demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Wapenzi na Mashabiki wa Simba SC tuwe tunajitokeza kwa wingi kwenye mitandao ya Kijamii hasa kwenye kurasa za msemaji wetu wa klabu Hadija Manara.
Mara baada ya kuisha kwa mtanange wa leo, na kupata na bumbuwazi lililo tokana na kikosi chetu cha Bilioni 1.3 kimetoka sare na kikosi cha wanajangwani walio kosa huduma za wachezaji wao 3 tegemezi Ngoma, Tambwe na Kamusoko, Msemaji huyo alijikuta akiweweseka na kupost mada kwenye ukurasa wake wa Instagram bila kuifanyia uchambuzi wa kina.
1. Kuhusu takwimu ya mechi kwenye kipindi cha kwanza.
Tumkumbushe Manara kuwa hata kama timu yetu iliongoza possesionkipindi cha kwanza, Possesion hiyo haina maana na mantiki yeyote ile kama Kikosi chetu chenye thamani ya Bilion 1.3 kimeshindwa kupata hata shuti moja on target.
Hili ni dhahiri kabisa kuwa mpira wa possesion tulikuwa tukiucheza mno kwenye upande wetu wa uwanja.
2. Kuhusu watani zetu kushangilia matokeo ya sare pale uwanja wa uhuru.
Pia tumkumbushe kuwa asitufanye sisi kuwa ndio misukule hata tushindwe kujua na kuitambua picha halisi ya tikio.
Kwenye hii picha amedai kuwa hawa ni wanayanga wakiwashangilia wachezaji wao baada ya kupata matokeo ya 1 - 1 wakiwa kwenye basi lenye muonekana na picha zamdhamini wa zamani Kilimanjaro.
Asijifanye kuwa kana kwamba hatuujui muonekano wa basi jipya la msimu wa mwaka 2017/18 lenye nembo ya mdhamini mpya...
Tumsaidie kijana mwenzetu aisee! Asije kupata ugonjwa ya kuchanganyikiwa.
Mara baada ya kuisha kwa mtanange wa leo, na kupata na bumbuwazi lililo tokana na kikosi chetu cha Bilioni 1.3 kimetoka sare na kikosi cha wanajangwani walio kosa huduma za wachezaji wao 3 tegemezi Ngoma, Tambwe na Kamusoko, Msemaji huyo alijikuta akiweweseka na kupost mada kwenye ukurasa wake wa Instagram bila kuifanyia uchambuzi wa kina.
1. Kuhusu takwimu ya mechi kwenye kipindi cha kwanza.
Tumkumbushe Manara kuwa hata kama timu yetu iliongoza possesionkipindi cha kwanza, Possesion hiyo haina maana na mantiki yeyote ile kama Kikosi chetu chenye thamani ya Bilion 1.3 kimeshindwa kupata hata shuti moja on target.
Hili ni dhahiri kabisa kuwa mpira wa possesion tulikuwa tukiucheza mno kwenye upande wetu wa uwanja.
2. Kuhusu watani zetu kushangilia matokeo ya sare pale uwanja wa uhuru.
Pia tumkumbushe kuwa asitufanye sisi kuwa ndio misukule hata tushindwe kujua na kuitambua picha halisi ya tikio.
Kwenye hii picha amedai kuwa hawa ni wanayanga wakiwashangilia wachezaji wao baada ya kupata matokeo ya 1 - 1 wakiwa kwenye basi lenye muonekana na picha zamdhamini wa zamani Kilimanjaro.
Asijifanye kuwa kana kwamba hatuujui muonekano wa basi jipya la msimu wa mwaka 2017/18 lenye nembo ya mdhamini mpya...
Tumsaidie kijana mwenzetu aisee! Asije kupata ugonjwa ya kuchanganyikiwa.