Nakumbuka nikiwa darasa la 5 mwaka 1999 alikuja ticha mmoja kutufundisha hesabu sasa kimbembe kikawa kwenye mtihani wa kumaliza mhula wa mwisho. Mimi nilipata 18/100, yaan 9/50. Mtu wa kwanza ambae ni mdogo wake alipata 72, yaan 36. Watu tulidata ila baada ya pale nilienda twisheni kwake, nikaanza kuigonga hesabu vizuri. Ticha Braison uliekuwa Buzuruga ubarikiwe sana kunifanya nikafaulu shule ya msingi. Ila nilipokuja sekondari kikawa kisanga kingine tena eeeh