Waungwana,
Marshall plan ya Mchungaji si "Fikra za Mwenyekiti" ambazo zilikuwa absolute and omnipotent.
Marshall plan hii ni kutoa changamoto kwetu sisi ambao ndio Taifa la sasa kujikimu na kujikwamua ili Watoto, Wajukuu, Vijukuu na zao 7 baada yetu wanufaike kwa matunda ya msingi bora tulioujenga.
Ndiyo nimekuwa pioneer hapa ndani lakini haina maana kuwa ninachoandika na kufikiri ni changu pekee.
Marshall Plan ya Mchungaji ni yetu sote na kama frame work na blue print ndiyo nimeanzisha, details and specifics zinahitajika kwa kila mtu. Anzia kina Bin Maryam waliopotea, Kahangwa, Nyambala, Richard, Mwanakijiji, Mpaka Kieleweke, Kada Mpinzani, FMES, Kuhani, JMushi, Madela wa Madilu, Susuviri, Koba, Game Theory, Kibunango, Steve D, Nyani Ngabu, Mkandara, Jasusi, Mpanda Merikebu, Bi Kirembwe, Mama, Asha Abdallah, YNIM, na wengine wote, hii ni kazi ya Ushirika na ni jukumu letu wote kuchangia na kuunda Marshall Plan ya Tanzania.
Ikiwa CCM, CUF, Chadema, TLP na Watanzania kwa ujumla wataona Marshall Plan yetu ndiyo njia ya kweli kujikwamua kutoka Umasikini, ndiyo iwe faraja yetu.
Kitu kimoja ambacho JF member wengi hawakijui na wanakipuuzia ni ile fursa kubwa tuliyonayo katika kulijenga Taifa letu.
We have the greatest opportunity to have solid and massive contribution to our country future.
Si suala la kupiga vita ufisadi tuu, bali inabidi tuanze kutoa solutions na njia bora za kutatua matatizo yetu ili future generation za Tanzania, zisiinshie kwenye Unyonge.
The time is now for us to work collectivelly. We need people to brainstorm to offer solutions and not always think how to criticise.
Challenge aliyotupa Allien, nimeichukua moyoni kwa kuwa nimeshalaumu sana, next thing ni kuanza kutoa njia za kusahihisha.
Sitegemei kuwa ninachoandika ni infinite na final, kila mmoja wetu anajukumu la kuingia na kuchangia, kujenga Taifa letu bila kujali tofaui zetu.
Adui wetu si wa Chadema pekee, ni wa CCM wenyewe, TLP, CUF na hata wale ambao hawana Chama.
So join me in the struggle and offer simple and workable solutions!