Masauni, Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, wananchi wako wanahangaika na shida ya maji

Masauni, Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, wananchi wako wanahangaika na shida ya maji

silent lion

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2012
Posts
1,278
Reaction score
1,794
Mheshimiwa najua una majukumu mengi ya kitaifa kwa vile wewe ni Waziri, lakini angalau ungezungumza na muwakilishi Mheshimiwa Jazira, mkalipatia ufumbuzi tatizo hili.

Majimbo ya Zanzibar ni madogo mno kulinganisha na bara, yaani huku jimbo unaweza kutembea kwa miguu nusu saa tu ukawa ushalimaliza. Lakini jimbo hilo lina muwakilishi, lina mbunge, lina diwani zaidi ya mmoja, lina sheha zaidi ya moja, cha ajabu wote hawa huwaoni mpaka uchaguzi ukaribie, si vizuri mnavofanya.

Taswira za watoto wadogo wakiwa na ndoo za maji kichwani, pamoja na wakina mama hazipendezi kwa kweli.
 
Huyu ilitakiwa atumbukiwe uwaziri hajui lolote wananchi wanakufa kwa ajali hatoi hata pole huyu anaramba asali tu
 
Hivi kwanini anakuwa na vyeo viwili?
Mbunge
Waziri
Hapa inaonesha atashindwa kimajukumu achague nafasi moja hii iwe sheria nchini.
 
Chumba kisima chako mwenyewe.
Hujui kwamba mheshimiwa Yuko bize anakula Bata Dodoma? Unataka aache starehe zake kwa shida yako?
Kwanza hamkumchagua huyu Ni chaguo la mwenda kuzimu.
 
Chumba kisima chako mwenyewe.
Hujui kwamba mheshimiwa Yuko bize anakula Bata Dodoma? Unataka aache starehe zake kwa shida yako?
Kwanza hamkumchagua huyu Ni chaguo la mwenda kuzimu.
Nimekuelewa, ila mnyonge kisima anamudu vipi kukichimba
 
Chumba kisima chako mwenyewe.
Hujui kwamba mheshimiwa Yuko bize anakula Bata Dodoma? Unataka aache starehe zake kwa shida yako?
Kwanza hamkumchagua huyu Ni chaguo la mwenda kuzimu.
Akumbuke wapiga kura wk
 
Back
Top Bottom