Marine is a stouge hana elimu hana uwezo hana ujuzi, kinachoniudhi ni hivi vyama vya utetezi wa demokrasia kwa nini havifanyi lolote? kwa sababu hili tu linatosha kuweka malalamiko na kudai Marine na Tido wake wote wasimamishwe kazi tuone kama atakwenda kula Ikulu kwa kikwete, pili Media Council of Tanzania inafanya nini? yaani nchi nzima hakuna mwenye maamuzi watu tumelogwa na nani? hii kusema tu haitusaidii na lazima vyama vya upinzani waweke watu wao wakina Tundu Lisu wanasheria wasiotaka mchezo wa deal na huu uchafu wa huko TBC kwa nin kodi zetu zichezewe hivyo? Juzi wananchi wa kenya wametoka barabarani kukataa upumbavu wa wabunge wao kujiongezea mshahara sisi tunafanywa kitu cha ajabu tunaona sawa tuna nini jamani? its very frustrating, wasomi wako wapi? wanafunzi wa vyuo wako busy kujikomba na sasa mpaka wanamuda wa kushindana kwa urembo hivi urembo ndio kazi ya vyuo vyetu vikuu siku hizi sio talents? Siamini kabisa kwamba huko ndiko tulikofika halafu tunataka kushindana na wakenya walio serious nakwamba watanzania na wanafunzi wa mbio za kampeni, u miss na mashindano ya pool ya safari larger, watasoma mpaka wapate Phd lakini wataishi kuajiriwa kama ma clearners na primary school leavers wa kenya, uganda, somalia n.k huwezi kupanda upuuzi ukategemea kuvuna maisha bora. Hizo ndio products za shule za kata