Masauni na IGP Wambura wakijiuzulu itatoa picha gani kitaifa na kimataifa?

Masauni na IGP Wambura wakijiuzulu itatoa picha gani kitaifa na kimataifa?

Mr-Njombe

Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
64
Reaction score
122
Wana JF
Kumekua na maoni, mitazamo, mapendekezo na wito kutoka kwa watu mbalimbali mashuhuri, taasisi na vyama vya kisiasa kumtaka waziri mwenye dhamana ya mambo ya ndani ajiuzulu nafasi yake, lakini pia hata mkuu wa Jeshi la Polisi nchini nae kufanya vivyo hivyo kulingana na changamoto za kiusalama zinazoendelea nchini.

Kwa maoni yangu, hilo halitaweza kutokea kwa sasa au kufanyika kwa wakati huu, kwani kwa kufanya hivyo ni kuthibitisha uzembe na ushiriki wao katika hayo yaliyotokea, ili hali bado haijathibitika dhahiri kama ni vyombo vya ulinzi ndivyo vinahusika au la. Hivyo kesi hii ya sasa ni tofauti kidogo na ile ya wakati wa Hayati mzee Mwinyi, kwani angalau kipindi cha Mwinyi ilikua bayana kua polisi walihusika kwa namna moja au nyingine.

Ila kwenye hili la sasa, mpaka sasa hakuna ushahidi wa moja kwa moja usio na shaka, bali ni hisia na mihemko binafsi ya wananchi, kitu ambacho sio kibaya na ni haki. Hivyo tusitegemee yeyote kujiuzulu labda Mama abadilishe tu mkeka, kuimarisha utendaji wa serikali yake.

Soma Pia:
Kwa yeyote kati yao kujiuzulu sasa, itathibitisha kua anajiuzulu kutokana na vitendo vya kizembe vya majeshi yaliyo chini yao, na kwa hivyo hawawezi na itakua vigumu kwa wao kua tayari kujiuzulu.

Mwaveja sana, kwa maoni yako unadhani itaashiria nini au itatoa picha gani?
 
Mmh! Mzee Butiku kasema Kuna mwaka hayati mzee Mwinyi alijiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani baada askari magereza kuuwa wafungwa. Mbona hakuna picha yoyote mbaya iliyochorwa juu ya taifa letu?

Huo ndiyo utakuwa uwajibikaji wa pamoja wa viongozi.

Waache kutafuta uchochoro wa kujifichia.
 
Mmh! Mzee Butiku kasema Kuna mwaka hayati mzee Mwinyi alijiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani baada askari magereza kuuwa wafungwa. Mbona hakuna picha yoyote mbaya iliyochorwa juu ya taifa letu...
ungekua wewe ungejiuzulu ilihali huna haika kama ni kweli vyombo vyako vinahusika au la. huoni itakua kama baba anaekimbia changamoto za kwenye familia
 
sioni sababu hata moja kwa hao wangwana kujiuzulu,
kuwajibika ni kufanya kazi kwa bidii kwenye mazingira yote magumu na rahisi na kutafuta majawabu ya mkwamo ulioko.

kijiuzulu ni kukimbia tatizo sasa sijui wamuachie nan? :pulpTRAVOLTA:
 
ungekua wewe ungejiuzulu ilihali huna haika kama ni kweli vyombo vyako vinahusika au la. huoni itakua kama baba anaekimbia changamoto za kwenye familia
Kule Japan kuna waziri mkuu alijiuzulu baada tu ya kusikia (pigia mstari neno kusikia) kuwa kuna mzazi kanunua maziwa ya pakti (ya kusindikwa) dukani akamnywesha mtoto Kisha mtoto yule akafa.

Kuna mwingine tsunami ilivyotokea alijiuzulu, akidai kuwa alipaswa kuwapa tahadhali wananchi. Kumbuka tsunami ni natura disaster.
 
ungekua wewe ungejiuzulu ilihali huna haika kama ni kweli vyombo vyako vinahusika au la. huoni itakua kama baba anaekimbia changamoto za kwenye familia
Issue sio kuwa vyombo vyako vimehusika. Umeshindwa kusimamia usalama wa raia.
 
Kujiuzulu ni kulinda heshima - wapumzike tu hawa wazee wetu. Mambo yashawaharibikia.
 
Sijasoma yote.

Picha ya kuwa tuna viongozi waadilifu wanaokubali kujiwajibisha.
 
Back
Top Bottom