KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,185
- 37,239
Alichokisema masanja kina akisi uhalisia wa maisha ya vijana wengi ambao wanajiita wazaliwa wa mijini ingawa ujumbe wake ameuleta katika njia ya kejeli.......kiukweli hata ukikaa katika maskani huwezi kusikia mawazo mbadala au mbinu za kujikwamua kimaisha zaidi kukutajia kila aina ya dawa zinazoongeza nguvu za kiume na gest na baa maarufu hapa mjini......ni vijana ambao hawajui kuwa siku zinakwenda na miaka inabadilika.....wao wanadhani kuwa wataendelea kuwa vijana milele na milele......na wataendelea kuishi kwenye vibanda vya baba zao wao pamoja na wajukuu zao.........ni akili za watu waliofeli maisha.......MUNGU AWAREHEMU WAPATE KUJUA KUWA TUNAISHI KATIKA NYAKATI NGUMU AMBAZO MWANAUME ANATAKIWA ALE KWA JASHO....TENA JASHO LA DAMU,......