...Correction mkuu, aliimba nyimbo moja tu kwenye album nzima na bila ubishi ndiyo iliyokuwa hit na ilisimama vilivyo, i used to criticize it as well ila si mbaya kihivyo, producer wa Album alikuwa Stephen Marley.
Ahhh,
Wee Tupac, afadhali ulinganishe Bob Marley na Jimmy Cliff nani zaidi. Wote walikuwa na sauti nzuri sana. Hapo ndipo twaweza kuwalinganisha. Tosh na Bob labda kuwalinganisha kwenye mambo kupigania Uhuru kuwa nani alikuwa mpiganaji zaidi.
Wote walifanya kazi nzuri sana. Pia msisahau kuwa Bob alisaidia sana na Lee Scratch Perry. Huyu Mzee sijui vipi maan sasa hivi anaishi Switzland na huko sasa anajaribia kuchanganya Reggae na mziki wa electronics (techno). Huo mchanyato heri uutafute mwenyewe uusikilize maana unashindwa kumuweka kundi gani.
....Du mkuu mbona una hasira na mimi, anyway siwezi kumlinganisha Marley na Cliff hata siku moja, Papa na Samaki unaweza kuwalinganisha? Come on? Be realistic for a change man, Jimmy Cliff anaimba hadi hii leo na Bob Marley ameacha kuimba tokea September, 23 1980. Na hadi leo huwezi kuwalinganisha, simply because Marley hapingiki na hazuiliki mbele ya Cliff.
Hata hivyo, bila Cliff nadhani Wailers wote watatu wangekuwa tu historia, unajua kwa nini? Cliff alikuwa juu kabla ya wao na kitendo alichomfanyia Producer Blackwell ndicho kilichomgharimu umaarufu na commercial success to a limited extent I must say. Check movie the harder they come na ujue nani aligharamia movie nzima na kuifanyia promotion na in return alipata nini as thanks!!
Pia Lee Perry na technologia yake sijui unaileta hapa ya nini, unaijua Black Ark wewe? Msome Lee Perry ujue alivyokuwa mwehu ndio uelewe.
Still, Marley na Tosh nani zaidi, pse do not deviate from the point(s)
Peace,
Killuminati, the Don
Mzee, naona ulinielewa vibaya. Sijaandika kwa hasira na wala sikuwa na nia ya kuandika kwa hasira. Ni katika kutoa tu mawazo yangu.
Juu ya Perry nilikuwa nasema kuwa Bob alisaidiwa na producer wengi na mmoja wao ni huyo miaka hiyo ya nyuma. Hiyo Black ark si ilikuwa studio yake anayodai aliichoma? Anyway achana naye ingawa bado ni muhimu.
Ukija kwa Chriss Blackwell na Island Record yake, ni kuwa huyu jamaa aliwaachia akina Bob studio yake, wawe wanaingia na kutoka anytime wakitaka. Hii iliwapa ari kubwa na nguvu kubwa kufanya vitu vya maana ukichukulia kuwa mwanzo Dodd aliwatia ndani hela zao.
Blackwell alikuwa mfanya biashara mwenye roho nzuri. Hakutaka kukamuwa watu hadi mifupa. Aliwapa na wao kidogo ili wawe na nguvu ya kuzalisha zaidi. Kama Bob, na yeye alikuwa Mu-Irish. Nafikiri hii ndiyo iliwagombanisha Bob na wenzake kwani walifikiri jamaa kawazika ila kwa maoni yangu ni kuwa walitumia jina la Bob (Irish) ili KUUZA album na huku pesa wakigawa kama walivyokubaliana. Jamaa wakawa na donge kuwa Bob kawazika na Bob akiwa na donge la kupakaziwa.
Juu ya Cliff na Blackwell, uko sawa kabisa mkuu. Na kama nilivyosema, jamaa alikuwa mfanya biashara, akiuma hapa na kupuliza pale. Ila ukweli unabaki palepale kuwa bila Blackwell, Mziki wa Reggae sijui kama ungelipata umaarufu huo. Jamaa ameutangaza si kawaida na hasa kwa kutumia studio lake la Island.
Nafikiri mwisho wa siku, inategemea masikio yako yamempenda nani. Mie ukweli ni mpenzi wa Tosh na the same reason nampenda Dube (copy ya Tosh). Bob sauti yake si mbaya na wala si nzuri ila QUALITY ya mziki (instruments) kwenye nyimbo za Bob hasa zile za mwisho kwa kweli INATISHA SANA. Ukiwa kwenye sehemu na chombo kikali, vynil ya Bob inacheza kwenye technics na spiker zinakwenda around 20Hz-20,000Hzs, kwa kweli utaona raha ya Mziki. Bob album zake alikuwa akifyatulia Jamaica ambako sijui kwa nini wana quality nzuri wakati Tosh alikuwa akifyatulia USA (baadhi ya album). Hivyo hata mie mwisho wa siku hujikuta nawapenda wote ila IN GENERAL, zaidi naelema kwa TOSH.
mimi binafsi BOB MARLEY yuko juu kwa sababu ukisikiliza nyimbo zake unaelimika,unaburudika nyimbo zake ni za ukweli man,
Hivi unafikiri TOSH haelimishi? Unajua nchi nyingi na hata Tanzania kwa sasa tunalia RA, Ufisadi, vyama vingi nk. Tunasahau msingi wa tatizo au matatizo yetu ni kuwa kuna watu wamejifanya miungu watu. Yeye anasema nini cha kufanya na kutoa onyo kwa hao ma-PRESSOR MAN.
Hebu sikiliza huu wimbo na huu ni ujumbe mzito kwa Mafisadi wote. You can run but you cant hide...... Rostam, Mkapa, Mramba, Makamba, Kingunge, Mgonja, Liyumba, Manji, Chenge, Mahalu, Mahita, Zombe nk.
True mkuu Sikonge, Tosh yupo juu, tofauti yao kubwa nadhani ni kuwa wakati Marley anasema kuwa Naomba haki yangu, Tosh yeye huwa anasema Nipe haki yangu, jamaa ni tough na amepetia misukosuko mpaka anakwenda kaburini.
Sikiliza nyimbo yake iitwayo Fool die for Wisdom , yaani imetulia ni kama vision fulani ya Redemption Song. For real jamaa anajua kutunga nyimbo zenye mafundisho na inabidi ku-read between the lines to understand him.
Tupo Pamoja.
Killuminati, The Don.
kina Tosh wamatumbi kabisa!
Hivyo albam yao badala ya kuiita The wailers tu, BBC wakaiita Bob Marley & wailers kama hila ya kumbeba mzungu mwenzao Bob na Bob aliifurahia hii.... Hii kitu ilimuuma sana Tosh na kumwona Bob kama msaliti mkubwa na ambaye hata umaarufu wake unasambazwa sana kwakuwa anadamu ya kizungu!
Ehh, bwana wee, hiyo nyimbo huwa ninaizimia sana. Ni safi sana kama ndiyo unataka kulala maana kimziki kama vile hakitaki. Iko kwenye album ya Wanted dread or alive kama sikosei maana hapa kwangu CDs zimepile hadi wakati mwingine naona heri kusikiliza kwenye YOUTUBE maana ni karibu.
Ukikaa sana unaona kama vile hata 2Pac alikuwa mpenzi wa Tosh. Sijui kama ni kweli au basi ilitokea kibahati bahati. Tupac alikuwa Soldier na Tosh ndiyo anaimba kwenye wimbo wake kuwa Recruting soldiers. Anyway mie nyumbani kwetu tu wapenzi zaidi wa album ya Misctic man. Miaka ileee tulikuwa tunasikiliza cassete hadi unaihurumia.
Jamaa alikuwa ananiuwa tu na hili gitaa lake. Ukorofi wa 2pac na jamaa unaweza kuuweka kapu moja.....
NB: Hivi kwa wazee wa sasa, mkali ni nani? Gregory kashajichokea na unga wake. Vipi Mzee Buring Spear? Huyu naye namzimia sana na sababu ni ileile kama Bob, mziki wake ni mkali sana (instruments).