa kuwa hii ndiyo njia pekee waliyoina ni sahihi, hawanabudi kulipa gharama ili kuyafikia malengo yao hususani kiusalama kama walivyodai.

Narudi sasa upande wa Ukraine, nadhani Raisi wa Ukraine siyo mwanafunzi mzuri wa historia, na hiyo imempelekea yeye kufanya makosa ya kiufundi toka mwanzo wa mgogoro hata kabla ya vita. Pamoja na kwamba alitambua kuwa na jirani mbabe, mwenye nguvu kubwa kijeshi, hakuona umuhimu wa kutumia diplomasia kutatua migogoro badala yake, alikimbilia kwa rafiki wa mbali huku akitarajia msaada endapo kingenuka.

Hakukua kwamba huyu jirani yake anaogopwa hata na huyo rafiki aliyemkimbilia, hivyo rafiki yake asingeweza kujiingiza ulingoni moja kwa moja kwa kuogopa varangati.

Lakini zaidi ya yote, hakutambua kwamba rafiki yake anamtegemea adui yake kwa vitu vingi ambavyo hawezi kulubali kuvipoteza kisa yeye Ukraine ameshindwa kuyajenga na jirani. Hakutambua pia kuna uwezekano mkubwa sana adui yake akapatana na rafiki yake kidiplomasia na kuyajenga baada ya vita kama ambavyo natabiri kutokea punde tu baada ya Urusi kumaliza shughuli. Kukosa kwake Zelensky kutambua haya, kulimfanya kiburi na jeuri kwa jirani katili. Hapa sasa anavuna mbegu ya jeuri yake.

Mwanzoni mwa vita, Zelensky alitakiwa asomo alama za nyakati. Hata kabla ya vita alitakiwa awe mjanja, angefanya maamuzi yenye tija kwa taifa lake kuliko tunayoyashuhudia.

Kwamba Marekani walikuwa tayari kumtorosha aende kwao ilikuwa ni taa nyekundu. Ilionyesha kwamba Marekani hana nia ya kuingia vitani kumsaidia kwa namna yoyote ile. Pale Zelensky alitakiwa aone umuhimu wa mjadala kidiplomasia, angetumia fursa ile kwenda kwenye meza ili amalize ugomvi. Badala yake, alijihisi kuwa na marafiki wababe. Marafiki wakampa kiburi, akajionyesha kama shujaa anaenda kwenye uwanja wa vita huku amevaa magwanda, alidhani vita ni kitu cha mchezo.

Marafiki wakampamba, akapewa majukwaa ya kuhutubia mabunge, akapewa heshima na mabunge lakini maombi yake hata moja hayakupata majibu.

1. Aliomba anga ifungwe- wakasema hawawezi kuingia kwenye mgogoro moja kwa moja na Urusi. Hiyo hakuona kama taa nyekundu.

2. Akaomba apewe silaha - washirika wakuvuta sana miguu mpaka leo, hajapewa aina ya silaha ambazo zingempa angalau uwezo uwanjani.

3. Akaomba waiwekee mafuta ya Urusi vikwazo - mpaka kesho, wanaendelea kununua mafuta ya urusi.

Kimsingi, Zelensky amesalitiwa na Marekani pamoja na washirika wake.

Lakini pia Zelensky ni mpuuzi sana, kwasababu wananchi wa Ukraine hawakumchagua Joe Biden au Borris au Macron. Walimchagua Afande maamuzi ya kuwalinda na kusimamia nchi yao, ni yeye tu ndiyo mwenye maamuzi juu ya yote toka mwanzo.

Tatizo, Zelensky alikuwa mpuuzi kiasi cha kuingia vitani na silaha za kuomba, kwamba nchi yake inaenda vitani na Urusi kwa silaha za kuokoteza ni ujinga wa hali ya juu. Kwa wanaosoma historia, kuna kitabu kiliandikwa na mwanajeshi mmoja aliyepigana kwenye WW2, kuna sehemu anaeleza kwamba kilichowapa Urusi ushindi dhidi ya Ujerumani ni wingi wa wanajeshi wake, kwamba unaweza kuwaua ukadhani wameisha, mara pap unashangaa wanakuja wengine kwa maelfu. Hivyo vifo vya wanajeshi wa Urusi haimaanishi Urusi inashindwa vita hata kidogo.

Kwa sasa, ningekuwa Zelensky ningeomba poo, yaishe. Akiendeleza ujinga, nahisi Urusi itaendelea kumega ardhi ya nchi yake taratibu mpaka atakapohisi ameridhika. Kwa sasa Mataifa ya Magharibi na Marekani tayari yamegawanyika na wanaona silaha zao hazitoi matokeo ya aina yoyote chanya.

Kuanza vita ni rahisi ila kumaliza vita ni kazi zaidi.

Pole kwa Ukraine, naamini Zelensky anaelewa sasa kwamba Marekani siyo wa kumuamini na anatambua kwamba Urusi siyo Zimbabwe. Vikwazo havisaidii.
 
Awali ya yote natangaza wazi kwamba mimi ninaiunga mkono Urusi.

Hata hivyo, kwa mtu yeyote ambaye amefuatilia hii vita, hitimisho iko wazi. Urusi pamoja na kuchukua muda mrefu kukamilisha malengo yake tofauti na wengi tulivyodhani ukizingatia uwezo wa Urusi kijeshi, bado ushindi upo kwake.

Kiuchumi na kisiasa, Urusi inapiga hatua kubwa sana japo inakuja kwa gharama ya damu ya wanajeshi wengi na halaiki ya raia. Ila kwa kuwa hii ndiyo njia pekee waliyoina ni sahihi, hawanabudi kulipa gharama ili kuyafikia malengo yao hususani kiusalama kama walivyodai.

Narudi sasa upande wa Ukraine, nadhani Raisi wa Ukraine siyo mwanafunzi mzuri wa historia, na hiyo imempelekea yeye kufanya makosa ya kiufundi toka mwanzo wa mgogoro hata kabla ya vita. Pamoja na kwamba alitambua kuwa na jirani mbabe, mwenye nguvu kubwa kijeshi, hakuona umuhimu wa kutumia diplomasia kutatua migogoro badala yake, alikimbilia kwa rafiki wa mbali huku akitarajia msaada endapo kingenuka.

Hakukua kwamba huyu jirani yake anaogopwa hata na huyo rafiki aliyemkimbilia, hivyo rafiki yake asingeweza kujiingiza ulingoni moja kwa moja kwa kuogopa varangati.

Lakini zaidi ya yote, hakutambua kwamba rafiki yake anamtegemea adui yake kwa vitu vingi ambavyo hawezi kulubali kuvipoteza kisa yeye Ukraine ameshindwa kuyajenga na jirani. Hakutambua pia kuna uwezekano mkubwa sana adui yake akapatana na rafiki yake kidiplomasia na kuyajenga baada ya vita kama ambavyo natabiri kutokea punde tu baada ya Urusi kumaliza shughuli. Kukosa kwake Zelensky kutambua haya, kulimfanya kiburi na jeuri kwa jirani katili. Hapa sasa anavuna mbegu ya jeuri yake.

Mwanzoni mwa vita, Zelensky alitakiwa asomo alama za nyakati. Hata kabla ya vita alitakiwa awe mjanja, angefanya maamuzi yenye tija kwa taifa lake kuliko tunayoyashuhudia.

Kwamba Marekani walikuwa tayari kumtorosha aende kwao ilikuwa ni taa nyekundu. Ilionyesha kwamba Marekani hana nia ya kuingia vitani kumsaidia kwa namna yoyote ile. Pale Zelensky alitakiwa aone umuhimu wa mjadala kidiplomasia, angetumia fursa ile kwenda kwenye meza ili amalize ugomvi. Badala yake, alijihisi kuwa na marafiki wababe. Marafiki wakampa kiburi, akajionyesha kama shujaa anaenda kwenye uwanja wa vita huku amevaa magwanda, alidhani vita ni kitu cha mchezo.

Marafiki wakampamba, akapewa majukwaa ya kuhutubia mabunge, akapewa heshima na mabunge lakini maombi yake hata moja hayakupata majibu.

1. Aliomba anga ifungwe- wakasema hawawezi kuingia kwenye mgogoro moja kwa moja na Urusi. Hiyo hakuona kama taa nyekundu.

2. Akaomba apewe silaha - washirika wakuvuta sana miguu mpaka leo, hajapewa aina ya silaha ambazo zingempa angalau uwezo uwanjani.

3. Akaomba waiwekee mafuta ya Urusi vikwazo - mpaka kesho, wanaendelea kununua mafuta ya urusi.

Kimsingi, Zelensky amesalitiwa na Marekani pamoja na washirika wake.

Lakini pia Zelensky ni mpuuzi sana, kwasababu wananchi wa Ukraine hawakumchagua Joe Biden au Borris au Macron. Walimchagua Afande maamuzi ya kuwalinda na kusimamia nchi yao, ni yeye tu ndiyo mwenye maamuzi juu ya yote toka mwanzo.

Tatizo, Zelensky alikuwa mpuuzi kiasi cha kuingia vitani na silaha za kuomba, kwamba nchi yake inaenda vitani na Urusi kwa silaha za kuokoteza ni ujinga wa hali ya juu. Kwa wanaosoma historia, kuna kitabu kiliandikwa na mwanajeshi mmoja aliyepigana kwenye WW2, kuna sehemu anaeleza kwamba kilichowapa Urusi ushindi dhidi ya Ujerumani ni wingi wa wanajeshi wake, kwamba unaweza kuwaua ukadhani wameisha, mara pap unashangaa wanakuja wengine kwa maelfu. Hivyo vifo vya wanajeshi wa Urusi haimaanishi Urusi inashindwa vita hata kidogo.

Kwa sasa, ningekuwa Zelensky ningeomba poo, yaishe. Akiendeleza ujinga, nahisi Urusi itaendelea kumega ardhi ya nchi yake taratibu mpaka atakapohisi ameridhika. Kwa sasa Mataifa ya Magharibi na Marekani tayari yamegawanyika na wanaona silaha zao hazitoi matokeo ya aina yoyote chanya.

Kuanza vita ni rahisi ila kumaliza vita ni kazi zaidi.

Pole kwa Ukraine, naamini Zelensky anaelewa sasa kwamba Marekani siyo wa kumuamini na anatambua kwamba Urusi siyo Zimbabwe. Vikwazo havisaidii.
Sasa ndo upuuzi gani umeandika hapa. Ni kama mipasho ya taaribu au kumsuta mtu uswahilini. Chambua mambo ukiwa balanced
 
Dah! Umechambua vizuri sana,ila naomba nikukosoe sehemu moja TU uliyoisema juu ya Muda aliotumia Urusi.
Naona hoja ya Muda aliotumia Urusi hii imekua ikirudiwa sana na watu mbalimbali,hususan Pro NATO.

Kwa ufahamu wangu katika vita kwa pande mbili zinazopigana Huwa Kuna kitu kinaitwa "Siri za Kambi".

Sisi wafuatiliaji wa vita,wala upande mmoja wa mahasimu,wala majasusi wa nchi nyingine hua tunasoma hisia TU za Upande mmoja wa mahasimu.
Au mahasimu hua wanasomama TU juu ya Siri za Kambi.

Hakuan sehemu yoyote Urusi walitamka juu ya Muda Gani watatumia.
Inawezekana kuwa ni kweli walipanga muda lkn hawakutuambia.
Inawezekana labda walipanga miezi SITA,sisi hatujui.,miezi minne sisi hawakutuambia.

Kama ukichunguza vizuri utagundua kuwa Ukraine ilikua Ina silaha nyingi kweli.
Ambazo Hadi Leo Urusi bado inaziharibu TU.
Achana na silaha zinazoingia kutoka nje mara baada ya op kuanza.
Nazu gumzia silaha zilizokua kwenye makambi ya kijeshi ya Ukraine kwa nchi yote ni nyingi mno.urusi abado anaziangamiza TU Hadi Leo.
Sasa kwa wingi wa silaha kiasi hicho sioni kama Urusi ingetunia wiki mbili,tatu au nne.
Sio Urusi bala hata wangekua NATO wenyewe.
Lakini kama kwa maana tu ya kupiga hovyo basi Urusi angeweza kutumia hata siku moja TU kumaliza mchezo.
Kama USA alitumia masaa TU kumaliza usumbufu huko Hiroshima na Nagasaki inamshinda ninj Urusi kutumia saa moja TU?
Jamani suala la muda ni Siri ya Kambi.
Ila kwa upinzani ambao Urusi kakutana nao ni kwamba,wanajeshi wa Ukraine sio watoto wa chekechea.
Wanajeshi wa Ukraine wanapigania ardhi Yao,nchi yao,mama zao ,baba zao ,dada zao na watoto wao,
Hawana pengine pa kwenda hapo Ukraine ndo kwao.kwa hiyo usitegemee askari wa Ukraine akawa na hisia sawa na askari wa kukodiwa.
Askari wa kukodiwa anaangalia fedha,askari wa Ukraine anaangalia taifa lake.huyu haangalii fedha.

NATO.
Nani asiejua NATO wanamsaidia Ukraine.
Nani asijua majasusi wa NATO ndio wanaotoa michongo ya walipo askari au Kambi za Urusi?
Nani asiejua moscova ilishambuliwa kwa msaada wa USA?
Nani asiejua Ukraine ilishashindwa mapema sana,kilichopo Sasa hivi ni NATO kurefusha TU op hii kwa matumaini kuwa wataichosha Urusi kiuchumi? Huku wakijua kua ukraine Hatashinda?

Tamaa hii ya kurefusha vita Iko kwa USA na wenzake wa NATO lakini bahati mbaya kwao Urusi imeonekana kutotetereka .

Suala la muda jamani hatukuambiwa ila sisi ni hisia zetu TU.
Hata kama Ukraine kwa ukubwa huo na kwa silaha ilizokua nazo hata kama Ingekua ni kisiwa haipakani kabisa na EU na kwa lengo la Urusi la ku demilitarize bado isingeweza kumaliza silaha hizo kwa mwezi mmoja nakataa.
 
Unajua watu hawaamini kinachoendelea,, Tulijua US ndiyo kapata mwanya wa kutumia UFO zake[emoji1787][emoji1787][emoji1787] lakini wap

Kaufyata muda sana. Sasa hivi hata ile kubwaka ameacha maana wananchi wake wanaumizwa na mfumuko wa bei, imebidi aanze mjadala kimya kimya na Urusi auziwe mbolea.

Urusi siyo Zimbabwe.
 
Kaufyata muda sana. Sasa hivi hata ile kubwaka ameacha maana wananchi wake wanaumizwa na mfumuko wa bei, imebidi aanze mjadala kimya kimya na Urusi auziwe mbolea.

Urusi siyo Zimbabwe.
Zelesky naye kuomba radhi anaona aibu... Hili la mbolea ndiyo limenichosha zaidi... Kweli Marekani Hana rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu..... Kuna raisi mmoja wa marekani alipata kunena"Damu zao zitakapomwagika uchumi wa America utazidi kunawili"
 
Back
Top Bottom