Mashabiki wa Simba SC wanaongoza kwa kujitoa ufahamu na hawajitambui

Mashabiki wa Simba SC wanaongoza kwa kujitoa ufahamu na hawajitambui

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Leo hii analaumiwa Okrah, mechi iliyopita alilaumiwa Zoran, ya ngao akalaumiwa Inonga, sasa nyie kila mechi mtakuwa mnatafuta kichaka cha kufichia madhaifu yenu?

Mlikuwa mnasema Juma Mgunda atainyoosha Yanga kwakuwa alipata sare moja ya nusu fainali kule Arusha, nikawauliza kabla ya mechi wanipe rekodi za Mgunda mara ya mwisho kuifunga Yanga ilikuwa ni lini wakaja na stori za hii ni Simba siyo Coast Union, nikasema sawa.

Hiyo Simba mara ya mwisho kamfunga Yanga lini wakaangaliana kama walioshikwa ugoni, nikawaambia rekodi zote zinawakataa. Jeuri ya kumfunga Yanga kwa sasa haipo kwenu hata mkatafute kocha chini ya bahari hamuwezi kumfunga Yanga.

Huyo Mgunda kwenye mechi 6 alizokutana na Yanga kaambulia sare mbili, nyingine kabutuliwa ndiyo mlitegemea leo awape ushindi mbele ya Yanga?

Kama siyo kurusha lawama kwa Okrah mngefanya nini? Viongozi wenu hawajampa mkataba, walikuwa wanategeshea hii mechi waone kama atapata matokeo ndiyo wampe Ukocha Mkuu. Lakini naona ngoma imekuwa nzito, ameshindwa kuutafuna mfupa uliowashinda makocha wengi. Inabidi sasa atafutwe Kocha Mkuu na yeye awe msaidizi, matunguli ya Kitanga yamekwamia bagamoyo.

Sasa kichaka kimoja kilichobaki kufyekwa watu waishiwe hoja ni mechi za kimataifa, na chenyewe kitafyekwa karibuni na hapo mashabiki uchwara wataibua jipya la hatumtaki Mo badala ya Mgunda na Matola.
 
"iyo simba mara ya mwisho kamfunga yanga lini wakaangaliana kama walioshikwa ugoni, nikawaambia rekodi zote zinawakataa jeuri ya kumfunga yanga kwa sasa haipo kwenu ata mkatafute kocha chini ya bahari amuwezi kumfunga yanga, uyo Mgunda kwenye mechi 6 alizokutana na yanga kaambulia sare mbili nyingine kabutuliwa ndo mlitegemea leo awape ushindi mbele ya yanga?"

[emoji115][emoji115][emoji1787][emoji1787]
 
Jamaa uwa wakipata sare hatupumui, Yaani Wana amini kabisa Kwa kikosi walichonacho wanaweza kuifunga Yanga!!

Safarihii Tff walianza na Morrison, Simba nao wakajiongeza Wakaja na Refa Kayoko lakini wamepata Sare.

Tunatarajia kitendo Cha Chama ku mkanyaga Kwa maksudi Aucho kamati ya massa sabini na mbili watachukua hatua stahiki kama ilivyokua kwa Morrison.

Hongera Refa, umekunja mtonyo wako ila bahatimbaya timu iliyokua uki ibebeba uwezo wao ndio umeishia hapo.
 
Huu ni utopolo mtupu halafu umeandika kwa maumiv makali bila kuacha nafasi.

Akili za kukalia nyuma mwiko
 
Jiwe gizani [emoji4]
.
JamiiForums1521774106.gif
 
Jamaa uwa wakipata sare hatupumui, Yaani Wana amini kabisa Kwa kikosi walichonacho wanaweza kuifunga Yanga!!

Safarihii Tff walianza na Morrison, Simba nao wakajiongeza Wakaja na Refa Kayoko lakini wamepata Sare...
Ifike hatua yanga muachane na simba komaeni na wakina al hilal ndio level zenu si ndio?
 
Jamaa uwa wakipata sare hatupumui, Yaani Wana amini kabisa Kwa kikosi walichonacho wanaweza kuifunga Yanga!!

Safarihii Tff walianza na Morrison, Simba nao wakajiongeza Wakaja na Refa Kayoko lakini wamepata Sare...

Hapa hata wenzako wanakuona kama hamnazo vile.

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Maelezo meeengi pumba tupu kumbe nawewe unalalamika,rubbish
Leo hii analaumiwa okrah, mechi iliyopita alilaumiwa zolan, ya ngao akalaumiwa inonga, sasa nyie kila mechi mtakuwa mnatafuta kichaka cha kufichia madhaifu yenu? Mlikuwa mnasema juma mgunda atainyoosha yanga kwakuwa alipata sare moja ya Nusu fainali kule Arusha nikawauliza kabla ya mechi wanipe rekodi za mgunda mara ya mwisho kuifunga Yanga ilikuwa ni lini wakaja na stori za hii ni Simba sio Coast Union nikasema ok, hiyo simba mara ya mwisho kamfunga yanga lini wakaangaliana kama walioshikwa ugoni, nikawaambia rekodi zote zinawakataa jeuri ya kumfunga yanga kwa sasa haipo kwenu hata mkatafute kocha chini ya bahari amuwezi kumfunga yanga, uyo mgunda kwenye mechi 6 alizokutana na yanga kaambulia sare mbili nyingine kabutuliwa ndo mlitegemea leo awape ushindi mbele ya yanga?

Kama sio kurusha lawama kwa okrah mngefanya nini? Viongozi wenu awajampa mkataba walikuwa wanategeshea hii mechi waone kama atapata matokeo ndo wampe ukocha mkuu lakini naona ngoma imekuwa nzito ameshindwa kuutafuna mfupa uliowashinda makocha wengi inabidi sasa atafutwe kocha mkuu na yeye awe msaidizi matunguli ya kitanga yamekwamia bagamoyo, Sasa kichaka kimoja kilichobaki kufyekwa watu waishiwe hoja ni mechi za kimataifa na chenyewe kitafyekwa soon na hapo mashabiki uchwala wataibua jipya la hatumtaki Mo badala ya Mgunda na Matola
 
Jamaa uwa wakipata sare hatupumui, Yaani Wana amini kabisa Kwa kikosi walichonacho wanaweza kuifunga Yanga!!

Safarihii Tff walianza na Morrison, Simba nao wakajiongeza Wakaja na Refa Kayoko lakini wamepata Sare.
Tunatarajia kitendo Cha Chama ku mkanyaga Kwa maksudi Aucho kamati ya massa sabini na mbili watachukua hatua stahiki kama ilivyokua Kwa Morrison.
Hongera Refa, umekunja mtonyo wako ila bahatimbaya timu iliyokua uki ibebeba uwezo wao ndio umeishia hapo.
Huu uloundika Si ndo ukilaza wenyewe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"iyo simba mara ya mwisho kamfunga yanga lini wakaangaliana kama walioshikwa ugoni, nikawaambia rekodi zote zinawakataa jeuri ya kumfunga yanga kwa sasa haipo kwenu ata mkatafute kocha chini ya bahari amuwezi kumfunga yanga, uyo mgunda kwenye mechi 6 alizokutana na yanga kaambulia sare mbili nyingine kabutuliwa ndo mlitegemea leo awape ushindi mbele ya yanga?"

[emoji115][emoji115][emoji1787][emoji1787]
Hiyo yanga mara ya mwisho kuingia makundi ilikuwa hujazaliwa yaani 1998
 
Jamaa uwa wakipata sare hatupumui, Yaani Wana amini kabisa Kwa kikosi walichonacho wanaweza kuifunga Yanga!!

Safarihii Tff walianza na Morrison, Simba nao wakajiongeza Wakaja na Refa Kayoko lakini wamepata Sare.
Tunatarajia kitendo Cha Chama ku mkanyaga Kwa maksudi Aucho kamati ya massa sabini na mbili watachukua hatua stahiki kama ilivyokua Kwa Morrison.
Hongera Refa, umekunja mtonyo wako ila bahatimbaya timu iliyokua uki ibebeba uwezo wao ndio umeishia hapo.
Huu sasa sio upenzi wa mpira wala kuujua mpira ila ni ushabiki mandazi, mpira mtasubiri sana,

Hivi makundi mwisho wetu kuingia ilikuwa mwaka gani ama malengo yenu ni kuifunga Simba tu na hapo ndio kipimo chenu cha ubora?
 
Back
Top Bottom