Mashabiki wa Arsenal wafanya maombi ya kuchukua kombe

Mashabiki wa Arsenal wafanya maombi ya kuchukua kombe

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
images (4).jpeg
Mashabiki wa Arsenal nchini Kenya leo wamefanya siku yao ya kitaifa ya maombi kuombea mafanikio ya timu hiyo.

Wafuasi hao hufanya maombi kila mwaka ambayo imekuwa desturi, na kwa kawaida hujitolea kushiriki katika shughuli za hisani ikiwemo kutoa shukrani makanisani na kufanya maombi ya klabu hiyo ya England.

Klabu ya Arsenal ya mashabiki hao wa Kenya, ambayo zamani ilijulikana kama Klabu ya Mashabiki wa Kenya Arsenal, ilizinduliwa awali Oktoba 2010.

Kundi hilo linatambuliwa na klabu hiyo na lina nafasi maalum ya bendera katika Uwanja wa Emirates jijini London.

Mkutano wa kwanza wa kikundi ulifanyika katika Club Red Carpet, na tangu wakati huo umekuwa na kufikia matawi mengi kote nchini Kenya, ikiwa ni pamoja na Nairobi, Mombasa, na Eldoret. Kikundi kinafanya kazi za hisani, kufanya mashindano, na kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya jamii.
 
Back
Top Bottom