Pre GE2025 Martin: Wabunge wanalipwa posho zaidi ya TSh. Milioni 86 kwa siku Bungeni Dodoma. Ama kweli Siasa ni Mchongo!

Pre GE2025 Martin: Wabunge wanalipwa posho zaidi ya TSh. Milioni 86 kwa siku Bungeni Dodoma. Ama kweli Siasa ni Mchongo!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Anaandika Martin Maranja Masese, Mtikila

Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu, Mwanasheria mkuu wa serikali, Spika wa bunge, Naibu Spika wa bunge, Mawaziri na Wabunge wote, wanalipwa posho ya kujikimu (perdiem) kwa siku ni Sh220,000.

Jumla ya idadi yote ya wabunge ni 393. Wabunge wa majimbo ni 264. Wabunge wa viti maalum ni 113. Wabunge wa baraza la wawakilishi ni 5. Wabunge wa kuteuliwa na Rais ni 10. Mwanasheria Mkuu wa Serikali 1.

Jumla ya wabunge wote bungeni ni 393. Hivyo, jumla kwa siku moja Dodoma wanalipwa Sh86,460,000. Hizi ni fedha zenu. Hebu tazama hapo kwenu, kata zenu zina vituo vya afya? Visima? Barabara? Shule?

Kwa maoni yangu, katiba ieleze; fedha ya kujikimu inapaswa kutolewa kwa wabunge (ukiondoa mbunge wa Dodoma Mjini), kwa hoja kwamba makazi yao siyo Dodoma, wapo nje ya kituo cha kazi, jimboni.

Kwanini watu hawa hapo juu walipwe fedha za kujikimu (perdiem) Sh220,000 wakati serikali imewajengea makazi yenye huduma zote Dodoma? Makazi yao yana walinzi wanaolipwa na serikali. Kujikimu vipi?

Waziri Mkuu na Naibu Waziri Mkuu, Spika na Naibu Spika wa bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, wanastahili hayo malipo ya Sh220,000 kwa siku kwa ajili ya kujikimu wakiwa Dodoma? Kwanini wanastahili?

Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu, Mawaziri na Spika wa bunge na Naibu Spika wa bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali; vituo vyao vya kazi ni Dodoma (lilipo bunge la JMT). Serikali imewapa makazi Dodoma.

Je, watu hawa wanalipwa kwa sababu tu na wao ni wabunge kama wabunge wengine? Au kuna sababu nyingine? Kama hiyo ndio sababu ya msingi, Je, hii ni sahihi? Je, sio matumizi mabaya ya fedha za umma?

MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.

1738935630625.png


photo_2025-02-07_16-45-23.jpg
 
Ndiyo maana Trump ameamua kusitisha huduma kwa shithole countries
 
Nimesoma hili bandiko huko twitter. Nasema Trump bora tu akate misaada yote.

Binafsi niliwahi hoja jambo kama hili kupitia hapa JF mwaka 2022:


 
Nimesoma hili bandiko huko twitter. Nasema Trump bora tu akate misaada yote.

Binafsi niliwahi hoja jambo kama hili kupitia hapa JF:


😀 😀 ila kumbuka bado wananchi ndio tutakaoumia zaidi
 
Anaandika Martin Maranja Masese, Mtikila

Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu, Mwanasheria mkuu wa serikali, Spika wa bunge, Naibu Spika wa bunge, Mawaziri na Wabunge wote, wanalipwa posho ya kujikimu (perdiem) kwa siku ni Sh220,000.

Jumla ya idadi yote ya wabunge ni 393. Wabunge wa majimbo ni 264. Wabunge wa viti maalum ni 113. Wabunge wa baraza la wawakilishi ni 5. Wabunge wa kuteuliwa na Rais ni 10. Mwanasheria Mkuu wa Serikali 1.

Jumla ya wabunge wote bungeni ni 393. Hivyo, jumla kwa siku moja Dodoma wanalipwa Sh86,460,000. Hizi ni fedha zenu. Hebu tazama hapo kwenu, kata zenu zina vituo vya afya? Visima? Barabara? Shule?

Kwa maoni yangu, katiba ieleze; fedha ya kujikimu inapaswa kutolewa kwa wabunge (ukiondoa mbunge wa Dodoma Mjini), kwa hoja kwamba makazi yao siyo Dodoma, wapo nje ya kituo cha kazi, jimboni.

Kwanini watu hawa hapo juu walipwe fedha za kujikimu (perdiem) Sh220,000 wakati serikali imewajengea makazi yenye huduma zote Dodoma? Makazi yao yana walinzi wanaolipwa na serikali. Kujikimu vipi?

Waziri Mkuu na Naibu Waziri Mkuu, Spika na Naibu Spika wa bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, wanastahili hayo malipo ya Sh220,000 kwa siku kwa ajili ya kujikimu wakiwa Dodoma? Kwanini wanastahili?

Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu, Mawaziri na Spika wa bunge na Naibu Spika wa bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali; vituo vyao vya kazi ni Dodoma (lilipo bunge la JMT). Serikali imewapa makazi Dodoma.

Je, watu hawa wanalipwa kwa sababu tu na wao ni wabunge kama wabunge wengine? Au kuna sababu nyingine? Kama hiyo ndio sababu ya msingi, Je, hii ni sahihi? Je, sio matumizi mabaya ya fedha za umma?

MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.

Wanalipwa kama wawakilishi wa wananchi,ukitaka kujua hiyo nafasi ni tamu nenda kichwa kichwa jimbo lolote ujifanye na wewe unataka kugombea,sijui kama mwaka utaisha ukiwa mzima.....
 
Haya mambo hata wabunge wa upinzani walikuwa wanatetea.
 
Aisee jamaa wanakula parefu sana aisee 86 mil kwa siku dah!

Hii pesa ya siku moja inaweza kulipa walimu wa shule za msingi au clinical officers zaidi ya 100 kwa mwezi

HApo hiyo hela hata watanzania mfe njaa haiwez punguzwa labda mpaka tumwage damu
 
Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu, Mawaziri na Spika wa bunge na Naibu Spika wa bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali; vituo vyao vya kazi ni Dodoma (lilipo bunge la JMT). Serikali imewapa makazi Dodoma.

Je, watu hawa wanalipwa kwa sababu tu na wao ni wabunge kama wabunge wengine? Au kuna sababu nyingine? Kama hiyo ndio sababu ya msingi, Je, hii ni sahihi? Je, sio matumizi mabaya ya fedha za umma?

MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.
Huo ni ufisadi wa wazi dhidi ya wanyonge (aka walipa kodi)
 
Dodoma pesa ipo,twendeni dodoma

Hawa jamaa wanapopewa hii pesa lazima iingie mtaan siku hyo hyo
 
Zitto Kabwe alishawahi kukataa kuchukua posho kina Lema wakamdhihaki. Wapinzani wanapiga kelele kwa sababu wako nje ya bunge. Wakiingia humo hawawezi kutaka posho isiwepo. Hizo hela ndo wanachukulia mikopo mikubwa na kufanya mambo yao. Martin ni wa kupuuzwa. Ni mnafiki.
 
Wanalipwa kama wawakilishi wa wananchi,ukitaka kujua hiyo nafasi ni tamu nenda kichwa kichwa jimbo lolote ujifanye na wewe unataka kugombea,sijui kama mwaka utaisha ukiwa mzima.....
Kuna jimbo huko Lindi walikuwa wanatekwa na kufichwa kabisa kupisha mchakato
 
Hao wabunge, mawaziri ,manaibu waziri, mwanasheria wa serikali na spika pamoja na wasaidizi wake wanatakiwa watengewe 5% ya pato la taifa ili tupunguze upigaji wa namna hii.
 
Back
Top Bottom