'Marshall Plan' - Restoration and Recovery Plan for Tanzania

Mkuu katika kipengele hiuki nadhani ipo haja ya kuelezea vizuri unapozungumzia NYUIMBA.. kwa sbaabu serikali inaweza kuwa na majumba kwa malengo ya HUDUMA sio BIASHARA..
Nina hakika hakuna nchi duniani ambayo serikali yake haina nyumba hata iwe zile tunazoziita PROJECT!.. yaani kuwasaidia wananchi wasiokuwa na uwezo wa kununua ama kupangisha nyumba ktk bei za soko.
 

Hapa alikuwa anaongelea nyumba za kuishi viongozi na watumishi wa ngazi za juu, sio project wala mafleti ya Ubungo National Housing au Magomeni Quarters!

Anasema Serikali isiendelee kuwa na nyumba za viongozi.

Sasa sijui kama anakubaliana na uamuzi wa Mkapa administration kuuza nyumba za Serikali. Mimi nadhani ulikuwa sawa, japo utekelezaji wake ulikuwa wa kifisadi.
 

Right on money Kuhani!
 
Nakushukuru mchungaji,
Najua umefanya kazi kubwa sana katika kuandika ujumbe huu kwetu,kwa hakika ujumbe umejitoreza.Mie naomba nishauri kitu kimoja,UJUMBE HUU UTUMWE KATIKA MAGAZETI YOTE YA HAPA BONGO KAMA MAKALA ILI NA WATANZANIA WENGINE WAWEZE KUUSOMA.NAAMINI TUKIFANYA HIVI VITA YETU ITAKUWA IMEFIKA MBALI ZAIDI.

UBARIKIWE SANA MCHUNGAJI NA BWANA AKUWEZESHE KWA MARA YA TENA.
 

Bibi Ntilie,

Shikamoo Bibi! Nashukuru kwa maneno mazito na ya kuhamasisha. Naomba ufungue kiambatanisho, kipige chapa uende ukajisomee mwenyewe ukipata chai na kashata halafu tafakari yule Mzee wetu angesemaje?

Kugombea sitagombea, kama nilivyowaambia kwenye ile thread ya Mwanitafuta ni mimi.. https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=14476 lakini sitakaa kimya, nafurahia uhuru wa kupembua na kuchangua mambo.

Uongozi si lelemama, ni kazi kubwa na nzito, ndiyo maana nilitamka wazi mapema miaka 4 iliyopita kuwa ifikapo 2025, nitakuwa tayari kuajiriwa na John Mnyika au January Makamba kama mwendesha kampeni na mshauri wa mambo ya siasa.

Naona wote Mnyika na January bado wanajifunza, hivyo huduma zangu ziko wazi kwa yule mwenye nia ya kulijenga Taifa na si kujenga Chama!

Hata ndugu yangu Zitto na Kitila nimewaambia, nitasaidiana nao. Kama kuna mwenye kumjua Nape au Zainabu wa Kawawa, kama nia yao ni kulijenga Taifa, waambieni wawasiliane na Mchungaji!
 
Waungwana,

Najua nimeandika kwa kirefu mawazo yangu na kuyawasilisha hapa kwenu ili muyachambue. Jambo moja, la muhimu ni hili, hakuna mpango wowote utakaoweza kufanikiwa kama uongozi na watendaji ni wabovu!

Hata kama hiyo master plan, manifesto au Marshall plan italetwa na Muumba mwenyewe, ikiwa tuna viongozi wabovu, kamwe tusitegemee kuona yaliyoandikwa na kupangwa yakitimilika.

Uongozi si mtu mmoja tuu, kosa lililotokea na Mwalimu Nyerere na mambo ya Azimio, Vijiji vya Ujamaa na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea.

Waliokuwa upande mmoja na Mwalimu walikuwa wachache sana. Wengi walikuwa ni wafuata mkumbu huko nyoyo zao zilikuwa zinasubiri nafasi ya kutanua kama walivyoona wale mabwana DC wa Kizungu wakitanua na kujichana.

Tutakapo kuwa na viongozi wa kutosha wenye mwamko na changamoto la kuleta maendeleo, basi Taifa letu litapiga hatua. Kinyume na hivyo ni sawa na mbwa kutaka kung'ata mkia wake!
 
Rev Kishoka,

Marekebisho yangu ya kwanza mbali na hotuba iliyotangulia mkuu ambayo imeniacha HOI...(laukamam ungekuwa mgombea Urais basi mkuu kura yangu umeipata).. Ni haya hapa:-

Nimeanza na ELIMU nafikiri ni kosa la kimaandishi tu... sehemu nilizo highlight ndio marekebisho yenyewe:-

Katika mpango wangu, kila Wilaya itapaswa kuwa na Shule si chini ya mbili za Sekondari (kidato cha Nne) na chuo cha ufundi ambazo zitakuwa chini ya mamlaka za Tamisemi. Kila mkoa utapaswa kuwa na shule za sekondari ya elimu ya juu (kidato cha Sita) si chini ya 4, Vyuo vya ualimu, uuguzi na utabibu, kilimo, uvuvi na mifugo, , biashara na uhasibu, ufundi (mithili ya Dar Tec), sanaa utamaduni na michezo kwa kila mkoa kulingana na idadi ya wakazi wake.

Katika elimu ya juu ya kiwango cha Chuo kikuu, msukumo utakuwa wa kuwa na chuo kikuu kwa kila mkoa ifikapo mwaka 2050. Tukianza na majimbo makuu manane ( yatakayoundwa. Katika hili, uchochezi wa kupanuka kwa sekta hii kilimo utajumuisha watu binafsi, taasisi za kidini na jumuiya za maendeleo za mikoa.
 
Mchungaji,
Nimeufuatilia huu mpango wetu, na napenda kukupongeza sana kwa kazi kubwa uliyoifanya. Ila napenda kuungana na Mkamap kuwa tatizo letu Tanzania siyo mpango wala sera, kwani hata nchi za jirani zetu wanatumia mipango yetu na sera zetu and they are making. Tukumbuke kuwa watekelezaji wa mipango hii ni watanzania walewale waliodanganywa kuanzia miaka 45 iliyopita, ambao wameshazoea kuona mipango mingi. Tunachokosa ni uongozi wenye nia ya dhati ya kutekeleza mipango mingi tuliyonayo. Ni matumaini yangu kuwa katika mpango huu, ungetanguliwa na mpango kabambe wa kuwaandaa watanzania kwanza kuwa wazalendo, wazifahamu haki zao, mipango ya maendeleo yao, aina na wajibu wa viongozi wanaowachagua ili kuleta maendeleo yao na kipimo cha kujua kiongozi anayefaa. Naamini kuwa tatizo si mipango wala sera, tatizo ni watanzania tumeshindwa kuleta viongozi wanaoweza kusimamia utekelezaji wa mipango na sera zetu. Tuandae mpango wa kuwaandaa watanzania kuchagua viongozi wanaofaa watakaotuongoza kuleta mabadiliko
 
Kinto,
Mkuu samahani umesema kinachotuangusha sio sera ila ni Uongozi...Mkuu hivi utawapata vipi Viongozi bora ikiwa mwenyewe huna Malengo..Huna plan ya kule unakotaka kwenda huyu rubani ama nahodha atawafikisha vipii?.. Huo Uongozi bora utapimwa kwa kutumia vigezo gani.. nadhani hiii ndio hoja kubwa ya Rev Kishoka. Kwanza tupange malengo yetu sisi wananchi hizo sera za vyama zibakie kama zilivyo wakiongozwa na malengo yetu.
Nafikiri Ukisoma kwa makini utangulizi wa Rev. umejieleza wazi majukumu yetu sote na amesisitiza sana majukumu ya wananchi na viongozi jambo ambalo litafanya kazi tu ikiwa malengo tayari yapo wazi...
Binafsi yangu ningekuombeni kwanza tuyatazame mapendekezo ya Rev. Kishoka tuongeze ama tupunguze ilimradi tuwe na dira kisha tukishajipanga sawa hapo ndipo unamtafuta Chama ama Kiongozi anayeweza kutufikisha tunakokusudia...

Ebu wewe nambie ni sera gani Kitaifa ambazo majirani wetu wanazifuata?... Na zipi hizo maanake nijuavyo mimi Tanzania ni Meli isiyokuwa na sio tu Nahodha bali hatufahamu tunakokwenda zaidi ya kuwa na fununu kuwa huko ktk nchi ya Ughibuni kuna Pepo!..hatuna Malengo hiyo dira (sera) na Uongozi kweli tutafika!.
 
Bob Mkandara,

Shukrani kwa masahihisho. Nitarekebisha na kuainisha vyema.

Kinto,

Waraka huu unaanza kwa kumhoji Mtanzania, unamsukuma Mtanzania ajichunguze kwanza pamoja na kuwa matatizo makuu yanajulikana Uchumi na Uongozi.

Waraka unaendelea kumhiji Mtanzania ni maendeleo ya namna gani anayoyataka na kumuuliza matarajio wake.

Waraka unatoa tafrsiri rahisi kuhusu Uongozi bora, na kumrudia msomaji Mtanzania kumuuliza, je amefanya nini katika kutafuta kiongozi bora?

Waraka unahama kutoka kumuuliza Mtanzania kama anajijua na kuelewa umuhimu wa Uongozi na hasa Uongozi bora ili kuwa msukumo wa maendeleo na kuanza kupembua vigezo vya kumpa Mwananchi huyu maendeleo na hasa kujikwamua kibinafsi na kama Taifa kiuchumi.

Dhumuni la waraka si Sera, bali ni kumpa Mwananchi fursa ya kujiuliza afanyeje ili awe na maendeleo ya kweli na yale yanaoonekana kuwa ni Sera, ni mambo ya kawaida ambayo yalipaswa kufanyiwa kazi lakini hayafanyiwi kazi kutokana na Uongozi mbovu.

Mtanzania akishajua anachokitaka, na kuelewa kinachowezekana na kuamua kwa umakini Uongozi anaoutaka, safari ya maendeleo itafanikiwa.

Ndiyo maana Waraka huu ni kwa Mtanzania, si kwa Chama au Serikali.
 

Wakuu nawashukuru kwa darasa, najichimbia kidogo niendelee kuufanyia kazi waraka huu. Mchungaji, tuko pamoja.
 
Mcungaji,
Nashukuru sana kwa waraka wako.Naendelea kusoma ni mawazo mazuri sana.Leo ngoja nidokeze kidogo kuhusu magari ya serikali kwa kweli fleet hii ni kubwa inasumbua walipa kodi wa Tanzania.
Magari yote ya serikali yamilikiwe na TAMESA ambayo imejaza watalaamu wa machenics.Huko itakuwa rahisi kujua mda wa gari kwenda maintenance na control ya mafuta kwa kilometre iliyotembea.Madereva waajiriwe na taasisi hiyo na officer wa serikali anapotaka kusafiri Transport officer wa idara ya serikali afanye arrangement na taasisi hiyo na charge iwe raised baada ya safari.Hii hatua itawabana maofisa wa serikali wasiabuse matumizi ya magari ya serikali.Vilevile maofisa wa serikali wenye kustahili usafiri wakopeshwe magari.
Bado naendelea kuisoma na nitahakikisha napeleka copy Kyela vijijini nina jamaa yangu ana NGO ataitoa copy na kuelemisha wanavijiji.
 
Umenikumbusha tukio moja ilitokea kijiji cha Lugombo kata ya Ngonga, wananchi walimdai Diwani wao report ya mapato na matumizi ya kata.Badala ya kuwapa report hiyo yeye akatamka kuwa wale watu wametumwa na vyama vya upinzani,akafunga mkutano na kupanda pikipiki na mtendaji wa kata.Hiyo ndio hali ya uongozi ulivyo wa hovyo huko kyela.
 
Any updates wadau mliousoma waraka?

Mchungaji,
Napata shida sana kwani watu kama wewe wenye mitazamo mizuri hampati nafasi ktk utawala wa taifa letu, nchi yetu sasa inarithishwa kwa watoto waviongozi na si vinginevyo.

Mchungaji hapo nyuma ktk thread yangu( Mbowe jiuzulu ukinusulu chama) nimeshauri kuwa tupate kiongozi mwingine anayeweza kuendeleza kazi njema aliyoianzisha, la kushangaza wewe na vigogo wengine ktk forum hii mmekaa kimya, ama mmeiona ni mada hiyo ni tete au vipi.

Mchungaji
Mchango wako bado unaitajika ktk taifa letu

Mungu ibariki Tanzania
 
Mzalendo Rev. Kishoka; Good stuff. Nitapitia na kutoa maoni yangu nitakapokuwa tayari Mkuu.

The fact kwamba umechukua muda kufikiri na kuandika plan hii, inaonyesha ni jinsi gani umedhamria kutoa mchango wako katika kuleta maendeleo ya kweli.
 
 

Rev. Kishoka, there are two issues which I would like to share here. The first one is having the "Agricultural Incubators" and secondly "Agricultural Entrepreneurship Villages"

Despite existence of many opportunities for commercial agriculture in rural areas, the barriers are just too daunting for a significant change in commercialisation of agriculture to take place in the foreseeable future. There is need for an innovative scheme to make agriculture a viable option for graduates of colleges. This is not the case for the time being.

I would recommended we establish hybrid institutions to nurture and produce commercial farmers. The proposed scheme could work as follows. Public or private sector promoters would identify large tracks of accessible land suitable for pre-determined types of crops or livestock for which existence of adequate long-term demand will have to be ascertained.

On this land will be established teaching and accommodation facilities, where students cum incubatees will stay for a fixed term, while collectively opening up and working hard on farms. These institutions will develop and deliver agriculture, agribusiness and entrepreneurship training directly related to developing successful commercial farms in that context. Students will graduate with both a certificate and an operating farm business.

Qualified youngsters who have positively decided they want to develop a career as commercial farmers will apply for the scheme. In order for the cost to be manageable, students will be required to spend significant amount of time doing practical work (labouring).

Towards the end of their incubation/studies, students will be allocated pre-determined developed land where they will build their basic houses. The college/incubator will relocate to another area, leaving hundreds of people, each with a significant, productive piece of farm as a cluster.

The incubatees could organise themselves into a co-operative and or/SACCOs, even before the incubator relocates. The co-operative or association could buy off the common physical facilities (classrooms, etc) so that they become community assets (schools, supermarket, health centre, meeting rooms, etc) for the new farmers upon graduation.

Graduating incubatees may have the option of selling their farms to other people, or some farms so developed could be sold to interested retiring army or other retirees. The advantage of this mode is that many of the constraints are simultaneously addressed.

. . . . I will explain next on Entrepreneurship Villages Concept . . .
 
KILIMO

ENTREPRENEURSHIP VILLAGES

Why a Model Entrepreneurship Village?

Tanzania is among the poorest countries in the world of which more than 50% of its population live below the poverty line. The main cause of the poverty can be attributed to various reasons one of them being under production and under utilization of our country natural resources as well as human resources.

Tanzania is blessed with a very big and fertile land. More than 80% of the population lives in rural areas, Farming or Agriculture Employs more than 80% of the population. However lack of application of modern farming methods backed up with professional support still remains to be a big problem. Agriculture can still alleviate the poor life of Tanzanians if done properly. Because of lack of proper resources and gears in farming, there is now a very big influx of people migrating to the towns and cities from villages. One of these cities is Dar Es Salaam, the capital of Tanzania.

Even for the people who remain in villages for farming, they always do so in a small scale. Sometimes there is no reliable rainfall for the products they have planted and even if there is a good rainfall, the quantity and quality of the farm products are usually of poor standards which attract low prices in the local and International market and thus does not sustain or adequately cover the farmers' financial requirement.

I believe, Tanzanians can change their lives and alleviate the poverty by engaging themselves in modern, mechanized and technological farming backed up with professional support. To succeed in this, there is a need to establish Entrepreneurship Villages which will turn our human resources and natural resources to be utilized in a profitable way, thus improving lives of the target groups and reducing the poverty. The Government in collaboration with other stake holders can build these villages and people can join these villages after giving them proper training on how to live and work in these villages.

Entrepreneurship Villages are villages which can be established as a means of eliminating poverty in our society. About fifty simple and low cost houses can be built in the villages, the villages will have all the relevant infrastructure and facilities like, Schools, Hospitals, Community Centers, Police Posts, Business Centers, Workshop Houses, Play grounds, Bank(s), Postal, etc. People who will live in these villages will be given Special Training on Entrepreneurship Life, Modern Farming, Positive attitudes, how to succeed in life etc on regular basis as a way of sustaining the skills in the people's mind.

The selected people will be given the houses, and be supported for sometime. However, these residents will have one mission: To do farming in a modern way of making profit. Every one will be given a large farm to take care. There will be all modern facilities to support this farming like, Tractors, Irrigation, Boreholes, Fertilizers, packaging and proper Storage facilities, Pesticides and there will be a very well researched market for their farm produces which will surely be sold at profitable margins at the local or foreign markets.

These villages can be managed under Public Private partnership or can be run and managed by Private Entities etc . . .

Goosh . . . was it a dream ???!! Rev. Kishoka, yote yanawezekana sana kama tu kutakuwa na utashi wa kweli wa kuleta maendeleo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…