Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Huyu mh alikuwa amesahalika sana ameamua kutafuta kick kwa nguvu ili akumbukwe.

Unajua tangu aibiwe guest house kule Moro alipotea sana. Sijui ile silaha yake aliipata?

Haya tumekukumbuka mh Adam km
 
Makelele yote hayo anamkamata mtu mwehe heshima zake kama Malima, angekuwa anamkamata kibaka au teja siangetamba kama dume la ng'ombe? Afyatua risasi hovyo tena masaki, angekuwa manzese je? Huu wote ni ujinga tu.

Na hili jambo la kijinga linapaswa kukemewa na kila mtu mwenye akili timamu. Hivi kazi ya usalama barabarani si ni kazi ya trafik hawa madalali wanahusikaje? Hii biashara ya kipumbavu ya kukamata magari barabarani ilitokea wapi?

Kama trafik wameshindwa kazi yao basi sumatra wachukue hili jukumu badala ya kutumia wahuni.
 
Nimependa sana jinsi Malima alivyojihamini,hakutikisika wala kutishika na SMG...Ni Kama Nape kipindi kile,inaonekana watanzania wameshapunguza uwoga wa silaha...Hii ni hatua nzuri.
 
polisi huyo alifuzu mafunzo kwel...anajua sheria na matumizi ya bunduki kwel cjui km hayo yalikuw mazngira maalum yakufyatua risasi
 
Akome ...mnashangaa ni kupigwa risasi juu!!

Kila Mtu anatumia nyenzo zake kujilinda..

mfano:walimu wengi huwaponda wanafunzi na chaki wanakosea darasani.
 
Hili jambo lina impact kubwa kiuchumi, huwezi kuungurumisha marisasi mchana maeneo ya masaki wanakoishi wawekezaji wataona tanzania sio salama kuwekeza.
 
Hii 'drama' ya ajabu sana.. Askari kitu cha kwanza kufundishwa ni nidhamu.. Ati Askari tena Mkuu wa msafara anapata hasira.. Anapoteza mwelekeo.. Anatulizwa na 'Junior' wake.. Hata maganda ya risasi anasahau kukusanya..
Hivi hawa Polisi wamefundishwa 101 za kazi kweli?
Unatumia bunduki kizembe (kwa mkono mmoja),unapoteza risasi('burst'),unashindana na raia..
Maisha ya askari yanategemea anavyoweza kupunguza matumizi ya ovyo ya risasi.. Risasi ndiyo ulinzi wake..
Huyu Afisa wa Polisi alipaswa kumweka huyu raia chini ya ulinzi siyo kuonyesha ubabe..
Hatuwezi kuvumilia kuwa na Polisi ambao ni 'cowboys' na 'trigger happy'..
 
Aniokoe yeye Mungu? Acheni kutukuza upuuzi, kwa miiko ya polisi hapo kesho anatakiwa site kupiga kazi ngumu. Madaktari nao wasemeje ambao unafika kwao hata hujatambui

Kila taaluma na kazi inaumuhimu wake.
Huyo Mungu mwenyewe aliweka jeshi kupigana vita na maadui wa Taifa la Israel Soma vitabu vitakatifu na misaafu utaona kuwa hata huyo Mungu anajua kulinda kwa kutumia askari na jeshi.

Kwa hiyo, heshimu polisi kwa sababu wanalinda maisha yako. Aidha, moja Kwa moja au vinginevyo.
 
Hata plate no za magari na pikipiki zina bendera.

Kikubwa ninachokiona ni kwamba askari wetu huwa hawapendi kusikiliza. Wanachopenda wao ni amri tu basi. Mimi sikuona cha kumfanya afyatue risasi hewani.
Alichokua anajaribu kufanya ni kumtishia yule jamaa ili asiongee.

Naipenda nchi yangu nawapenda askari. Ila wajifunze namna ya kuwa na busara. Sio kila raia ni mharifu. Ndio maana wanapewa mafunzo ya kumjua mharifu kwa kumtazama tu.

Alafu wapunguze ubabe na wafuate sheria

wanahasira zisizosaidia

kama ningekuwa mtoa maamuzi yule asikari leo angelala rumande
 
27da66724a294deb876775eccb2389dc.jpg
ndo huyu anapewa heshima
 
Watu Wengi humu JF, wanawalaumu polisi ila ukiwa pale Benki unaambiwa egesha au ondoa gari eneo hili au lile mbona huwa hamji humu kusema polisi wabaya!?

Mbona tukiwa tunachukua hela kiasi kikubwa tunawalilia polisi watufanyie escort ili pesa zetu ziwe salama!?

Majambazi, wakikuvamia mbona kilio cha kwanza huwa ni kutoa taarifa polisi na kuomba msaada wao!?

Hebu jiulize, kama gari lilokuwa limeegeshwa kisha aliyeegesha akatenda uhalifu!?
Sasa hivi, ingekuwa tofauti kabisa humu JF , kuwa polisi inawaachia watu wanapaki ovyo na kusababisisha waharifu kutekeleza azima zao.

Angalia, lugha iliyotumiwa na hao waliopaki gari , kweli mtu mwenye sitaha na kujiheshimu na kuheshimu watu wengine anaweza kujibu vile!? Mbaya zaidi eti amekuwa hadi naibu waziri!?

Jiulize, ni mara ngapi watu wanapaki mahala siyo sahihi ila wanatumia lugha ya staha ao hao watendaji wanawaacha na kuondoa magari kwa ustarabu!?

Vyeo, nafasi fedha isiwe chanzo baadhi kuwadharau na kuona kazi za wengine hazifai.

Kutii, sheria na amri ndiyo suruhisho tu kwa mambo kama haya ili yasijitokeze.

Kama unamiliki gari basi jaribu kutembelea msasani na masaki yake uje usimame japo dakika mbili tu za kununua soda au maji kando ya barabara hata kama ni mita kumi kutoka ilipo barabara kuu halafu wale mbwa wanaoibia watu mchana kweupe wakukute ndio utuonyeshe mfano wa kuongea nao kauli nzuri.

Bila ya elfu 50 hawakuachi hata kama maneno yako yatakuwa na vina na virari.
 
Mungo park, kwanza alishaishiwa risasi akaanza kupanik na kuchimba mkwara apate msaada wa wenzie, halafu alipaswa aokote maganda hakufanya hivyo, tutajuaje labda risasi zingine alishauza.
 
Nimeangalia clip,Askari Polisi wa namna hawatakiwi kufanya kazi za operations kama hizo,anaonekana anafaa sana kuwa ktk kikosi cha kufuatilia wahalifu au majambazi wanaotumia silaha hukooo field ata enjoy sana kazi yake ya Polisi.
 
Kuna haja ya kutazama umri wao hawa jamaa, iwe kuanzia miaka 28 na kuendelea,naona utoto umezidi sana sasa.
Mtu anajiita serikali huku anafanya utoto hivyo?Halafu kavaa bendera yetu huku anaitambia?Maneno yake yanaonyesha bado hajakomaa kichwani,maana anajisikia inferior kwa raia mwenye v8 kiasi cha kulazimisha aonekane wa maana wakati tayari yeye ni wa maana.
 
Back
Top Bottom