Mariam Sagini: Wababa wamekuwa wavivu wanaenda kwa Waganga kutafuta utajiri, Watoto wanaharibika

Mariam Sagini: Wababa wamekuwa wavivu wanaenda kwa Waganga kutafuta utajiri, Watoto wanaharibika

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mjumbe wa Baraza Kuu UWT Taifa, Mariam Sagini amesema kina baba wamekuwa wavivu wa kufanya kazi inafikia mawazo yanawapeleka kwa waganga kutafuta utajiri na huko wanapewa masharti ya kubaka mtoto wake wa kumzaa.

Akizungumza na Wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi katika Kata ya Nsemulwa Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi amesema kuwa wakina baba nao wamekuwa wakiongoza kuharibu watoto kwa namna hiyo kutokana na kushindwa kulea familia na kugeuka hatari katika familia.

"Baadhi ya kina baba wametuachia majukumu kina mama na hapo ikitokea mtoto ameharibika wanasema ni wamama ila akiwa mzuri ni wa baba sasa kama baba anatoka kimapenzi na mwanaye wa kumzaa akija ndugu nyumbani kwako na ukiangalia una watoto huwezi kumwamini maana ukimpa nafasi hatowaacha salama.

"Dunia imeharibika ndio, ila kina mama pia mtaulizwa mlikuja duniani kuzaa na kulea familia au kushindia kwenye vikundi? jukumu la wote kulea familia ila wakinamama wakipunguza ubize wa vikundi na soga mtaani wataboresha familia kwa sababu jukumu alilopewa na kulea mume wake na watoto wake," amesema
 
Uzuri wababa ni tofauti na wazee wa hovyo....

Wababa shame upon you
 
Back
Top Bottom