Masaa ya kufanya kazi Tanzania ni machache mno, Nini kifanyike

Naongelea mambo kama maduka ya binafsi 24 hours. Sasa unaniambia ni salama kuwa kufungua duka lako kwa masaa 24 kwenye sehemu nyingi hapa kwetu?
Umesoma post yangu au umeanza kwa ku coment kwanza?

Nimetaja miji mikubwa kama Dar, Mwanza na Arusha na Mbeya.

Why miji mikubwa? huko ndo watu huja kwa shoping. Chukulia mfano Arusha watu wan mikoa kama Manyara na Singida na Kilimanjaro wanakuja so inatakiwa juwa bise.

Dar inahudumia nchi nzima. Kariakoo haipaswi kufungwa.

Swala la usalama nazani nimeeleza kabisa kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kama ni Kariakoo au just few Centres of Business District siyo vigumu kabisa. i thought you were making wider point.
 
Tutafika tu huko subiri SGR IKAMILIKE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi zipi?,usikute unazungumzia Kongo au Somalia. Majiji mengi usiku ni mchana. Huduma kuanzia za Safari za ndege na treni ni masaa 24 mkuu mambo ya kulala yako Africa huku.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nchi nyingi za Africa [emoji288] zimeamuka kama Egypt, South Africa, Nigeria, Algeria na Morocco majiji makubwa kalibia mengi yanafanya kazi 24 hrs. Serikali ingeboresha usalama, watu wakafanya kazi masaa 24
 
Inawezekana kabisa lakini pale tu kungewekwa pilot projects kuona kama itafaa kuweka kila mahala.

Yaani unaanza na kasehemu kadogo kujaribu hiyo ya kufungua maduka na biashara kwa msaa 24 halafu kama kuna mafanikio ndiyo unaweka sera na sheria na kuongoza hayo hivyo ndivyo wenzetu waloendela wanafanya.

Kwa mfano inaamuliwa kwamba maeneo kama Kariakoo, Masaki, Ubungo (tayari tuna Mlimani City), Kinondoni, Kimara na Mbezi yanakuwa maeneo ya biashara rasmi masaa 24 yaani Financial Districts.

Yaani hapo kuna kila kitu maduka makubwa Shopping Centres, mabenki yaaani ATMs na kufungua hadi jumamosi), migahawa, kumbi za cinema, bustani maalum za kupumzikia na kadhalika.

Bila kukosa , ulinzi, ama physical au CCTV, maegesho ya magari na mambo mengine yote muhimu.

Lakini unapoanza unaanza na eneo moja na twaweza sema kwamba twaanza na Mlimani City kupafanya Financial District, pawe na kila kitu mtu anachohitaji.

Ikifanikiwa hiyo basi unahamishia hiyo concept kwenda hayo maeneo mengine.

Ila hayo yote yanategemea na mazingira ya hizo sehemu kama idadi ya watu yaani uwezo wao wa kutumia pesa na mahitaji mengine kama umeme wa masaa 24 na maji.

Vinginevyo wazo lako ni top class.
 
Kwa mshahara huu huu wa TGS?? Una wazim weewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…