Marudio ya mkutano wa Balozi Dkt Emmanueli Nchimbi alipozungumza na Waandishi wa Habari na Wahariri

Marudio ya mkutano wa Balozi Dkt Emmanueli Nchimbi alipozungumza na Waandishi wa Habari na Wahariri

Amepangua na kujibu maswali yote kwa ufasaha mpaka waandishi wa habari wakabaki wanashangaa tu.
Ni mjinga kiwango cha zezeta atakayetegemea uchunguzi huru na wa haki.
Kwani polisi ili wafanye uchunguzi wanategemea mpaka Rais atoe amri kuwa uchunguzi ufanyike?
Magari mengi ya abiria siku hizi yamewekewa CCTV CAMERA, unadhani hilo gari alilokuwa amepanda Ali Kibao liko chini ya kiwango mpaka likose CCTV CAMERA?
Unafikiri kama zilikuwepo CCTV CAMERA, watakosa kuzingoa kama walivyozingoa Dodoma kwenye makazi aliyokuwa anakaa Lissu walivyompiga risasi?
 
Watanzania wenye akili Timamu na wanaojitambua wanafahamu wazi kuwa CCM haihusiki hata kidogo na inalaani sana matukio yote ya utekwaji na kupotea kwa watu.ndio maana imeiagiza serikali na vyombo vyake kufanya uchunguzi wa kina kukomesha matendo na matukio hayo na kuhakikisha inawatafuta wote waliopotea .kikubwa ni sisi sote kuendelea kutoa ushirikianao kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama.

Kama ccm ingekuwa haihusiki na huu utekaji na mauaji, tungeona tume ya kijaji, ama shirika la kijasusi toka nje lingekuja kuweka ukweli hadharani. Lakini kuitaka serekali na vyombo vyake kujichunguza wakati ndio watuhumiwa, kuna lengo la kuficha ukweli maana ccm ni wafaidika wa huu unyama.
 
Amepangua na kujibu maswali yote kwa ufasaha mpaka waandishi wa habari wakabaki wanashangaa tu.
Ni kweli amepangua na kujibu maswali ya hao waandishi wa habari ambao wana hofu ya chama dola, lakini bado kila muandishi katoka hapo moyoni akiwa anajua ccm na serekali yake ni wahusika wa huu utekaji! Hicho kizazi cha kuongepea kiko wapi siki hizi?
 
Back
Top Bottom