Masanja na Uropokaji kwa Wazee!

Masanja na Uropokaji kwa Wazee!

Mimi niliangalia kipindi kile, ijapokuwa nilikuwa na hama hama kati ya TBC1 na EATV, pale mwishoni alipokuwa anafunga kipindi Masanja alitoa maneno yaliyokuwa yanaonyesha hasira yake juu ya EATV na R. Mengi.

Ingawa hakutaja jina, lakini sentensi kama hii ahihitaji mtu kujua sayansi ya kurusha roketi kujua alimaanisha nini, alisema...."watu wana hela lakini wana roho mbaya (huku akionesha ishara ya kukunja kidole) wana hela nyingi lakini hawatosheki......na je kwa nini wameweka muda huu huu......si wangetafuta muda mwingine?" Alafu akaendelea..."najua sasa hivi watazamaji mnaenda kwa jirani ku angalia....lakini sisi ndo wenye vipaji vya ukweli...hatuna hela lakini tuna vipaji...."

Ni wazi alikuwa akiwasema EATV na kipindi chao kipya cha Ze Comedy....ambacho kinarushwa muda sawa sawa na kipindi cha Orijino Komedi cha kina Masanja!!!

Masanja anasahau kwamba EATV walikuwa wanarusha hicho kipindi muda huo huo hapo mwanzo....na ni TBC1 na kina Masanja unaweza ukasema ndo waliiga muda (ambapo kwangu naona sio issue).

Nakumbuka hata kipindi kile Futuhi wa Star TV na Vimbwanga time wa Channel 10 wanaanza, kina Masanja waliwapiga madongo sanaaaa!!

Ninachokiona hapa ni kwamba kina Masanja, Joti na Seki hawajui maana ya soko huria ambapo kila mtu ana uhuru wa kuingina sokoni na kuuza bidhaa au huduma anayoitaka. Katika mfumo huu ni soko tu ndilo litakalomfanya mtu aitoe bidhaa yake sokoni, kwa mfano Vimbwanga time cha Channel 10 walivyoacha kurusha kipindi hicho.

Masanja et al acheni kutukana watu........TV station zenyewe ziko 3 tu hapa nchini sijui mtakimbilia wapi mkitemwa TBC1. Kila mtu atakayetaka kufanya kazi na nyie ataogopa kudhalilishwa siku mtakapo vunja mkataba!!

Naona upeo wenu wa kufikiria ni mdogo sana, nawashauri acheni majungu na visilani.......pigeni kazi, kipindi bora ndicho kitakachoangaliwa na watamaji na si vinginevyo!!

Ni hayo tu!

Kiongozi umeona senksi niliyokukabidhi kwa hii yuzifuli posti?
You have said it. You have said it well.
Nadhani mjadala umeuhitimisha vizuri.
Kwamba The Orijino komedy Hawana adabu, waoga na hawana shukrani: Period!
 
hodi wenyeji, hodi tena!
Naomba kukaribia kwenye jamvi na kamchango kadogo Huyu mshkaji masanja hakumtaja jina mtu. Mchangiaji kwa fikra zake amemrenga R. Mengi. Ni sawa na maneno ya kwenye khanga mwingine anaweza soma akasema amenivalia mimi je mtengenezaji alijua wewe na huyo mna bifu? ACHA KUJISHUKU NGOMA HUJAPIGIWA WEWE, UNACHEZA.
Kijana nna mashaka na wewe. Unaanza na posti ya kwanza kwa pumba?Kuwa muungwana bisha hodi kwanza ukaribishwe!

Nenda kwenye jukwaa la utambulisho kwanza ujitambulishe huko, ndo uanze kuflow
Ahaa! Kumbe na wewe kiongozi umemtukia? Anaitwa Bandaz! Kule kwetu ukisema Bandaz........! Hehehehe!
 
Wenye shida siyo kina Masanja bana,hao ni nyasi tu kwenye bonde la mpunga mwenye maamuzi ni mkulima kupalilia nyasi na kuacha mpunga au kupalilia mpunga na kuacha nyasi. Hivyo basi hata mwajiri wao pia ana matatizo makubwa katika jamii.Kama Utawala wa sheria ni kutupiana madongo kwenye chombo cha umma kwa kuuchafua umma unatarajia nini???
 
Masanja aache mambo ya kitoto,yote maisha na wala pesa haina mwisho hata uwe tajiri vipi.
Kama alishindwa ITV atulize boli afanye kazi na si ushambenga tuuuuuuuuuu.
 
Kama ni kupiga vijembe watu maarufu mbona walianza tokea wako EATV? Au ndio tunawaona sasa?
 
Sioni kama hawa Orijino Comedy wanakwenda vizuri siku hizi. Tangu wametoka EATV wanapiga majungu tu. hata huko kuchekesha hakuna. Nawaona huko mbele hawatakuwa na mwisho mzuri.

Si hilo la juzi tu. hata week kama mbili kabla waliimba wimbo wakimkashifu Mengi, baadhi ya Maneno ya wimbo huo yalikuwa hivi,

".. Ningetoa mali zangu,, kuwalisha masikini,.... kama sinao upendo... mimi si kitu kabisa..."
Sifai Mbele za Bwana.... Sifai Mbele za Bwana,,, kama sinao Upendo Mimi si kitu kabisa,,,,
huku Masanja akiongezea baadhi ya maneno kama "na vilema na viwete". Akimaanisha Mengi analisha Maskini, Vilema Na Viwete wakati hana upendo.

Lets wait and see mwisho wa haya yote.
 
Sioni kama hawa Orijino Comedy wanakwenda vizuri siku hizi. Tangu wametoka EATV wanapiga majungu tu. hata huko kuchekesha hakuna. Nawaona huko mbele hawatakuwa na mwisho mzuri.

Si hilo la juzi tu. hata week kama mbili kabla waliimba wimbo wakimkashifu Mengi, baadhi ya Maneno ya wimbo huo yalikuwa hivi,

".. Ningetoa mali zangu,, kuwalisha masikini,.... kama sinao upendo... mimi si kitu kabisa..."
Sifai Mbele za Bwana.... Sifai Mbele za Bwana,,, kama sinao Upendo Mimi si kitu kabisa,,,,
huku Masanja akiongezea baadhi ya maneno kama "na vilema na viwete". Akimaanisha Mengi analisha Maskini, Vilema Na Viwete wakati hana upendo.

Lets wait and see mwisho wa haya yote.


Once you know they are stupid, jus leave them as they are! Their destiny us ful of shame. I can assure you
 
kila siku wanatupunguzia hamu ya kuendelea kuangalia Ze Komedy
 
Jana kama kuna mtu alipata kutazama kipindi cha Orijino Komedi, basi lazima angepatwa na jazba nyingi, hasa katika sehemu ya umalizaji wake.
Masanja katika hali ya kuonyesha kukerwa na kuanza kwa kipindi-pinzani cha EATV cha kusaka wachekeshaji, basi alitoa kauli 2 chafu zote zikimlenga R.MENGI, kama hivi:
i-Mtu anajifanya tajiri na ana hela, sijui kwanini anachanganyikiwa na mambo madogo kama haya!

ii-Nilitegemea UMRI wake (Mengi) ungeendana na mambo yake, lakini kumbe wapi, ndo hivyo tena!

Binafsi niliboreka sana na maneno hayo, si kwamba nampenda sana Reginald, lakini kumkashifu mtu kama yule aliyemzidi umri mno ni kinyume cha maadili kabisa!
Hana adabu kabisa Masanja, *+$%%*inkoskaz huyu!😡....
be cool men hayo mambo ya kutiana adabu ni mambo ya komedi zote duniani. Uharibifu wa utandawazi yep no ukweli wa mambo yes kabisaaaa lakini nanbi anamjua Mengi kisawasawa. kisha kwanini watu wanakuwa pissed off very izi. kama kucharazwa mtu kalamu si unakaa na domo lililojaa hasira na matrusi yalifungwa zip. Hii dunia huru bana kwe kwe kwe kumbe huuma ehe ehe
 
Sio masanja tu, bali pamoja na washirika na washabiki wake wote IQ zao ni finyu sana.

Hizi kauli ndio uwa sizipendi. Inaonyesha wewe mwenye IQ ndogo pia. Yeye kamkashfu mengi indirect bila kumtaja jina. Alichofanya ni uupuzi na vitu kama hivi vinaweza kumletea matatizo.

Kwa upande wingine wale ni watu wa comedy kuna wakati wanatoa comedy nzuri tu na kupata washabiki wengi.. Sasa unapokuja na kusema washabiki wao IQ zao ni finyu unaweza kukuta mshabiki mkubwa wa masanja ni MAMA yako sasa hapo sijui inakuwaje?

Kuwa makini kabla ya kuandika kitu....Unaboa


Regards
 
Wenye shida siyo kina Masanja bana,hao ni nyasi tu kwenye bonde la mpunga mwenye maamuzi ni mkulima kupalilia nyasi na kuacha mpunga au kupalilia mpunga na kuacha nyasi. Hivyo basi hata mwajiri wao pia ana matatizo makubwa katika jamii.Kama Utawala wa sheria ni kutupiana madongo kwenye chombo cha umma kwa kuuchafua umma unatarajia nini???
kwani hawa wameajiriwa na nani? hebu kwanza tutazame data zetu vizuri. Wameajiriwa na nani? wana kampuni yao hawa walichofanya wameingia mkataba na TBC .Sasa nani hasa ana matatizo? Mbona tunafurahia sana methali ya kiswahili samaki mmoja akioza katika tenga wote wameoza. Msitie kabali isiyopimwa katika mizani unaweza kuwa unajaribu kumtemu papa na ndoana ya tuna. Utachekesha
 
Kiongozi umeona senksi niliyokukabidhi kwa hii yuzifuli posti?
You have said it. You have said it well.
Nadhani mjadala umeuhitimisha vizuri.
Kwamba The Orijino komedy Hawana adabu, waoga na hawana shukrani: Period!
Mjadala haujahitimishwa hata kidogo. Unaposema watu wanakosa shukurani unamaana gani.Yaani kwa kuwa hawa CCM (enzi hizo Tanu) imeleta uhuru basi wao waendelee kuwapo tu hata kama wanaboronga? kila mtu anastahili kufanyakazi zake nashukurani si ya kusubiriwa.Hivi mnajua hasa dhuluma maana yake nini?kukosa shukurani si dhuluma bali kuomba upewe shukurani kwa kosa lililohitimisha dharuba ya mwisho katika ncha ya sindano ndio dhuluma yenyewe.Mwenye masikio huambiwa asikie na mwenye macho aambiwa aone na ambaye hana macho lazima atembee afungue hisia namba sita au la kama ni mchonga vinyago kipofu kupapasa kunaweza kukuletea jibu zuri.Acheni hizo hakuna anayemjua mengi vizuri zaidi kama aliyeshawahi kuingia mkataba naye.Sisi kwetu vicheko na zaburi tu, kila kitu kityalipwa hapa hapa.Unadhani kesi za wafanyakazi wale wanahangaika ni za bure tchao mwenye hasira aropoke mpaka nyongo
 
Jamani Masanja simlaumu sana na siwezi kukubaliana na mtu akisema Masanja ni mlopokaji. Hivi mtu anayesoma taarifa ya habari anaweza kuwa ni mlopokaji? Sasa msi - mjaji Masanja kwa hilo, ila kwa kifupi waandaaji wa kipindi cha the commedy ndo wamekiharibu na kama business world watu lazima watumie weakness zako kutoka hapo sio kosa la EATV. Wakati the comedy ikiwa EATV ukweli mbaya hata mimi nilikuwa naangalia sasa walipohamia huku, du ukikaa na mwanao mtajikuta mnavuliwa nguo maana wanafurahisha aina furani ya jamii na sio mlengo kwa jamii yote. Hivyo tuwaache watakuwa fundisho kwa wengine watakaposhindwa kulipia bill TBC. Maana watakosa watu kabisa, ukipata cheza nacho vizuri usijisahau, sasa wale walijua ndo wenyewe wenye kuweza. haya weee.

Pia mimi nimeona watu wenye access na media mara nyingi huwa wana mis-use, mwangalieni Kibonde clouds anaweza akaanza ku-judge kitu ambacho hana data na kumharibia mtu mambo yake maana kuna watu wanasikiliaza na kuamini period ! hawaendi in details. Lakini jambo ambalo hawajalijua ni adhabu za kificho, they create enemies.
 
Jana kama kuna mtu alipata kutazama kipindi cha Orijino Komedi, basi lazima angepatwa na jazba nyingi, hasa katika sehemu ya umalizaji wake.
Masanja katika hali ya kuonyesha kukerwa na kuanza kwa kipindi-pinzani cha EATV cha kusaka wachekeshaji, basi alitoa kauli 2 chafu zote zikimlenga R.MENGI, kama hivi:
i-Mtu anajifanya tajiri na ana hela, sijui kwanini anachanganyikiwa na mambo madogo kama haya!

ii-Nilitegemea UMRI wake (Mengi) ungeendana na mambo yake, lakini kumbe wapi, ndo hivyo tena!

Binafsi niliboreka sana na maneno hayo, si kwamba nampenda sana Reginald, lakini kumkashifu mtu kama yule aliyemzidi umri mno ni kinyume cha maadili kabisa!
Hana adabu kabisa Masanja, *+$%%*inkoskaz huyu!😡....
you should 1st know what is the so called COMEDY?? na madhumuni yake.....
......then mie sijawahi angalia hicho kipindi sababu nipo mbali na nje ya nyumbani Tz......BUT i'm sure kabisa huyo mchekeshaji hakutaja jina uliloliandika hapo.......
..(kama vp tutafutie hiyo video utuwekee hapa na kututhibitishia akilitaja hilo jina la ulilolitaja wewe hapo juu).....
....USHAURI...usipende tafsiri kauli za watu in negative attitudes bila kujua ukweli halisi wa msemaji binafsi alimaanisha nini .....then kumbuka THAT IS A COMEDY...
 
Big Up Hofstede na Kiranga. kikubwa hapa ni kutoa lugha ya kashfa iwe kwa mtoto hata mkubwa.Binafsi siipendi regardless hiyo lugha inatolewa kwa Ndg.Mengi or ndg Machache . Ila hilo jina la Mengi hatujasikia likitajwa mwanzo hadi mwisho wa kipindi.mwenzetu pakajimmy mmh! ni feelings zako na BROOKLYN au?
 
BABA umesema mwenyewe kuwa huwa hutazami kipindi hicho, kwa jinsi masanja alivyo present kile kipindi huhitaji akutajie jina ili ujuwe mlengwa ni nani? yes wakati wako EATV kipindi kile likiwa COMEDY lakini sasa nafikiri ni zaidi ya komedi. Si mmakumbuka walipoanza kuwasema watu waziwazi katika ile session yao ya ALYEFULIA! tuliposema sana wameondoa! tatizo la crew nzima ya Orijino Komedi ni wapenda visasi sana. Hebu niulize kuna connection gani kati ya MANJI na Orijino Komedi, isije kuwa hawa vijana wanatumiwa tu na "washindani" kama sio wapinzani wa mzee Mengi! BABA nakushauri tu kabla hujaanza kumtetea sana Masanja jaribu kufuatilia historia ya kundi hili!
 
Nilitazama hicho kipindi tangu mwanzo hadi mwisho sikusikia jina la Mengi likitajwa.


Hahah mama mkwe unanitia aibu, sasa kweli wewe hukusikia jina la Mengi na ulitazama kipindi mpaka mwisho. Sasa mkweo muongo basi. Pole
 
massanja hajaenda shule...lete thread za kujadili watu wa maana..ni mpuuzi yule..achana nae.
 
Back
Top Bottom