Marekani yatoa onyo jipya la usafiri wa Urusi

Marekani yatoa onyo jipya la usafiri wa Urusi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

1648625854004.png

Marekani imetoa onyo jipya la usafiri kwa Urusi ambayo inasema mamlaka "inaweza kuwatenga na kuwaweka kizuizini" Wamarekani nchini humo.

Ikitaja uwezekano wa kuwanyanyasa raia wa Marekani, onyo hilo linarudia wito kwa Wamarekani kutosafiri kwenda Urusi au kuondoka "mara moja". Pia ilionya Wamarekani kuhusu "utekelezaji holela wa sheria za mitaa".

Ushauri huo pia ulisema kulikuwa na ripoti zinazoendelea za raia wa Marekani "kutengwa na kuzuiliwa na jeshi la Urusi" wanapokuwa Ukraine, au wanapohama kwa ardhi kupitia eneo linalokaliwa na Urusi.

"Ikiwa unataka kuondoka Urusi, unapaswa kufanya mipango peke yako haraka iwezekanavyo,"onyo hilo lilisema. Marekani ilisimamisha ubalozi wake na ubalozi mdogo nchini Ukraine siku chache baada ya Rais Putin kutangaza uvamizi wake.

BBC Swahili
 
Nyie jifanyeni wakuda tu....urusi ikikamata ukiranja wa Dunia meusi maafrica mtakoma nawambia...bora USA mtaheshimika......Urusi hkn mweusi hata mmoja aliyeko madarakani....mtakula mavi..heee! Wale jamaa na china siyo kabisa...watawageuka hamtaamini.. bora zimwi likujualo li USA....mtamtamani USA lkn hamta muona.bora watishane tu lkn USA abaki super power....mrusi hamjui nyani wala hajawahi kukaa nao meza moja.
 
Back
Top Bottom