Nadhani unayo hoja ya msingi kabisa. Ila kukufumbua macho zaidi ni vema ukafahamu kuwa ndoa haijawai wala haitawahi kuja kuwa outdated concept bali shida ni wahusika wanaoingia ndani ya ndoa kutokuwa na vigezo au uwezo wa kusimama ndani ya ndoa.
Kuna sababu ambazo kimsingi zinasababisha ndoa katika kizazi cha sasa kuwa kazi kubwa kuitumikia, na sababu zenyewe ni kama ifuatavyo:
1. Ndoa ni taasisi, na kila taasisi ndani yake ina watendaji wenye vigezo na uwezo wa kuitumikia. Huwezi kuajiri askari jeshi bila mafunzo ya jeshi. Huwezi ajiri muhasibu bila kufuzu mafunzo ya chuo na CPA, huwezi ajiri mkemia bila kuwa na cheti cha mkemia, je kwenye ndoa, hawa mabinti wa kisasa na vijana ni wapi hukaa kambi hata ya mwaka m'moja kupitia mafunzo makali ya ndoa?
2. Wanaume wameshusha sana standards zao kwa wanawake na wanawake wamepandisha sana standards zao kwa wanaume. Mwanamke zamani aliqualify kuwa mke kwa kuwa bikra kama sifa ya lazima, halafu tabia nzuri ikawekwa kama sifa inayofuata ya lazima.
Leo hii wanaume hii sifa hamuhangaiki nayo tena wanaume wengine wanatetea kabisa kwa kusema kwan kuna ubaya gani akiwa hana bikra, hawa ni wanaume wanaotetea si wanawake, sasa kwann wanawake wasikubaliane na huo uhalisia kuwa wanaume hawana shida na bikra watatuoa hata wakikuta tulishazaa na wanaume kwahiyo wacha tukachezewe kuna mabwege yatatulipia mahari na kutuoa.
3. Wanaume miaka hii wamekuwa wakwepa majukumu au wabeba majukumu yasiyowahusu. Mwanaume anazaa na binti ila hajui wajibu wake kama Mume na baba, hajui majukumu yake kwa kitu alichokianzisha mwenyewe anatoa toa macho kama ng'ombe na kusubiria wakwe, mashemeji, na familia yake wafanye jambo kumsaidia. Au anakutana na mwanamke ambaye sio wake ana watoto yeye huyo kabebelea, ni wa kwako? Kwann usitafute wa kwako? Hiyo roho nzuri si ungelea watoto wa dungu zako wenye hali ngumu, kwenda kulea mabao ya watu halafu ndio uitwe mwanaume wa shoka ni ujinga kutoka sayari gani huo? [emoji848] Kwa sampuli hii ya wanaume ndoa haiwezi kuwa imara.
4. Kudharau mafunzo ya kimaadili na Maagizo ya mwenyezi MUNGU ambayo kaagiza watu kuyafuata ili kuwa imara kiimani na kimwili ila viburi sasa vya wanadamu leo ndio matokeo yake tupo hapa ndoa zinaendeshwa kwa idea za movies za Hollywood, tamthiria za Telemundo, na hawa relationship coaches wa mitandaoni.
5. Wanawake wa sasa ni wavivu eneo la ndoa ila wanabidii kujihangaikia. Mwanamke unaweza mkuta alikuwa amepanga analipa Kodi kwa biashara ndogo ndogo au ameajiriwa lakini siku ukianza kaa nae ndani hatochangia hata 1000 endapo kutakuwa na dharula na mwanaume haupo karibu au haupo na vema kiuchumi kwa kukwambia wewe ni mwanaume as if yeye ndie huwa analipa 100% ya bills. Kwa kifupi ubinafsi.
So kimsingi Ndoa haijawai na haitakuja kuwa outdated concept shida ni wahusika kutokutambua na kusimamia vigezo vya ndoa na kuisimamia vilivyo kwa kila mojawapo kukaa eneo lake na si kuingiliana.
Mkuu hapo kwenye point yako namba mbili nafikiri umesahau kitu kimoja tu, hiyo zamani wakati sifa za mwanamke kuolewa zilikuwa ni bikira na tabia njema zilikuwa ni enzi ambazo wanaume hawatongozi wanawake hovyo ili wapunguze tu upwiru, bali mwanaume alikuwa akimpenda mwanamke anaenda direct kwao kumchumbia na kumtolea mahari kisha anapewa mke wanaanza maisha ya ndoa
Lakini kwa hii dunia ya leo ambayo watu wamefanya ngono kama chakula mahusiano yanajengwa based on one night stand, friends with benefit, kufurahishana, kulana kimasihara, na upumbavu mwingine kama huo, watu wanajifanyia tu sex halafu mwisho wa siku mwanaume akitaka kuoa, aje aseme eti anataka bikira na tabia njema huyo atakuwa mzima kweli kichwani
Na mbaya zaidi ukisema jinsia zote zibadilike wanaume wanakuambia eti wanaotakiwa kubadilika ni wanawake ndio waache kukubali wakitongozwa, ila wao wanaume wanaona ni haki yao kutongoza wanawake hata wasio na malengo nao kwa gia ya kwamba watawaoa kumbe lengo lao ni kupunguza haja zao tu, yani eti wao kuwahadaa wanawake wanajiona wako sawa na wanafaa kuwa waume ila wanawake kuwakubalia wanaonekana wana matatizo na hawafai kuwa wake
Yani mtu urukeruke huku na huko ufanye umalaya uchezee na uharibu wanawake to your heart's content halafu ukitaka kuoa, ndio uje ujifanye unawalalamikia na kuwatukana wanawake kuwa hawajitunzi na hawajiheshimu kana kwamba siyo wewe uliyeshiriki kwenye kuwaharibu na kuwachezea, huku ukidhani kwamba jinsia yako itakubeba kwa kuwa unajua kwamba siku zote wanaodhalilishwa kuhusu suala la ngono ni wanawake kwa sana
Mimi ninachoweza kusema ni kwamba hao wanaume walioamua kushusha standards siyo kwamba ni wapumbavu ila wameamua kuacha kuwa delusional na kukubaliana na hali halisi, kwamba huwezi kuzini na wanawake halafu ukitaka kuoa uanze kutafuta mabikira katika hao hao wanawake ambao ulikuwa unazini nao sasa hao mabikira watoke wapi, huwezi kuyachafua mazingira halafu utegemee yakupe hewa safi lazima uchague moja ni either uyatunze mazingira ili yakupe hewa safi au uyachafue kisha uikubali hewa chafu yatakayokupa
Yani wanaume mnatakiwa muelewe kwamba kujitunza is not about nani anaonekana malaya na anadharaulika na jamii kati ya hizi jinsia mbili bali it's all about kupata mwenza bora wa maisha, maana hapa tulipofikia wanawake hawajali tena na wameshaanza kuzipuuzia hizo gender stereotypes na ndio kwanza wanazidisha maovu na huko tunakoelekea ndio kubaya zaidi, so it's up to you wanaume kuamua either mbadilike muache kuchezea na kuharibu wanawake au muendelee halafu mwisho wa siku mje kuoa hao hao maana ndio ambao wapo wala msidhani mtashushiwa hao mabikira mnaowataka
Ni kwa sababu imeshaonekana kwamba wenye shida na hizo bikira na tabia njema kutoka kwa wanawake ni ninyi na siyo wao wenyewe so ninyi kama ninyi mnafanya jitihada gani ili mfike nao wakiwa na hizo sifa hadi kwenye umri wa ndoa, kama bado mtaendelea kushindana nao kwamba wao ndio wajitunze kwa visingizio vya kipumbavu eti maumbile sijui nini basi msitegemee lolote na wala msiwalaumu pale ambapo mnataka kuoa bali mkubali tu kushusha vigezo vyenu na kuvuna mlichokipanda, tangu jamii imeanza kuwatukana wanawake matusi na kuwaita majina yote mabaya kama wanawake wangekuwa wanajali basi wangeshaanza kubadilika lakini matokeo yake ndio kwanza wanazidisha tabia za hovyo so my point is wanaume mkiona mnaumizwa na mnachukizwa na umalaya na ukahaba wa wanawake basi chagueni moja either anzeni ninyi kubadilika au la hamuwezi basi kubalianeni na hali halisi