Mashabiki wa Galatasaray wapagawa kuwasili kwa Osimhen

Mashabiki wa Galatasaray wapagawa kuwasili kwa Osimhen

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
1725348414782.png

Baada ya saga lake la usajili kutikisa hatmaye mshambuliaji wa the Super Eagles, Victor Osimhen amekubali kujiunga na klabu ya Galatasaray kwa mkopo kwa msimu ujao.


Mashabiki wa Galatasaray wameonyesha shangwe na furaha kubwa baada ya kuwasili kwa Osimhen, mshambuliaji mahiri anayetarajiwa kuimarisha kikosi cha timu hiyo. Ujio wake umewafanya mashabiki kujaa mori, wakimkaribisha kwa shangwe na nderemo, huku wakitarajia kuiona timu yao ikifanya vizuri zaidi msimu huu


Liverpool ilikuwa ni moja kati ya timu zilizotaka kumsajili mshambuliaji wa Napoli na Nigeria, Victor Osimhen katika dirisha lililopita la majira ya kiangazi, lakini ilishindikana baada ya kutaka mshahara mkubwa.Mabosi wa Liverpool walitaka kumsajili Osimhen, 25 kujiandaa na maisha bila Mohamed Salah ambaye mkataba unamalizika mwisho wa msimu huu. Salah anahusishwa na timu nyingi za Saudi Arabia tangu majira ya kiangazi 2023.
1725349020667.png

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye alikuwa kwenye rada za klabu ya Premier League Chelsea kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili la England siku ya Ijumaa, na pia klabu ya Saudi Arabia, sasa ameelekea Istanbul. Osimhen amefunga mabao 76 katika mechi 133 alizochezea Napoli na alikuwa na mchango mkubwa katika ushindi wao wa taji la Serie A msimu wa 2022-23 kwa kufunga mabao 26.

Osimhen amefunga mabao 76 katika mechi 133 na aliongoza Napoli kutwaa taji la Serie A msimu wa 2022-23. Hata hivyo, kiwango chake kilishuka msimu uliopita akifunga mabao 15 pekee. Napoli wamesajili Romelu Lukaku kwa pauni milioni 30, wiki iliyopita kama mbadala wake
1725349073466.png
 
Mbona bado mdogo tu kwanini ameenda klabu ya kiwaki hivyo?

Wakati mwingine mshahara sio kila kitu, angeenda Liverpool japo kwa mshahara kiduchu perfomance yake ingembeba.
Unasaini mi4 kwa mshahara kiduchu wakati ni hot cake of strikers ukiondoa majeruhi. Asubiri mshahara mdogo miaka mi4? Siku hizi wanaangalia sana maslahi

Angalia timu ya Al Hilaal wachezaji wake.
 
Nadhani kaenda hapo sababu ya mgogoro wake na Napoli maana kwanza waliweka dau Al Hilal kama sio Ahly wakafika bei wakapandisha tena
Hadi dirisha linafungwa walishindwa kufanya maamuzi huku wakiwa wameshamliplace na lukaku hawakuwa na namna zaidi ya kumuachia aende kwa mkopo ili asikae benchi huku mteja akiendelea kupangwa hope dirisha dogo ataenda uarabuni
 
Mbona bado mdogo tu kwanini ameenda klabu ya kiwaki hivyo?

Wakati mwingine mshahara sio kila kitu, angeenda Liverpool japo kwa mshahara kiduchu perfomance yake ingembeba.
Alizingua mwenyewe mkuu alikua anataka hela nying hata ambazo halland wala mo salah alipwi uingereza mkuu ko wakampiga chini
 
Osimhen anajiharibia mwenyewe, mpira ni mchezo usio na uhakika, kuna kuFLOP, injuries na mengine, sasa ukiharibika ukiwa timu ndogo hali inakuwa tete.
 
Back
Top Bottom