Maselle "Chapombe" afunga ndoa!!

Freyzem

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2013
Posts
10,120
Reaction score
24,667
Msanii wa siki nyingi wa vichekesho aliyejipatia umaarufu katika kundi la vituko show kwa style yake ya kuigiza kama mlevi, Chrispine Lyogello "Masele" ameaga ukapela baada ya kufunga pingu za maisha na mchumba wake wa siku nyingi Specioza Malick katika kanisa Katoliki, Bikira Maria Consolata lililopo Mbezi Makabe jijini Dar es salaam.
 
Big up sana. Mshkaji nilikuwa naikubali sana style yake ya uigizaji, sana sana zile ajali zake. Mlevi mwenye swag. Brothaman's the truth.

Kila la kheri kwao.
 
Katika mahusiano ya sasa kuna kitu hakiko sawa.

Inafika mahali hata umuhimu wa kwenda HONEYMOON haupo tena maana watu wanafanya tendo la ndoa hata kabla ya ndoa yenyewe.

Hili tatizo ni kubwa sana.
 
Kuna watu wapo kama hawana dhambi vile... unaweza ukawa huna dhambi ya uzinzi ila ni msengenyaji,mwizi na muuaji mzuri tu. Nyie sio Mungu na wala hamuwezi jua kabla ya kufunga ndoa yao waliongea nini na Mungu.
 
Katika mahusiano ya sasa kuna kitu hakiko sawa.

Inafika mahali hata umuhimu wa kwenda HONEYMOON haupo tena maana watu wanafanya tendo la ndoa hata kabla ya ndoa yenyewe.

Hili tatizo ni kubwa sana.
Honeymoon ivi ipo kwenye vitabu vitakatifu au kaja nayo mzungu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…