Mariam Wangwe na Jukwaa la Wahariri

Mariam Wangwe na Jukwaa la Wahariri

Status
Not open for further replies.
Mkuu hakwenda...na hawezi kwenda... bahati mbaya Ushahidi haupo ktk maandishi.

Mkandara,
Asha amesema alienda. Pia naona angelikuwa hajaenda tungeshasikia yameandikwa. Binafsi sijui maana sijasoma popote. Unasema hakwenda, Asha anasema alienda.

Inabidi tusubiri wengine watuelemishe.
 
Wewe toa hoja zako na sio kutumia mambo binafsi ya kujenga hoja zako,

Wewe unashangaa Msiba kufanyika kwa kaka wa marehemu ?? Acha uhuni ndugu yangu Je tukisema wewe ndio unatumiwa sio huyo mama anayetumiwa tutakua tumekosea??

Wewe hujui baadhi ya mila zetu Baba wa familia anapokua hayupo KAKA mkubwa ama mtu mmoja mwenye heshima huteuliwa na familia na ndiye ana act kama BABA MPYA wa FAMILIA??

Ama wewe hujui baadhi ya mila zetu Mwanamke hana ushauri wowote na ndugu wa marehemu wanaume ndio wanaamua nini wafanye na kwa wakati gani??
Unashaanga nini Arobaini kuwa kwa kaka wa marehemu?? Ama kwako CHADEMA/CCM ni bora sana kuliko udugu wa DAMU?

Ndugu yangu wee
Acha kabisa kuzungumza mambo ya aibu. Kaka kuwa Baba Mpya! siku hizi? wacha kabisa hiyo.
Kwa Taratibu na mila zetu hata kama mwanamke atarithiwa, basi maamuzi hufanyika nyumbani kwa marehemu wala siyo mahali pengine popote. Hivyo nyumbani halali kwa Chacha Wangwe ni Kijijini kwao huko Tarime na wala sio Mikocheni. Huko ndiko alikozikwa. Full stop..............
Hata hivyo kama Prof. Wangwe kama ndiye baba mpya wa familia ndiye mwenyejukumu la kulea hii familia, basi hata matamshi aliyoyatoa Mariam alitakiwa ayatoe huyo BABA MPYA na si vinginevyo. Hapo kama anamkubali Prof. Wangwe kuwa ndiye baba mpya, tayari ameshamkosea adabu hivyo anatakiwa aadabishwe kwa kukiuka taratibu, mila na desturi ambayo wewe ndugu yangu unaiamini.

Mtazamo wangu ni kuwa huyu sasa anaanza kusumbuliwa na njaa. Akae atulie aone anapata nini. Mbona mwenzake Dotto ana busara. Soma Mwananchi ya leo utaona alivyoongea kwa busara.
Watu wa aina hii wanataka kujihalalishia visivyo halali yao. Mama Gati hajasema, wao midomo juu tu.
Njaa njaaa itawaangamiza.
 
Mtanzania,
Yawezekana lakini sivyo nilivyosikia mimi na nimekuwa nilifuatilia kwa pembeni msiba wa Wangwe kwa sababu nataka kujua ukweli...
Mtililiko wa mambo yanayojitokeza tk msiba huu yanatisha sana...tumeona vifo kibao vya viongozi tena vinatatanisha zaidi lakini kifo hiki kimekuja na tungo nyingi sana..
Mimi nashauri itakuwa vizuri kama Mwanakijiji ataweza kuhojiana naye na ayaweke maswali haya wazi..

Unamkumbuka shahidi aliyefika sehemu ya ajali mzee Goerge Mwigunde?.. taarifa yake hadi leo ilipuuzwa hadi leo sijasikia mtu akimzungumzia wala kuijadili huyo MTU wa TATU...Kumbuka tu yule mzee alizungumza siku chache baada ya kusikia taarifa ya Malya ikitofautiana na Ukweli..Sio siku ya ajali kama watu wengi walivyojaribu kum discredit..
Kisha kama sikosei kuna watoto wa Marehemu ambao tunawaona wakiwa Dodoma nyumbani (sijui nyumba ya mke yupi) wakitoa ushahidi wao kumhusisha Mallya moj kwa moja na ajali hii kama dereva.
Mallya alitoka msafii na hana hata vumbi na wallet yake mkononi...
Kisha basi inasemekana Wangwe alikuwa akirudi Dar kuhudhuria mazishi.. kwa nini isiwe alikuwa akirudi Dar nyumbani kwa mkewe Marium!.. kumbuka watu wali question kwa nini alikuwa akienda Dar na kulikuwa na haja gani..
haya yote ni maswali ambayo ukiyatazama kwa makini mkuu yanazidi kupotosha kama vile kuna watu wamepangwa kuvuruga kabisa Upelelezi na ukweli kuhusiana na kifo cha Wangwe kwa kuendesha kampeni za kumtafuta mchawi nje ya clues za ajali yenyewe....Wanataka tuamini kuwa Chadema ndio mchawi lakini mimi naamini kabisa kuwa ukweli umefichwa na watu wakubwa sana...wapo wendawazimu watakao kubali kutumiwa kueneza chuki za kipumbavu..
 
Wanafamilia wa Wangwe waendela kulumbana (Mwananchi)
Na Frederick Katulanda, Tarime

MALUMBANO baina ya ndugu wa aliyekuwa mbunge wa Tarime kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), marehemu Chacha Wangwe, yamezidi kupamba moto baada ya dada wa mbunge huyo kuibuka na kumkana mke mdogo, Doto Mohamed, kuwa hatambuliki kwenye ukoo.


Kuibuka kwa dada wa mbunge huyo, Mary Zakayo Wangwe kumekuja siku mbili baada ya Dotto, ambaye alidai kuwa ndiye aliyeshirikiana na Wangwe hadi kupata ubunge, kupinga madai ya mke mwingine mdogo kuwa Chadema imeitelekeza familia ya marehemu, akisema kuwa ni mapema mno kuzungumzia hilo.


Mariam alikuwa wa kwanza katika malumbano hayo baada ya kuitisha mkutano na waandishi wa habari wiki iliyopita na kuzungumzia mambo mengi kuhusu utata wa kifo cha mbunge huyo, akilitaka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi zaidi, lakini akamwaga lawama kwa Chadema, jambo ambalo limezua malumbano baina ya wake hao na dhidi ya viongozi wa chama hicho, hasa katibu mkuu, Wilbroad Slaa.


Akizungumza na gazeti hili jana kijijini Kemakorere, dada huyo, Mary Zakayo Wangwe alisema kuwa Dotto Mohamed si mke halali wa marehemu Wangwe kwa kuwa walishatengana na kwamba aliwahi kumshtaki Ustawi wa Jamii akidai apewe mali, lakini akashindwa katika kesi hiyo.


Alisema Dotto hatambuliki katika familia yao kutokana na kuwa alitimuliwa wakati Wangwe akiwa hai kutokana na matatizo ya kifamilia ambayo yalifikia hadi mbunge huyo akalazwa ndani mara kadhaa akisaidiwa na mwanasheria maarufu, Tundu Lissu.


"Dotto alikuwa mtumishi wa ofisini kwa marehemu, pale LACOP," alisema dada huyo. "Akiwa mtumishi wake walianza uhusiano wa kimapenzi na marehemu na hivyo kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake na mkewe mkubwa Christina Gatti.


"Lakini kutokana na kumfanyia visa na vituko na hata kushtakiana waliachana. Waliishi wakiwa katika mgogoro huo kwa kipindi cha miaka mitano na kutengana."


Alisema wakati akiwa na Dotto, Wangwe hakuwa anatambua kuwa Dotto ni mke wa mtu, jambo ambalo lilisababisha mtafaruku baada ya mbunge huyo wa zamani wa Tarime kubaini ukweli.


"Kila mara walikuwa wakigombana kwa sababu ya tatizo hilo," alisema dada huyo.


"Leo tunashangaa anathubutu kujitokeza hadharani na kudai kuwa yeye ni mke wa marehemu. Hana haki hiyo kwa kuwa walishatengana na marehemu na ndipo Wangwe alipoamua kumuoa Mariam."


Hata hivyo, katika mahojiano yake na Mwananchi, Dotto alieleza bayana kuwa walishatengana na Wangwe.


Mary aliendelea kusema: "Sababu nyingine iliyomfanya atimuliwe na marehemu ni kuwa alimchukua na kukaa naye kimada akiwa na mimba ya mtoto (Mwajuma) ambaye baada ya kugombana na marehemu alimweleza mahakamani kuwa mtoto huyo si wake, jambo ambalo marehemu alitangaza kwa wanandungu na familia na kuwa kati ya watoto wawili Mwajuma na Gatti aliozaa naye, mtoto wake (Wangwe) ni Gatti."


Mary alidai Dotto amekuwa akitumiwa na Chadema kutokana na kukubaliana nao mambo yao na kwamba kwa sasa amekuwa akitoa kauli ambazo lengo lake ni kuisafisha Chadema kwa sababu amepewa ahadi ya kusaidiwa kisheria katika kesi ya kudai mirathi ya marehemu.


Dada huyo alionya kuwa masuala ya familia ya marehemu yako wazi, hivyo wanaotaka kuyaingilia wanajisumbua.


"Nadhani Chadema wanapaswa kutulia na kuacha mambo ya familia, wala wasiyaingilie, bado hawajatupatia majibu mengi kati ya maswali tunayouliza kila siku," alisema dada huyo.


"Watambue huyo si mke wa marehemu ingawa wao wanatangaza kumtambua. Wanapaswa wajue kuwa kusema kuwa wanamtambua Dotto ni kuingilia masuala ya familia.... hii ni familia ina mamlaka yake na wasemaji wake, sasa tunaomba Dk. Slaa asituingilie."


Dada huyo wa Marehemu alisema kitendo cha Dotto kuthubutu kuzungumzia masuala ya familia ni kutaka kujijengea uhalali kwa watu kuwa yeye ni mke halali wakati anajua na kutambua kuwa hana haki katika familia kwa vile marehemu alishamshinda katika kesi zake za kudai mali na kutengana na kwamba mahusiano waliyokuwa wamebakiza ni utunzaji watoto.


"Viongozi wa Chadema wanamtumia... anasahau kuwa wanapokuja Tarime wanashindwa kufika hata nyumbani kwa marehemu alipozikwa wanapita tu... wameshindwa kufika katika arobaini yake licha ya kufanyika Dar es salaam, wameshindwa kutoa hata rambirambi wakizingizia mambo mengi, leo wanamdanganya kusimama kusema uongo," alieleza.


Akizungumza na vyombo tofauti vya habari, Dk. Slaa alishangazwa na kitendo cha Mariam kuishutuma Chadema kuwa imeitelekeza familia ya Wangwe na kwamba haikuhudhuria arobaini ambayo mke huyo mdogo aliifanya jijini Dar es salaam.


"Sisi ni Watanzania," alisema Dk. Slaa. "Tunajua kuwa arobaini hufanyika nyumbani kwa marehemu. Hatujawahi kusikia arobaini zinafanyika sehemu mbili tofauti.


"Chadema ilihudhuria arobaini iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Tarime, lakini arobaini aliyoifanya Mariam ilikuwa ya mialiko. Alialika watu kwa majina, lakini Chadema haikualikwa.


"Tusingeweza kuhudhuria wakati hatukualikwa, lakini arobaini iliyofanyika kwa mke mkubwa tulihudhuria. Mariam aseme kama ana kitu kingine, lakini si kuitupia Chadema lawama."


Wangwe, ambaye alikuwa mbunge wa jimbao la Tarime na diwani wa Tarime Mjini, alifariki kwa ajali ya gari mkoani Dodoma wakati akiwa safarini kuelekea Dar es salaam.
 
Source:

Na Waandishi Wetu

FAMILIA ya aliyekuwa mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe, imesema inamtambua Bibi Mariam, kuwa miongoni mwa wajane watatu wa marehemu ndugu yao.

Na imemtaka Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa, kutorudia kutamka kuwa mwanamke huyo hakuwa mke halali wa marehemu.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, msemaji wa familia hiyo Profesa Samwel Wangwe, alimtaka Dkt. Slaa kuacha kuingiza siasa katika familia yao na kama alitaka kujua alipaswa kuuliza.

"Yule (Mariam) ni mke wa mdogo wetu, yeye (Dkt Slaa) hapaswi kuhoji mambo ya familia," alisema na kusisitiza kuwa familia inamtambua. Alisema wake wote watatu wa marehemu Wangwe waliolewa kwa ndoa ya kimila na kulipiwa mahari, hivyo alimalizana na wazazi wao.

Alisema anaamini Dkt. Slaa amekosea kwa kutoa kauli hiyo na anaamini kuwa hatarudia kutoa maneno ya aina hiyo.

Kauli hiyo ya Profesa Wangwe iliungwa mkono na mdogo wake, Bw. Gideon Wangwe, ambaye alimtaka Dkt. Slaa kuacha mara moja kuingilia masuala ya familia kwa kuwa Bibi Mariam alikuwa mke halali wa marehemu ndugu yao.

"Dkt. Slaa ameanza kuwa mwongo, kwa sababu huyo anayemsema ndiye anaishi na watoto wote tisa na ni ndiye anayewasomesha," alisema na kusisitiza kuwa wanamtambua kwa muda mrefu kuwa ni mke wa marehemu Wangwe.

"Kama anasema si mkewe basi awataje wale anaowafahamu ... ana ushahidi gani kuwa yeye si mke wa marehemu?," alihoji Profesa Wangwe na kuongeza kuwa kutokana na kauli yake hiyo, kwa sasa familia inafikiria kumpeleka mahakamani, kwa kuwa ameanza kudhalilisha familia na kutumia kifo cha ndugu yao kujitafutia umaarufu kisiasa.

Kwa upande wake, Bibi Mariam alisema madai yaliyotolewa na Dkt. Slaa dhidi yake kuwa si mke halali wa marehemu, inaonesha kuwa ni mwendelezo wa chuki dhidi ya familia yao hata baada ya kifo cha Bw. Wangwe.

Aliitafsiri kauli hiyo kuwa "ni ya kihuni na ya kike, kwani haikutakiwa kutolewa na mtu kama Dkt. Slaa, ambaye aliwahi kuwa padri.

"Kama anasema mimi sikuwa mke wake, aeleze yeye alihudhuria harusi ya nani kati ya wake watatu kati ya Ghati, Dotto na mimi (Mariam), wakati ndugu walioshiriki kunilipia mahari wananitambua," alisema Bibi Mariam.

Alisema Dkt. Slaa anapaswa kutambua kuwa hoja iliyopo mbele yao si nani mke wa marehemu, bali ni utata uliogubika mazingira ya kifo cha mumewe.

Huku akionekana wazi kukerwa na kauli hiyo, Bibi Mariam alisema hata wao wakiamua kumchambua Dkt. Slaa, si msafi, lakini hawawezi kufanya hivyo kwa sababu watakuwa wakifanya mambo aliyoyaita ya kike.

Alisema kama anasema yeye si mke halali wa marehemu ilikuwaje kifo kilipotokea alipewa nafasi ya kutambua mwili na kusimamia kazi ya uchunguzi iliyokuwa ikifanywa na madaktari.

"Dodoma aliniona nikiutambua mwili wa marehemu, iweje sasa ananikana?," alihoji na kuongeza kuwa hata kwenye mikutano ya CHADEMA alikuwa akipewa nafasi ya kujitambulisha kama mke wa marehemu Wangwe na Dkt. Slaa alikuwa akiona, iweje ahoji sasa?," alihoji.

Alimtahadharisha kuwa hizo siri ambazo Dkt. Slaa anadai atazitoa dhidi yake, awe na uhakika nazo vinginevyo akiendelea kumchafua, atamburuta mahakamani.

"Atakachokisema awe na uhakika, vinginevyo 'nitakufa' naye mahakamani," alisema na kusisitiza kuwa hawezi kunyamaza kutokana na vitisho vya Dkt. Slaa, badala yake ajiulize yale anayosema ana uhakika nayo vipi ndani ya jamii.

"Mimi ninachokisema kina maslahi kwa familia, aliyekufa ni mume wangu nataka uchunguzi ufanyike ili kuondoa majungu," alisema na kuongeza kuwa tangu kifo cha mumewe kitokee, hajawahi kusema kitu chochote hadi alipozungumza na waandishi wa habari Ijumaa wiki iliyopita.

Kuhusu kauli ya Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta ya kupuuza ombi lake la kutaka aunde Tume ya kuchunguza kifo cha marehemu Wangwe, alisema hakutarajia majibu yaliyotolewa na Spika.

"Kama anaona nilikosea, alipaswa kunishauri, anajua uchungu nilionao na yeye alikuwa na uchungu mwingi na alilia sana siku ya msiba, sasa leo anataka kutuambia uchungu aliokuwa nao umekwenda wapi?," alihoji Bibi Mariam.

Alisema kauli ya Bw. Sitta kuwa Bunge lisitwishwe mzigo wa kuchunguza kifo hicho, inalenga kuonesha kuwa leo hii kifo cha mumewe kimeishageuka mzigo kwa Bunge.

Akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki iliyopita, Bibi Mariam aliomba kufanyika upya kwa uchunguzi wa kifo cha mumewe. Pia alidai viongozi wa CHADEMA wamemtelekeza.

Wakati huo huo, viongozi wa CHADEMA wilaya ya Kinondoni, wamemtaka Dkt. Slaa kumwomba radhi mjane huyo, kutokana na kauli aliyoitoa kuwa hamtambui kama mke wa marehemu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu wa Vijana wa Wilaya ya Kinondoni, Bw. Maulid Mkwanja, alisema umoja huo umesikitishwa na kauli ya Dkt. Slaa kwa sababu Bi. Mariam anatambulika kama mke wake tangu zamani.

"Tangu zamani anafahamika kuwa ni mke wa marehemu Wangwe na kila alipokwenda iwe kwenye mikutano ya kichama alitambulishwa kuwa ni mke wake, iweje leo hii wamkane?," alihoji Bw. Mkwanja na kuongeza:

"Sisi kama chama wilaya, tunamtaka Dkt. Slaa amwombe radhi huyo mjane na kama hatafanya hivyo, watakutana ili kujua hatua za kuchukua."

Alisema kama Dkt. Slaa alikuwa na chuki binafsi na marehemu Wangwe asiziingize kwa mkewe au familia yake.

Kiongozi huyo alimtaka Dkt. Slaa awe anatafakari kauli zake kabla ya kuzitoa hadharani kwa sababu amemdhalilisha Bibi Mariam na watoto wake kwa ujumla.

Akizungumzia kauli ya Spika Bw Sitta, aliyoitoa baada ya mjane huyo kumwomba aunde Tume, alisema haikuwa busara kumwambia kuwa amekurupuka, bali alitakiwa kumsaidia.

"Alitakiwa amsaidie kwa kuunda Tume kwa kuzingatia kuwa kifo chake kiligubikwa na mazingira ya utata," alisema.

Dkt. Slaa alikaririwa akisema hawamtambui mjane wa Wangwe, Bibi Mariam aliyeomba kufanyika kwa uchunguzi upya, kwani wake za marehemu wanaowatambua wako Tarime.

Dkt. Slaa kupitia taarifa ya habari ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC Taifa) juzi alimtaka mjane huyo kuweka wazi ni kwa vipi CHADEMA haikushiriki mazishi ya Wangwe.

Marehemu Wangwe alikufa katika ajali ya gari iliyotokea Julai 28 mwaka huu, wilayani Kongwa eneo la Pandambili mkoani Dodoma akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam.

Mazingira ya kifo chake yalizua utata ambapo hadi sasa baadhi ya watu hawaamini kama alikufa kifo cha ajali ya kawaida.
 
Nadhani imefika wakati muafaka wa familia mbalimbali kuwa na msemaji wa familia asiyelemea upande wowote na atakayetenda haki kwa pande zote za familia na ukoo.

Na hili pia liwe funzo kwa wanaume wa Kitanzania wajue hizi ndoa za mitaala ni kuwabakizia watoto, wake na ndugu maumivu makubwa na mioyo mizito mno. Hebu angalia hili suala la Wangwe, yaani watoto hawana mtetezi wala msemaji, kila mtu ni mjuaji. Tazama watu wanvyobwabwaja hapa na wala Mke mkubwa hajafungua kinywa. I feel her pain and understand her choice of taking the high road. Na ni heri akae kimya. She deserves better

Wanaume kwa wanawake mtumie fursa hii kujifunza, maana pale ambapo ndoa ya kwanza ikaruhusiwa kuvunjika ina maana ndoa yenu tayari imetengeneza mwanya wa mtu yeyote katika ukoo kuisemea hiyo ndoa kadri apendavyo

Habari hii ndio imeanikwa kwa kuwa Wangwe alikuwa mbunge na almaarufu. Haya zile ndoa za makabwela je? Sipati picha na wala sipendi kufikiria. Jamani mtunze ndoa zenu. Haya ni mambo ya aibu.
 
Simwelewi huyu mama anaposema tabia aliyofanya Dr Slaa ni ya "kike", kumbe kitu kikiwa cha hovyo basi ni cha kike? Na huyu Slaa anapaswa kuwa makini na kauli zake sasa, aangalie asiporomoshwe kutoka kwenye kilele cha umaarufu kwa maneno yake mwenyewe kama ilivyompata Lyatonga.
 
This Wangwe Circus makes me sick!! I do not know kama watu wanawafikiria watoto wake...........those kids need serious therapy.
Its so sad!!
 
Wanafamilia wa Wangwe waendela kulumbana (Mwananchi)



"Dotto alikuwa mtumishi wa ofisini kwa marehemu, pale LACOP," alisema dada huyo. "Akiwa mtumishi wake walianza uhusiano wa kimapenzi na marehemu na hivyo kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake na mkewe mkubwa Christina Gatti.


"Lakini kutokana na kumfanyia visa na vituko na hata kushtakiana waliachana. Waliishi wakiwa katika mgogoro huo kwa kipindi cha miaka mitano na kutengana."


Alisema wakati akiwa na Dotto, Wangwe hakuwa anatambua kuwa Dotto ni mke wa mtu, jambo ambalo lilisababisha mtafaruku baada ya mbunge huyo wa zamani wa Tarime kubaini ukweli.


"Kila mara walikuwa wakigombana kwa sababu ya tatizo hilo," alisema dada huyo.




Mary aliendelea kusema: "Sababu nyingine iliyomfanya atimuliwe na marehemu ni kuwa alimchukua na kukaa naye kimada akiwa na mimba ya mtoto (Mwajuma) ambaye baada ya kugombana na marehemu alimweleza mahakamani kuwa mtoto huyo si wake, jambo ambalo marehemu alitangaza kwa wanandungu na familia na kuwa kati ya watoto wawili Mwajuma na Gatti aliozaa naye, mtoto wake (Wangwe) ni Gatti."

Kuna maneno nilifundishwa kuwa kila mwanaume ana vichwa viwili, kikubwa na kidogo, na huwa vinapokezana katika kufanya kazi ama kupumzika. Kichwa kikubwa kinapokuwa macho, kile kidogo hulala, na hali kadhalika kichwa kidogo kinapokuwa kazini kile kikubwa hupoteza kabisa uwezo wake. Wanaume tunaaswa, tuwe makini kuhakikisha siku zote kuwa ni kile kichwa kikubwa ndicho kinachotuongoza, ndipo kitaweza kusimamia kile kidogo ipasavyo. Vinginevyo tukikubali kuongozwa na kichwa kidogo basi matokeo yake ni kama haya, pamoja na heshima zote kwa marehemu mbunge Wangwe.
 
This Wangwe saga is becoming too much now! Na mahakamani kutaipata mwaka huu....
 
Simwelewi huyu mama anaposema tabia aliyofanya Dr Slaa ni ya "kike", kumbe kitu kikiwa cha hovyo basi ni cha kike?

this is crap

Na huyu Slaa anapaswa kuwa makini na kauli zake sasa, aangalie asiporomoshwe kutoka kwenye kilele cha umaarufu kwa maneno yake mwenyewe kama ilivyompata Lyatonga.

hii ndio hoja
 
Simwelewi huyu mama anaposema tabia aliyofanya Dr Slaa ni ya "kike", kumbe kitu kikiwa cha hovyo basi ni cha kike? Na huyu Slaa anapaswa kuwa makini na kauli zake sasa, aangalie asiporomoshwe kutoka kwenye kilele cha umaarufu kwa maneno yake mwenyewe kama ilivyompata Lyatonga.

Kithuku heshima yako Mkuu .
Maneno yako nadhani Mkuu Slaa ameyapata .Mimi binafsi nitampelekea ujumbe wako .Dawa ni Chadema kubakia kama Chama na leave alone maneno midomoni mwao juu ya Chacha Wangwe .Chacha amekuwa akiwa hero wa maendeleo ya Tanzania .Leo Prof Wangwe na kundi wanatumia vibaya shida hii kuwaunga mkono CCM.

Ni mbaya sana.
 
Wanafamilia wa Wangwe waendela kulumbana
Na Frederick Katulanda, Tarime

MALUMBANO baina ya ndugu wa aliyekuwa mbunge wa Tarime kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), marehemu Chacha Wangwe, yamezidi kupamba moto baada ya dada wa mbunge huyo kuibuka na kumkana mke mdogo, Doto Mohamed, kuwa hatambuliki kwenye ukoo.

Kuibuka kwa dada wa mbunge huyo, Mary Zakayo Wangwe kumekuja siku mbili baada ya Dotto, ambaye alidai kuwa ndiye aliyeshirikiana na Wangwe hadi kupata ubunge, kupinga madai ya mke mwingine mdogo kuwa Chadema imeitelekeza familia ya marehemu, akisema kuwa ni mapema mno kuzungumzia hilo.

Mariam alikuwa wa kwanza katika malumbano hayo baada ya kuitisha mkutano na waandishi wa habari wiki iliyopita na kuzungumzia mambo mengi kuhusu utata wa kifo cha mbunge huyo, akilitaka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi zaidi, lakini akamwaga lawama kwa Chadema, jambo ambalo limezua malumbano baina ya wake hao na dhidi ya viongozi wa chama hicho, hasa katibu mkuu, Wilbroad Slaa.

Akizungumza na gazeti hili jana kijijini Kemakorere, dada huyo, Mary Zakayo Wangwe alisema kuwa Dotto Mohamed si mke halali wa marehemu Wangwe kwa kuwa walishatengana na kwamba aliwahi kumshtaki Ustawi wa Jamii akidai apewe mali, lakini akashindwa katika kesi hiyo.

Alisema Dotto hatambuliki katika familia yao kutokana na kuwa alitimuliwa wakati Wangwe akiwa hai kutokana na matatizo ya kifamilia ambayo yalifikia hadi mbunge huyo akalazwa ndani mara kadhaa akisaidiwa na mwanasheria maarufu, Tundu Lissu.

"Dotto alikuwa mtumishi wa ofisini kwa marehemu, pale LACOP," alisema dada huyo. "Akiwa mtumishi wake walianza uhusiano wa kimapenzi na marehemu na hivyo kusababisha kuvunjika kwa ndoa yake na mkewe mkubwa Christina Gatti.

"Lakini kutokana na kumfanyia visa na vituko na hata kushtakiana waliachana. Waliishi wakiwa katika mgogoro huo kwa kipindi cha miaka mitano na kutengana."

Alisema wakati akiwa na Dotto, Wangwe hakuwa anatambua kuwa Dotto ni mke wa mtu, jambo ambalo lilisababisha mtafaruku baada ya mbunge huyo wa zamani wa Tarime kubaini ukweli.

"Kila mara walikuwa wakigombana kwa sababu ya tatizo hilo," alisema dada huyo.

"Leo tunashangaa anathubutu kujitokeza hadharani na kudai kuwa yeye ni mke wa marehemu. Hana haki hiyo kwa kuwa walishatengana na marehemu na ndipo Wangwe alipoamua kumuoa Mariam."

Hata hivyo, katika mahojiano yake na Mwananchi, Dotto alieleza bayana kuwa walishatengana na Wangwe.

Mary aliendelea kusema: "Sababu nyingine iliyomfanya atimuliwe na marehemu ni kuwa alimchukua na kukaa naye kimada akiwa na mimba ya mtoto (Mwajuma) ambaye baada ya kugombana na marehemu alimweleza mahakamani kuwa mtoto huyo si wake, jambo ambalo marehemu alitangaza kwa wanandungu na familia na kuwa kati ya watoto wawili Mwajuma na Gatti aliozaa naye, mtoto wake (Wangwe) ni Gatti."

Mary alidai Dotto amekuwa akitumiwa na Chadema kutokana na kukubaliana nao mambo yao na kwamba kwa sasa amekuwa akitoa kauli ambazo lengo lake ni kuisafisha Chadema kwa sababu amepewa ahadi ya kusaidiwa kisheria katika kesi ya kudai mirathi ya marehemu.

Dada huyo alionya kuwa masuala ya familia ya marehemu yako wazi, hivyo wanaotaka kuyaingilia wanajisumbua.

"Nadhani Chadema wanapaswa kutulia na kuacha mambo ya familia, wala wasiyaingilie, bado hawajatupatia majibu mengi kati ya maswali tunayouliza kila siku," alisema dada huyo.

"Watambue huyo si mke wa marehemu ingawa wao wanatangaza kumtambua. Wanapaswa wajue kuwa kusema kuwa wanamtambua Dotto ni kuingilia masuala ya familia.... hii ni familia ina mamlaka yake na wasemaji wake, sasa tunaomba Dk. Slaa asituingilie."

Dada huyo wa Marehemu alisema kitendo cha Dotto kuthubutu kuzungumzia masuala ya familia ni kutaka kujijengea uhalali kwa watu kuwa yeye ni mke halali wakati anajua na kutambua kuwa hana haki katika familia kwa vile marehemu alishamshinda katika kesi zake za kudai mali na kutengana na kwamba mahusiano waliyokuwa wamebakiza ni utunzaji watoto.

"Viongozi wa Chadema wanamtumia... anasahau kuwa wanapokuja Tarime wanashindwa kufika hata nyumbani kwa marehemu alipozikwa wanapita tu... wameshindwa kufika katika arobaini yake licha ya kufanyika Dar es salaam, wameshindwa kutoa hata rambirambi wakizingizia mambo mengi, leo wanamdanganya kusimama kusema uongo," alieleza.

Akizungumza na vyombo tofauti vya habari, Dk. Slaa alishangazwa na kitendo cha Mariam kuishutuma Chadema kuwa imeitelekeza familia ya Wangwe na kwamba haikuhudhuria arobaini ambayo mke huyo mdogo aliifanya jijini Dar es salaam.

"Sisi ni Watanzania," alisema Dk. Slaa. "Tunajua kuwa arobaini hufanyika nyumbani kwa marehemu. Hatujawahi kusikia arobaini zinafanyika sehemu mbili tofauti.

"Chadema ilihudhuria arobaini iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Tarime, lakini arobaini aliyoifanya Mariam ilikuwa ya mialiko. Alialika watu kwa majina, lakini Chadema haikualikwa.

"Tusingeweza kuhudhuria wakati hatukualikwa, lakini arobaini iliyofanyika kwa mke mkubwa tulihudhuria. Mariam aseme kama ana kitu kingine, lakini si kuitupia Chadema lawama."

Wangwe, ambaye alikuwa mbunge wa jimbao la Tarime na diwani wa Tarime Mjini, alifariki kwa ajali ya gari mkoani Dodoma wakati akiwa safarini kuelekea Dar es salaam.


source: mwananchi
 
Hii tena kasheshe.Dr.Slaa kajiingiza kwenye matatizo yasiyokuwa ya lazima kabisa.
 
Hii tena kasheshe.Dr.Slaa kajiingiza kwenye matatizo yasiyokuwa ya lazima kabisa.
ni sawa Dr. Slaa kijiingiza maana hii famimilia inachafua chama ambacho yeye ni katibu mkuu. issue hapa kifo kimegeuka politics
 
ni sawa Dr. Slaa kijiingiza maana hii famimilia inachafua chama ambacho yeye ni katibu mkuu. issue hapa kifo kimegeuka politics

Right on! watu wanataka CHADEMA ichafuke sijui wana malengo gani
 
Nadhani imefika wakati muafaka wa familia mbalimbali kuwa na msemaji wa familia asiyelemea upande wowote na atakayetenda haki kwa pande zote za familia na ukoo.

Na hili pia liwe funzo kwa wanaume wa Kitanzania wajue hizi ndoa za mitaala ni kuwabakizia watoto, wake na ndugu maumivu makubwa na mioyo mizito mno. Hebu angalia hili suala la Wangwe, yaani watoto hawana mtetezi wala msemaji, kila mtu ni mjuaji. Tazama watu wanvyobwabwaja hapa na wala Mke mkubwa hajafungua kinywa. I feel her pain and understand her choice of taking the high road. Na ni heri akae kimya. She deserves better

Wanaume kwa wanawake mtumie fursa hii kujifunza, maana pale ambapo ndoa ya kwanza ikaruhusiwa kuvunjika ina maana ndoa yenu tayari imetengeneza mwanya wa mtu yeyote katika ukoo kuisemea hiyo ndoa kadri apendavyo

Habari hii ndio imeanikwa kwa kuwa Wangwe alikuwa mbunge na almaarufu. Haya zile ndoa za makabwela je? Sipati picha na wala sipendi kufikiria. Jamani mtunze ndoa zenu. Haya ni mambo ya aibu.

Bimkubwa,

Familia zote zinakuwa na msemaji mmoja ila tu katika mazingira ya TZ ukiingiza siasa na umaskini ni balaa tupu. Kila mtu anaweza kupewa kitu kidogo ili aseme kile ambacho hao wakubwa wanataka aseme.

Hayo ndio matatizo ya mitala, hata uwe fair namna gani bado huwezi kutoa haki sawa kwa kila mtu na matokeo yake ni ugomvi na chuki.

Nawashangaa watu wanaohangaika na mitala katika karne hii ya 21 iliyojaa matatizo ya kiuchumi na magonjwa. Ukombozi wetu unatakiwa uanzie majumbani kwetu na sio kwenye majukwaa ya siasa au JF.

Ukiona wabunge mpaka mawaziri na huenda hata marais wanahangaika na mitala, jua Afrika bado tuna safari ndefu sana kuelekea ukombozi wa kweli.
 
Bimkubwa,

Familia zote zinakuwa na msemaji mmoja ila tu katika mazingira ya TZ ukiingiza siasa na umaskini ni balaa tupu. Kila mtu anaweza kupewa kitu kidogo ili aseme kile ambacho hao wakubwa wanataka aseme.

Hayo ndio matatizo ya mitala, hata uwe fair namna gani bado huwezi kutoa haki sawa kwa kila mtu na matokeo yake ni ugomvi na chuki.

Nawashangaa watu wanaohangaika na mitala katika karne hii ya 21 iliyojaa matatizo ya kiuchumi na magonjwa. Ukombozi wetu unatakiwa uanzie majumbani kwetu na sio kwenye majukwaa ya siasa au JF.

Ukiona wabunge mpaka mawaziri na huenda hata marais wanahangaika na mitala, jua Afrika bado tuna safari ndefu sana kuelekea ukombozi wa kweli.

Tararibu ile rangi ya familia ya Chacha, na yeye mwenyewe niliyoiandika kabla hajafariki inaanza kujionyesha.

Na ipo siku ile mitala ya kisiasa ya kuwa CHADEMA na kufanya kazi na wakina Rostam na Makamba kuibomoa CHADEMA baada tu ya kupata ndoto na matumaini ya kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho nayo itajitokeza.

Marehemu alikuwa mtu mwenye msimamo sana hasa katika kuyafuata madaraka. Alikuwa yuko tayari kufanya chochote na kushirikiana na yoyote ili mradi ndoto zake za kupanda kimamlaka ziweze kutimia. Alikuwa hatazami madhara kwa chama chake wala kwa watu wake wa karibu akiamini kila kitu kitajirekerekebisha mbele kwa mbele.

Tunamjadili sana marehemu Mwalimu Nyerere lakini wengine tukianza kuwajadili marehemu wengine huwa tunashambuliwa sana. Kwetu sisi waandishi wa habari za uchambuzi kushambuliwa huko tunaona ni sehemu tu ya kazi yetu.

Bado nasubiria kwa hamu nipate namba ya yule mwarabu wa Tabora aliyeachwa na Mariam baada ya kuzaa naye watoto wawili na kufilisika. Nataka kuthibitisha kauli kuhusu Sitta kabla ya kuandika chochote.

Pia kama kuna mwenye namba ya Mke wa Kwanza wa Chacha, anayeitwa Ghatti aliyezaa naye watoto wakubwa zaidi. Huyu anaweza kutusaidia mengi.

Mary bado ni mwendelezo wa mikakati ile ile maana sio tumbo moja na Chacha, huyu ni dada upande wa Keba ambaye yupo kwenye jukwaa la CCM hivi sasa.

Hakika hili sakata kila siku linakuwa kama sinema.

Hivi ripoti ya Jukwaa la Wahariri hakuna mwenye nakala yake?


PM
 
Bimkubwa,

Familia zote zinakuwa na msemaji mmoja ila tu katika mazingira ya TZ ukiingiza siasa na umaskini ni balaa tupu. Kila mtu anaweza kupewa kitu kidogo ili aseme kile ambacho hao wakubwa wanataka aseme.

Hayo ndio matatizo ya mitala, hata uwe fair namna gani bado huwezi kutoa haki sawa kwa kila mtu na matokeo yake ni ugomvi na chuki.

Nawashangaa watu wanaohangaika na mitala katika karne hii ya 21 iliyojaa matatizo ya kiuchumi na magonjwa. Ukombozi wetu unatakiwa uanzie majumbani kwetu na sio kwenye majukwaa ya siasa au JF.

Ukiona wabunge mpaka mawaziri na huenda hata marais wanahangaika na mitala, jua Afrika bado tuna safari ndefu sana kuelekea ukombozi wa kweli.


Kudus Mzee, your absolutely right...safari ni ndefu sana Africa, ushirikina, uzinzi and the like....
 
Tararibu ile rangi ya familia ya Chacha, na yeye mwenyewe niliyoiandika kabla hajafariki inaanza kujionyesha.

Na ipo siku ile mitala ya kisiasa ya kuwa CHADEMA na kufanya kazi na wakina Rostam na Makamba kuibomoa CHADEMA baada tu ya kupata ndoto na matumaini ya kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho nayo itajitokeza.

Marehemu alikuwa mtu mwenye msimamo sana hasa katika kuyafuata madaraka. Alikuwa yuko tayari kufanya chochote na kushirikiana na yoyote ili mradi ndoto zake za kupanda kimamlaka ziweze kutimia. Alikuwa hatazami madhara kwa chama chake wala kwa watu wake wa karibu akiamini kila kitu kitajirekerekebisha mbele kwa mbele.

Tunamjadili sana marehemu Mwalimu Nyerere lakini wengine tukianza kuwajadili marehemu wengine huwa tunashambuliwa sana. Kwetu sisi waandishi wa habari za uchambuzi kushambuliwa huko tunaona ni sehemu tu ya kazi yetu.

Bado nasubiria kwa hamu nipate namba ya yule mwarabu wa Tabora aliyeachwa na Mariam baada ya kuzaa naye watoto wawili na kufilisika. Nataka kuthibitisha kauli kuhusu Sitta kabla ya kuandika chochote.

Pia kama kuna mwenye namba ya Mke wa Kwanza wa Chacha, anayeitwa Ghatti aliyezaa naye watoto wakubwa zaidi. Huyu anaweza kutusaidia mengi.

Mary bado ni mwendelezo wa mikakati ile ile maana sio tumbo moja na Chacha, huyu ni dada upande wa Keba ambaye yupo kwenye jukwaa la CCM hivi sasa.

Hakika hili sakata kila siku linakuwa kama sinema.

Hivi ripoti ya Jukwaa la Wahariri hakuna mwenye nakala yake?


PM

PM,

Nimekusikia mkuu, ila mimi sipendi waandishi wa habari hasa pale wanapoingilia mambo ya ndani ya familia na kuwa tayari kuvuruga vuruga (The SUN type). Kwi kwi kwi!!!

Mwacheni huyo bi mkubwa wa Wangwe maana inaelekea anajiheshimu mno. Msije mkamshawishi kwa vijisenti na yeye akaishia kujianika wazi kweupe.

Sawa tunaandika hapa na kusoma na kucheka lakini hao ni watu kama sisi ambao wana uchungu wa kupotelewa na mpenzi wao.

Wote ni guilty kwenye hili kuanzia nyie waandishi wa habari mpaka sisi akina Mtanzania tunaosoma na kuchangia.

Inasikitisha jinsi familia moja inavyoweza kuwa kwenye media kwa muda mrefu kwa faida ya makundi mbalimbali. Losers wakubwa hapa ni hiyo familia yenyewe. Prof. Wangwe inatakiwa awe na busara zaidi na kuhakikisha anaondoa mambo ya familia yake kwenye siasa na media. Ikibidi hata awapige stop wote kuongea na media mpaka baada ya uchaguzi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom