Masanja Kadogosa katumbuliwa kama Katibu wa Bodi ya TRC. Je, anabaki na Ukurugenzi wake? Kama anabaki nao ni halali?

Acha kupotosha

Katibu wa Bodi ndio mratibu na muandaaji wa Mikutano yote ya bodi ikiwemo kuandaa board paper

Ushawishi wake ni mkubwa zaid ukiondoa wa mwenyekiti
wapi nimepotosha
mzee kuratibu na kuandaa haimpi mamlaka ya maamuzi (maamuzi yako kwa mwenyekiti na bodi yake)

katibu hutoa ufafanuzi wa kitaalamu kwa bodi (na wala bodi hailazimishwi kuukubali )

katibu ni mshauri tu kwenye bodi hana maamuzi yoyote

hii kuandaaa mikutano, kuandaa agenda mbona n kazi zake za kawaida unaona umenambia.jambo jipya
 
Wapi Masanja wawili kwenye story
 
Paschal
Tusimame kwenye ukweli tuache favour favour
Kama Mh. Rais angetaka kumuondoa kadogosa sababu ni msukuma angefanya hivyo but kadogosa anatuhumiwa kwa kuendesha kandarasi Tena yenye Bei ya juu na kuletela hasara
Sasa kadogosa ni mtu safi, mkarimu, very social man kila mtu anajua but kwa kashfa hii anaachwa Ili iweje

Hapa ishu sio usukuma
 
Ndiyo matatizo ya kofia 2. Ni sawa na CCM inakaa chini ya mwenyekiti wa ccm (rais) kuitaka serikali (inayoongozws na huyo huyo mwenyekiti) ikamilishe miradi.

Mbwa kala mbwa!
 
Kama magufuli aliteuwa wasukuma wengi kwa nn unamshauri mama asiwatoe?
 
Mhe Rais amevunja Bodi ya Wakurugenzi wa TRC. Kwa uelewa wangu Bodi yeyote inaundwa na Mwenyekiti, Wajumbe na Mtendaji Mkuu wa Taasisi husika. Swali langu Je Mtendaji Mkuu wa TRC pia ameondolewa?. Kama jibu ni hapana ni kwa nini hakuondolewa yeye akiwa "Think Tank" katika Bodi hiyo.
 
Rejea thread zilizopita.
Futa hii
 
Mtendaji mkuu wa Taasisi yeye si sehemu ya wajumbe wa Bodi..
 
Manejimenti sio sawa ba Bodi. Watendaji wakuu wanaingia kwenye bodi za taasisi zao kwa nyadhifa zao na kuwa Katibu wa bodi. Angetenguliwa nafasi yake ya CEO kabla ya kuvunjwa bodi, ndio atapoteza sifa ya kuingia kwenye bodi.
Ni kama Mwanasheria Mkuu anavyokuwa bungeni. Bunge likivunjwa mwanasheria Mkuu atabaki kuwa AG. Lakini akitenguliwa AG yake, basi haingii tena bungeni.
Watu wana chuki hadi akili hazichaji vizuri.
Wasikupotoshe.
 

..kwa uelewa wangu mkurugenzi mkuu wa shirika huwasilisha mapendekezo au mpango kazi halafu bodi ya wakurugenzi humpa ruhusa ya kutekeleza.

..kwangu mimi inaniwia vigumu kuamini kwamba bodi ya wakurugenzi ya shirika inaweza kuwa imekosea, na mkurugenzi mkuu akawa hahusiki na makosa hayo.
 

..nadhani hili suala lina mkanganyiko.

..kwa mfano kuna wakati Raisi alivunja bodi ya wakurugenzi ya Tra kwa kuituhumu kufanya makosa fulani.

..sasa ndani ya bodi ya Tra kuna wajumbe kama Katibu Mkuu Hazina ambao wanaingia ktk bodi kwa nafasi zao.

..sasa mimi nilidhani kama mhusika ametimuliwa ktk bodi ya Tra basi atatimuliwa hata huko alikotokea.

..kama Raisi ameona mhusika amefanya madudu akiwa mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa Tra, anawezaje kuendelea kumteua / kumuacha ktk nafasi ya Katibu Mkuu Hazina?
 
Kuna Utata sana
 
Katibu Mkuu Hazina ni individual responsibility. Ndani ya bodi kuna collective responsibility.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…